Na
Khamis Salum
TUME
ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), inakusudia kufanya kazi ya uchunguzi wa idadi, majina na mipaka ya
majimbo ya uchaguzi Zanzibar, katika kipindi cha miezi sita ijao.
Hayo
yalibanishwa na Mwenyekiti wa ZEC, Jecha Salim Jecha, katika mkutano na wadau
wa uchaguzi uliofanyika jana hoteli ya Grand Palace, Malindi mjini Unguja.
Alisema,
kazi hiyo itaendeshwa kwa matakwa ya katiba na inaelekezwa kufanyika katika kipindi cha kila baada ya miaka minane hadi 10.
Mara
ya mwisho kazi hiyo ilifanywa na ZEC mwaka 2005.
Jecha,
alisema historia ya Zanzibar inaonesha
kazi ya uchunguzi wa idadi, majina na mipaka ya majimbo ya uchaguzi visiwani hapa
inafanywa kila baada ya kipindi
maalum kama inavyoelekezwa katika sheria.
"Jambo hili limeshatokea tangu miaka ya 1957, 1961 na 1963 wakati
visiwa vyetu vilipoanzisha utaratibu wa kuchagua viongozi wake kwa njia ya
uchaguzi," alisema.
Aidha,
alisema, kazi kama
hizo zimeshaendeshwa mara mbili na ZEC
mwaka 2000 na 2005.
Alisema, hivi sasa ni miaka tisa tangu Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar ilipofanya uchunguzi wa idadi, mipaka na majina ya majimbo ya
uchaguzi Zanzibar na sheria hiyo inaelekeza
kuwa kazi hiyo inaweza
kufanyika katika kipindi cha miaka minane
hadi miaka 10.
Alieleza,
kwa maelekezo hayo, hesabu zinaonesha kuwa hivi sasa tayari Tume imeshachelewa kuifanya kazi hiyo
kwa mwaka mmoja, hivyo upo mwaka mmoja wa kuifanya kazi hiyo, vyenginevyo
itakuwa imekiukwa maelekezo ya katiba.
Alisema,
uamuzi wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar kupanga kuifanya kazi hiyo katika kipindi
hichi, unatokana na matakwa ya katiba.
Aliseka
kazi hiyo tayari imepangiwa utaratibu
wake na ZEC na utekelezaji wake utaanza rasmi mwezi huu na kuendelea mpaka mwanzoni mwa 2015.
Mwenyekiti
huyo, alisema, pamoja na kazi hiyo kusimamiwa
na kutekelezwa na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar kisheria, utendaji
wake mpaka kufikia maamuzi umepangwa
kuwashirikisha watu wote katika jamii ya Wazanzibari.
"ZEC
inategemea kwa kiasi kikubwa kupata maoni yenu juu ya hali halisi ya majimbo ya uchaguzi ilivyo
hivi sasa katika wilaya mbali mbali Unguja na Pemba,” alisema.
Alisema,
ili kupata maoni hayo, ZEC imeandaa utaratibu wa kukusanya maoni juu ya majimbo kwa utaratibu mzuri ambao
utatoa fursa kwa wadau wote kuchangia.
Hata
hivyo, alisema, kwa taasisi au watu ambao hawatapata kutoa maoni ana kwa ana mbele ya Tume ya
Uchaguzi juu ya idadi, majina na mipaka ya majimbo ya uchaguzi, wanaweza kutoa
maoni hayo kwa maandishi.
Mkurugenzi
wa ZEC,Salum Kassim Ali, alisema, kumekuwepo na changamoto mbali mbali juu ya
hilo, ikiwemo kutojulikana mipaka, ukubwa wa majimbo na idadi ya watu.
Alisema,
kazi hiyo itafanyika kwa uweledi mkubwa kwa kushirikiana na taasisi nyengine
ikiwemo Wizara ya Tawala za Mikoa, Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali na Idara
ya Upimaji na Ramani.
Hivyo,
aliwataka wananchi kutoa kila aina ya ushirikiano kwa ZEC katika kufanikisha
zoezi hilo muhimu kwa maendeleo ya taifa.
Mapema
wakichangia mkutano huo, baadhi ya wajumbe waliishauri ZEC kujipanga vyema
kuhakikisha zoezi hilo linakwenda kwa amani na utulivu kwa wananchi.
Naibu
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Zanzibar, Vuai Ali Vuai, aliitahadharisha
ZEC kuwa makini na namna wananchi watakavyoshirikishwa katika zoezi hilo ili
kuepuka vurugu zinazoweza kujitokeza na kuharibu dhamira njema ya zoezi hilo.
itasaidia kuleta maendeleo
ReplyDelete