Habari za Punde

Mdahalo wa Rasimu ya Katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mwenyekiti wa Mdahalo wa kuhusu Rasimu ya Katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania  ambaye Mjumbe Mstaaf wa Tume ya Marekebisho ya Katiba Tanzania Mhe. Mohammed Yussuf, akizungumza katika mdahalo huo ulioandaliwa na Zanzibar Institute for Research and Public Policy  kwa ufadhili wa Taasisi isiyo ya kiserekali ya The Foundation for Civil Society Tanzania, uliofanyika katika ukumbi wa Taasisi ya Lugha za Kigeni Vuga Zanzibar.  
Mgeni rasmin Mzee Hassan Nossor Moyo akitowa hutuba ya ufunzuzi wa Mdahalo la kujadili Rasimu ya Katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, iliofanyika katika ukumbi wa Taasisi za lugha za kigeni Vuga Zanzibar na kuhudhuriwa na wananchi mbalimbali Zanzibar.  
Washiriki wa Mdahalo wa Rasimu ya Katiba wakimsikiliza Mzee Moyo akizungumza katika mdahalo huo uliofanyika katika ukumbi wa Taasisi ya lugha za kigeni Vuga Zanzibar. 

                                                   Wananchi wakifuatilia mdahalo huo

Mshiriki wa Mdahalo huo Mzee Enzi Talib akichangia mada katika Mdahalo huo uliofanyika ukumbi wa Taasisi za lugha za kigeni Vuga. 

Mjumbe Mstaafu wa Tume ya Marekekebisho ya Katiba Tanzania Mhe. Ali Saleh akitowa ufafanuzi wa jambo wakati wa kujibu michango ya Wananchi walioshiriki mdahalo huo.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.