Habari za Punde

Bustani ya Forodhani ni Pahala Mwanana Pa Kupumzikia Zanzibar.

Na Waandishi Wetu ZJMC. Zanzibar.
Unaweza kustaajabu na namna ya kipekee isiyomithilika, mandhari yake hutoa taaswira ya rangi ya dhahabu kila jua linapozama, huku mvumo wa mawimbi ya maji yenye kuchanua, yakigonga ukingoni mwa bahari ya hindi katika bustani ya Forodhani.

Bustani ya Forodhani ni bustani ambayo inapatikana katika kisiwa cha Unguja maeneo ya mji mkongwe, ambapo watu tofauti hufika kutokana na mandhari nzuri ya eneo hilo.

Uzuri wa mandhari hiyo ni kuzungukwa na bandari kuu ya Zanzibar, pamoja na vivutio mbali mbali vya watalii kama vile Beit-el-Ajaib, Ngome kongwe, jumba la kulelea watoto, pamoja na makumbusho ya kasri, hali ambayo inapelekea mamia ya watu kuizuru kwa nyakati tofauti.

Kwa upande wa shughuli ambazo zinafanywa katika buastani ya Forodhani; ni pamoja na kupumzika, kustarehe, matembezi  pamoja na uuzaji wa biashara mbali mbali  za vyakula na vinywaji baridi  vyenye asili ya 
Zanzibar vyenye kusisimua, ni miongoni mwa vivutio vinavyopatikana katika eneo hilo.

Licha ya kuwa na maeneo ya kupumzika pia  bustani ya Forodhani ina sehemu tofauti zikiwemo sehemu ya kucheza watoto  na kuogelea baharini.

 Vile vile bustani ya forodhani ina sehemu nzuri kwa ajili ya biashara ambayo hupatikana vyakula vya aina mbali mbali vyenye mvuto wa kipekee kama vile Zanzibar pizza, chipsi kuku,urojo wa kizanzibar, Vyengine ni mashelisheli ya kukaanga,mihogo,bila ya kusahau vyakula yva baharini(sea foods) kama vile chaza,kaa, pweza na samaki wa aina mbali mbali walioungwa kwa viungo maridhawa.

Kwa upande wa wafanya biashara, makala haya ilibahatika kuongea na ndugu Said Ali Mwinyi ambaye ni muuza vyakula vya baharini(sea food) na alieleza kuwa, anafurahishwa na kupata fursa ya kufanya biashara katika eneo la bustani ya Forodhani kutokana na wageni wengi kupendelea kununua vyakula vya aina hiyo.

Aidha aliendelea kusema kiasi cha faida ni elfu thamanini huzipata ndani ya siku za jumamosi na jumapili kutokana na wageni pamoja na wenyeji wengi hutembelea bustani hiyo ndani ya siku hizo.


Hata hivyo bibi Raiyani Khamis Ali, ambaye ni mkaazi wa Tunguu, hupendelea kuwepo siku ya jumamosi na jumapili, ili aburudike na ladha tamu ya urojo wa kizanzibar na kuwatembeza watoto wake ambao hufurahishwa zaidi na kuwepo utulivu, na mandhari ya bahari pamoja na sehemu maalumu ya kufurahishia watoto.

 Vijana wengi kutoka sehemu mbalimbali za  ng`ambu na mjini hufika katika eneo hilo kustarehe  na kuogelea ukingoni mwa bustani hiyo.

“Unajua nini? nimekuja hapa kwa ajili ya kupast time then nakumbukia mandhari ya home Nungwi,” hayo ni maneno ya ndugu Hajji Ali Hajji, mkaazi wa Mwembe makumbi, wilaya ya Mjini   akimaanisha kuvutika na mandhari ya bustani ya Forodhani, baada ya kuhojiwa na waandishi wa makala haya.

Katika bustani hii, wageni  wanaopenda sana kutembelea ni wataliano,ambpoi ni kutokana na kuwepo urahisi wa usafiri wa ndege ya moja kwa moja kutoka Italy hadi Zanzibar.

