Habari za Punde

Nani anafaidika na rasilimali za Tanzania?















Mwandishi wa makala hii Muhamed Khamis akizungumza 

na chifu wa kabila la kimasai katika kata ya idodi wilaya ya 

Iringa vijijini Chif Lameck mtemisika.


Na  Mohammed khamis 

University of Iringa (UoI)

0652729061

Tanzania ni miongoni nchi chake 

katika bara la Africa  iliojaaliwa kuwa na vivutio vingi vya 

utalii.Tofauti na nchi nyengine nyingi za Africa na hata 

dunia kwa jumla.miongoni mwa vivutio hivo vya utalii nchini 

Tanzania ni mbuga za wanyama.

Katika mkoa wa Iringa ambao unapatikana nyanda za juu 

kusini mwa Tanzania umejaliwa kuwa na mbuga ya 

wanyama ‘Ruaha Nationa park’mbuga hii ipo magharibi mwa 

Iringa katika kijiji cha tunga malenga kata ya Idodi kilimota 

128 kutoka Iringa mjini.

Mbuga hii ni ya kipekee yenye wanyama wa kila aina na 

adimu kupatikana kuonekana sehemu nyengine 

ulimwenguni wanyama hao ni kama vile ‘kadu’ni aina ya 

wanyama ambao kisura wameshabihiana sana na swala 

lakini sio swala na ndio maana mwandishi wa makala hii 

anasema mbuga hii ni ya kipekee, Kijografia mbuga hii ya 

Ruaha imepakana na mikoa kadhaa ya Tanzania,miongoni 

mwa mikoa hio ni singida,Dodoma,mbeya na ina ukubwa wa 

kilomita za mraba 1300.

Wakaazi wa kijiji cha karibu na eneo 

hili’tungamalenga’wameleza kusikitishwa kwao licha ya 

uwepo wa kivutio kikubwa cha wageni lakini kwa upande 

wao wanaeleza hawafaidiki na lolote lile kupitia mbuga hio.

Kwa nyakati tofauti wakizungumza na mwandishi wa makala 

haya walisema uwepo wa mbuga hio kwao ni kama mzigo 

kwani haina faida kwao,bali ni  hasara inayotokana na 

wanyama hao kwa vipando vyao mashambani.

Wamesema haina faida kwa sababu hakuna kijana hata 

mmoja kutoka maeno hayo ambae ameajiriwa badala yake 

huajiriwa zaidi wageni kutoka mikoa mengine jambo ambalo 

linawalenga kuona uwepo wa mbuga hio ni kama mzigo na 

faida kwa wageni.

Mwenyekiti wa serikali ya kijiji hicho Bwana Silasi 

mgeza  alisema tokea kuanza  uongozi wake takribani 

mwaka mmoja sasa hajawahi kuskia wala kuona uwepo wa 

ajira kwa vijana wake bali anachokijua yeye wanaoajiriwa 

wote ni wageni wa eneo hilo.

Alisema hio ni changamoto kubwa kwa wanakijiji hicho 

kwani matumaini yao waliamini uwepo wa mbuga hio 

wangeweza kuajiriwa vijana wao lakini hali ni kinyume na 

ndio maana wanasema mbuga hio ni mzigo kwao.

‘’licha ya uwepo wa kivutio hichi lakini hadi barabara  hii ni 

mbovu nadhani umeona ndugu mwandishi wakati unafunga 

safari ya kuja kijijini hapa’’alieleza mwenyekiti huyo.

Licha ya tatizo hili la barabara lakini pia suala la elimu bado 

kabisa miundombinu mibovu katika suala la elimu katika kijiji 

hichi,wananchi waliamini uwepo wa secta hii ya utalii kwa 

kiasi kikubwa ungesaidia secta hii ya elimu kwa kiasi 

kikubwa ikiwa ni kujenga skuli ya kileo na kusaidia 

kupatikana kwa walimu.

