Habari za Punde

Kampuni ya simu ya Zantel yatoa msaada wa shilingi milioni 20/- kwa watoto wenye ulemavu wa macho wa shule ya msingi Kisiwandui Unguja.

Mkurugenzi Mkuu wa Zantel, Benoit Janin akisaini barua ya kampuni ya Zantel kwa ajili ya kuanza kulisaidia  darasa la walemavu wa uoni wa shule ya msingi Kisiwandui ambapo pia walikabidhi msaada wa jumla ya shilingi milioni 20. Waanaotazama kutoka ulia ni Mwalimu Mkuu wa Shule ya Kisiwandui, Bi Taifa Ahmed, akifuatiwa na Mkurugenzi wa Elimu, Bi Safia Ali, na mwisho kushoto ni Shinuna Kassim, Mkurugenzi wa Mipango ya Biashara wa Zantel.
Mkurugenzi wa Elimu, Bi Safia Ali akizungumza wakati wa hafla ya kupokea msaada wa jumla ya shilingi milioni 20 kutoka kwa kampuni ya Zantel kwa ajili ya kununulia vifaa vya wanafunzi wa ulemavu wa macho.
Mkurugenzi wa Zantel, Benoit Janin akizungumza wakati wa hafla ya kupokea msaada wa jumla ya shilingi milioni 20 kutoka kwa kampuni ya Zantel kwa ajili ya kununulia vifaa vya wanafunzi wa ulemavu wa macho.
Mkurugenzi Mkuu wa Zantel, Benoit Janin akimkabidhi, mwalimu mkuu, Bi Taifa Ahmed mfano wa hundi ya shilingi milioni 20 kwa ajili ya kununua vifaa vya wanafunzi wenye ulemavu wa uoni wa shule ya msingi Kisiwandui.
Mkurugenzi Mkuu wa Zantel, Benoit Janin akisaini barua ya kampuni ya Zantel kwa ajili ya kuanza kulisaidia  darasa la walemavu wa uoni wa shule ya msingi Kisiwandui ambapo pia walikabidhi msaada wa jumla ya shilingi milioni 20. Waanaotazama kutoka ulia ni Mwalimu Mkuu wa Shule ya Kisiwandui, Bi Taifa Ahmed, akifuatiwa na Mkurugenzi wa Elimu, Bi Safia Ali, na mwisho kushoto ni Shinuna Kassim, Mkurugenzi wa Mipango ya Biashara wa Zantel. 
 Mkurugenzi Mkuu wa Zantel, Benoit Janin akimkabidhi, Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo, Bi Taifa Ahmed barua inayoonyesha nia ya kampuni ya Zantel kusaidia shule ya Kisiwandui. Anayetazama katikati ni Mkurugenzi wa Elimu, Bi Safia Ali. Zantel pia walikabidhi shilingi milioni 20 kwa ajili ya kununua vifaa vya walemavu wa uoni.
Mwanafunzi, Mbarouk Nassor akitoa shukrani kwa kampuni ya Zantel baada ya kupokea msaada wa shilingi milioni 20 kwa ajili ya kununua vifaa vya kuwasaidia kusoma.
Uongozi wa kampuni ya Zantel pamoja na walimu na wanafunzi wa shule ya Kisiwandui katika picha ya pamoja baada ya kupokea msaada wa shilingi milioni 20 kwa ajili ya kununua vifaa vya walemavu wa uoni wa shule hiyo.

Na Mwandishi Wetu.
Kampuni ya simu ya Zantel leo imetoa msaada wa shilingi milioni 20 kwa wanafunzi wenye ulemavu wa macho wa Shule ya Msingi Kisiwandui iliyopo Ugunja kwa ajili ya kununua vifaa vitakavyo wasaidia wanafunzi hao wawapo  shuleni.

Akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano, Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Zantel, Benoit Janin alisema vifaa hivyo ni sehemu ya mkakati wa  kampuni ya Zantel katika  kuhakikisha kuwa kila mtanzania anapata elimu bora bila kujali tofauti zao.

‘Wajibu wetu kama wanajamii ni kuhakikisha kuwa watu wenye ulemavu wanapata msaada kama ilivyo kwa watu wengine na pia kuweza kuwaanda  kwa ajili ya kuweza kufikia malengo yao kama walivyo kusudia’ alisema Benoit.

Vifaa hivyo vipya ni sehemu ya jitihada za kampuni ya Zantel kwa ajili ya kushughulikia mahitaji ya elimu kwa wanafunzi wenye  walemavu ili kuhakikisha wanapata elimu bora kama ilivyo kwa wanafunzi  wasio na ulemavu .

‘Kama sehemu ya jamii tumedhamiria kuwasaidia wanafunzi wenye ulemavu kwa kuwapatia vifaa wanavyovihitaji ili kuwasaidia kupata elimu bora, na kuanzia leo tutalichukua darasa hili kuendelea kuwasaidia mahitaji mengine’ alisema Benoit.

Naye Mkuu wa  Shule hiyo, Bi Taifa Ahmed, alitoa shukrani za dhati kwa Zantel kwa ukarimu wao  na kusema kuwa msaada huo ni wa kipekee na utarahisisha ufundishaji kwa wanafunzi hao, na hivyo kupelekea wanafunzi hao kupata elimu bora kama ilivyo kwa wengine wasio na ulemavu.

‘Tunawashukuru Zantel kwa kuziona changamoto tulizokuwa tunakabiliana nazo, na hakika kwa msaada huu utatatusaidia katika kuwafundisha wanafunzi hawa na pia kuwawezesha  kufikia malengo yao ' alisema Bi Taifa.

Katika hatua nyingine, Mwalimu Taifa aliongeza kwa kusema kuwa wanafunzi wenye ulemavu ni wanafunzi wa kawaida kama wanafunzi wasio na ulemavu hivyo wakiwezeshwa wanaweza kushika nafasi  yoyote katika jamii.

Shule ya msingi Kisiwandui ilianzishwa mwaka 1991, na mpaka sasa wanafunzi 199 wamepitia shuleni hapo.


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.