Hivyo, wanapofika ndani ya Zanzibar hupenda kuizuru bustani ya Forodhani kutokana na kuwepo kwa mandhari nzuri na kupatikana vinywaji mbali mbali vyenye asili ya Zanzibar na vyenye kusisimua.

Miongoni mwa vinywaji wnavyopendelea zaidi wakiwa katika bustani hiyo ni juisi ya miwa ambayo ina ladha nzuri ya asili na ni maarufu kwa wakaazi wa Zanzibar.

Sambamba na hayo bwana Dickson Michael, raia wa Ujerumani, alisema hupendelea kuwepo ndani ya bustani ya Forodhani nyakati za kuzama jua kwa lengo la kuiangalia na kutathmini mabadiliko ya jua hilo wakati linapozama.

 Bwana Bonifex Charles ambaye ni raia wa Italia amesema anapenda kuwepo katika mandhari ya mwambao wa bahari hasa wakati wa jioni, hivyo akiwa ndani ya mji wa Zanzibar hupendelae kuwepo katika bustani ya Forodhani, kwani ni sehemu  nzuri ya mapumziko.

Akizungumza na waandishi wa makala  haya Bwana Captain Rabbot ambaye ni raia  wa Afrika  Kusini aliyefika katika bustani hiyo, alisema amefika hapo ili kustarehe na kuangalia tamaduni za watu wa aina mbalimbali.

 Alisema anafurahishwa na bei za vyakula vinavyouzwa hapo, kutokana na utofauti wa bei na nchi aliyotoka.

Sambamba na hayo mamlaka ya mji mkongwe hujaribu kuifanya mpya bustani hiyo kila siku kwa kuratibu mambo mbali mbali kama vile usafi wa mazingira, utunzaji wa nyasi, pembea na mambo mbali mbali ya kufurahishia watoto, ambapo watoto wengi hupedelea kufika hapo ili kufurahika na huduma hizo.

“Nikwambie kitu watu ambao wamewahi kuja wakapata huduma nzuri pale, wameendelea kuwa  ni mabalozi wazuri katika nchi zao,”   alisema   ndugu Mussa Awesu Ameir, ambae ni mhandisi wa mji mkongwe  Zanzibar,  wakati akizungumza na mmoja wa waandishi wa makala haya.

Ndugu Mussa alisema kwamba, bustani ya Forodhani hupendelewa kutembelewa na watalii na watu mbali mbali nyakati za usiku mwepesi, ambapo huvutiwa na huduma zinazoendeswa chini ya uongozi wa mamlaka ya mji mkongwe  Zanzibar.

Aidha ndugu Mussa aliendelea kusema kuwa mara nyingi hupata fursa ya kuagiziwa vyakula mbali mbali ambavyo vinauzwa ndani ya bustani ya Forodhani na kupelekwa nje ya nchi.

Hali hii husababishwa na wageni wengi kutembelea na kujionea vyakula mbali mbali vinavyouzwa hapo na kuvitangaza nchini kwao.

Bustani ya Forodhani mwanzoni ilikuwa ipo katika usimamizi wa baraza la mji (manispaa) na baada ya kufanyiwa marekebisho kwa kuboreshwa zaidi mnamo mwaka 2009,hapo ikawa chini ya usimamizi wa mamalaka ya mji mkongwe kwa kuratibu shughuli zote zinazoendelea hadi sasa.

Forodhani Park hakika pahali mwanana pa kupumzika.tembele kujisijia raha.


 PREPARED BY; HAMAD SULEIMAN SHAABAN
                            SITI ALI SALIM
                            MWANAPILI KOMBO FASIHI
                            MWIABA KOMBO FASIHI
                            KHATIB KHAMIS ALI
                            ZENA ABDALLA ALI
 QUESTION:  TO WRITE FEATURE ABOUT                                                           FORODHANI PARK.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.