Rashid Salehe ni mwanafunzi aliehitimu kidato cha nne kwa 

sasa anasubiri matokeo yake alisema anashangazwa hadi 

leo hii shule yao ni mbovu huku kukiwa na uhaba mkubwa 

wawalimu shuleni hapo,anaamini iwapo mbuga za wanyama 

zingetumiwa vyema zingewasaidia wanafunzo mashuleni 

kusoma katika mazingira bora.

Alieleza tayari amemaliza kidato cha nne lakini hana imani 

kama anaweza kufaulu kutokana na ukosefu wawalimu 

waliokuwa nao jambo ambalo linamkatisha matumaini 

makubwa alikuwa nayo ya kufika chuo kikuu.

Aliamini kupitia waandishi wa habari kufichua 

yanayowakabili kijiji kwao hwenda siku moja kijiji hicho 

kikapiga hatua kimaendeleo kama vijiji vyengine Tanzania.

‘’Wakati mwengine natamani hata kuwalaumu wazazi wetu 

ni kwanini walikubali uwepo wa hifadhi hii bila kutoa 

masharti maalumu,angalia sasa watoto wao tunafeli kwa 

kukosa walimu huku watoto wa wengine wanasoma vizuri 

kupitia rasilimali zetu’’alieleza Rashid.

Tukizungumzia suala la afya katika kijiji hichi nalo pia 

limeonekana kuwa mtihani mkubwa mwenyekiti wa serikali 

ya kijiji cha Tungamalenga alinileza wana uhaba mkubwa 

wa madaktari hospitalini hapo,jambo ambalo linawawia 

vigumu sana kina mama wanaotaka kujifungua .

‘’Wake zetu wanalazimika kujifungulia Iringa mjini jambo 

ambalo ni shida sana kutoka hapa mpaka Iringa mjini ni 

karibu masaa manne,hali hii inaweza hata kupelekea kufariki 

dunia wakati mwengine ukizingatia njia mbovu tulionayo 

alinieleza mwenyekiti huyo.

Wahusika wakuu wa suala hili ni kina mama nao hawakuwa 

kimya walipaza sauti zao wakati wakizungumza na 

mwandishi wa makala hii ingawa hawakupenda kutajwa 

majina yao kwa kuhofia kile kilichowakuta wenzao mwaka 

jana ambapo walitoa taarifa kwa moja ya chombo cha habari 

na wakapata matatizo makubwa kijijini hapo ingawa 

hawakuwa tayari kueleza matatizo hayo.

Waliniambia changamoto kubwa wamekuwa wakizipata 

wanapokwenda hospitali ya kijiji hicho ambacho dawa ni 

kwa uchache sana lakini pia uhaba wa wauguzi hospitalini 

hapo.

‘’Tunaiomba Serikali ichukue tatizo hili tukiwa kama 

wananchi wa Tanzania ambao tunahitaji msaada wa 

kutatuliwa changamoto zetu’’walieleza kina mama hao kwa 

nyakati tofauti.

Wakazi wengi wa kijiji hichi cha tungamalenga ni wakulima 

na wafugaji ingawa yapo makabila kadhaa yanayoishi 

hapa,mwandishi wa makala hii alizungumza na mwenyeti wa 

kijiji na kuelezwa makabila hayo ni wahehe,wangoni,wamasa

i na nk.

Kwa nyakati tofauti baadhi ya kina mama ambao 

wanajishughulisha na shughuli za kilimo walinieleza 

wanatamani angalau kupatiwa nyezo za kilimo chao ili 

watimize ndoto zao siku moja kuwa wakulima bora kama 

walivo wengine.Walieleza wanatamani kuona angalau 

uwongozi wa mbuga ya wanyama katika kijiji hicho 

wanawapa kipaombele zaidi kutoka na shida walizonazo.

‘’Chakushangaza hawajali kabisa hata jitihada zetu na ndio 

maana wanyama wao wanakuja hapa kila mda kuharibu 

mazao yetu na wanajua kila kitu hatuna 

lakuwafanya’’walieleza kina mama hao.

