Habari za Punde

Maalim Seif Atembelea Masoko ya Bidhaa Zenj.

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, akiulizia bei ya samaki, akiwa katika ziara yake ya kutembelea masoko ya manispaa ya Zanzibar.
Mfanyabiashara wa muhogo na majimbi, akitoa bei ya bidhaa hizo wakati Maalim Seif alipofanya ziara ya kutembelea soko la Mwanakwerekwe, katika soko hilo bei ya majimbo kwa fungu shilingi 2000/= na 5000/=
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, akiangalia biashara ya mitumba katika kituo cha biashara Saateni, akiwa katika ziara yake ya kutembelea masoko ya manispaa ya Zanzibar.

Mfanyabiashara wa soko la matunda Mombasa, akimkabidhi boga Maalim Seif kwa ajili ya futari, wakati alipotembelea soko hilo.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, akiulizia bei ya samaki na pweza katika soko la darajani, akiwa katika ziara yake ya kutembelea masoko ya manispaa ya Zanzibar.(Picha na Salmin Said OMKR)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.