Jitihada za mwandishi wa makala hii zilikwenda mbali zaidi 

kwa kufanikiwa kuonana na mmoja miongoni mwa walinzi 

wa mbuga hio ambae hakupenda kutajwa jina lake kwenye 

makala hii alisema ni kweli wananchi wa kijiji jirani hakuna 

hata mmoja anaefanya kazi hapa(Tungamalenga).

Alisema wakuu wa sehemu hio wamekuwa wakitumia 

kigenzo cha elimu katika ajira zao jambo ambalo ni 

changamoto kubwa kwa wakaazi wa hapo ingawa wapo 

wachache waliosoma lakini pia hawakuajiriwa.

Mlinzi huyo alieleza kuskitishwa kwake na utaratibu huo 

ingawa yeye pia si miongoni mwa wananchi wa kijiji hicho 

lakini alidai anaona uchugu zaidi kuona hakuna hata mtu 

mmoja kutoka Tungamalenga alieajiriwa ingawa nafasi ni 

nyingi zisizohitaji elimu.

‘’Zipo kazi tele hapa za kufanya kwa kutumia nguvu zaidi na 

sio akili,aina hii ya kazi haihitaji elimu sijui ni kwanini uongozi 

wa hapa unabaguwa katika ajira’’alieleza mlinzi huyo kwa 

masikitiko.

Kuhusiana na suala la mapato yanayotokana na mbuga hio 

mlinzi huyu alisema hana uhakika juu ya matumizi yake 

sahihi ingawa anaamini ni lazima ubadhilifu uwepo 

kutokana na hali halisi ilipo mbugani hapo na Tanzania kwa 

ujumla.

Upande wa pili kwa wakaazi wa kijiji hichi ni kutoka katika 

kabila la kimasaid ambapo mwanidishi wa makala hii 

alikutana na kiongozi wa kabila hilo kuzungumzia uwepo wa 

tatizo hili la ajira kwa vijana wa kijiji hichi.

Alisema hata wao ambao wana weledi mkubwa wa 

wanyama wamekoseshwa ajira lakini hilo haliwaumizi zaidi 

kinachowaumiza wao ni kuondolewa maeno wanayoishi kwa 

madai kupewa wawekezaji huku wamamasai wakisahauliwa 

kabisa.

‘Wametusahau kama sisi ni watanzaia kama walivowengine 

pia tunahitaji haki kama wanayopewa wawekezaji,angalia 

kundi hili la ngombe linakosa chakula sasa tumefukuzwa 

kilichobaki ni kutuletea mgogoro na wakulima kwa 

mashamba yao’’alieleza chifu lamek.

Alishauri Serikali  kupitia wizara ya mali asili Tanzania 

kuangalia upya suala la wawekezaji vyenginevyo linaweza 

kuibuwa mgogoro mkubwa zaidi hapo badae lisipochukuliwa 

hatua suala hili.

Jicho la Serikali limekuwa likiangaza zaidi kuhusiana na 

suala la ujangiri kwa wanyama pori huku wakisahau uwepo 

wa hali hio unatokana na tatizo la wananchi wenyewe 

kutokufaidika na hifadhi zao na ndio maana wamekuwa na 

maamuzi yasiosahihi kwa taifa huku wakiamini ndio njia 

peke ya kujinufaisha kupitia mali zao.

Tanzania iwapo itatumia vyema rasilimali zake zilizonazo ni 

wazi kabisa tutafika mbali kimaendeleo ikiwa tutakubali 

rasilimali hizi ziwafaidishe watanzaia wenyewe na sio 

wageni au wachache huku tukiwasahau wananchi wanaoishi 

karibu na rasilimali zao.

Naamini suala la ujangiri na mabaya yote kwa rasilimali zetu 

yataondola iwapo watanzania watakuwa miongoni mwa 

wanaofaidia kinyume na hivi sasa ambapo watanzania 

wamekuwa njia ya kuwafaidisha wachache miongoni mwao.                                                              

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.