STATE HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar
26.08.2016
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.
Ali Mohamed Shein amepongeza juhudi zinazoendelea kuchukuliwa na Serikali ya Jamhuri
ya Watu wa China na Serikali ya India katika kuendelea kuiunga mkono Zanzibar
katika kuimarisha sekta za maendeleo na kukuza uchumi wake.
Dk. Shein aliyasema
hayo wakati alipokuwa na mazungumzo na
Balozi Mdogo wa Jamhuri ya Watu wa China aliyepo Zanzibar Xie Xiaowu na Balozi Mdogo wa India Mhe. Tek
Chand Barupal kwa nyakati tofauti walipofika Ikulu mjini Zanzibar kwa ajili ya
kujitambulisha.
Katika mazungumzo yake
na Balozi Mdogo mpya wa China Xie Xiaowu
Dk. Shein alieleza kuwa uhusiano na ushirikiano mzuri uliopo kati ya Serikali
ya Mapinduzi ya Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China umeleta mafanikio
makubwa ya maendeleo ya kiuchumi pamoja na kuimarisha huduma za jamii hapa
nchini.
Dk. Shein alieleza
kuwa China na Zanzibar zinauhusiano wa muda mrefu ambao unaendelea kuimarika
siku hadi siku kutokana na nchi hiyo kuendelea kuiunga mkono Zanzibar kwa muda
wa miaka 52 hivi sasa jambo ambalo pande zote mbili zinajivunia.
Alieleza kuwa Zanzibar
inathamini sana uhusiano huo na ushirikiano kati yake na China ambao umeasisiw
na viongozi wakuu wa nchi hizo ambao ni Marehemu Mzee Abeid Amani Karume,
Marehemu Mwalimu Julius Kambarage Nyerere pamoja na kiongozi muasisi wa China
Marehemu Mao tse tung.
Dk. Shein alitumia
fursa hiyo kutoa pongezi kwa Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China kwa kuendelea
kuiunga mkono Zanzibar katika kuimarisha sekta za maendeleo zikiwemo elimu,
kilimo, afya, viwanda, miundombinu na nyenginezo huku akiipongeza nchi hiyo kwa kuimarisha uchumi wake.
Aidha, Dk. Shein
aliipongeza China kwa kuiunga mkono Zanzibar katika ujenzi wa Hospitali ya
Abdalla Mzee huko kiswani Pemba ambapo ujenzi wake unatarajiwa kukamilika hivi karibuni, ujenzi
wa jengo jipya la abiria katika kiwanja cha ndege cha Abeid Amani Karume pamoja
na ujenzi wa bandari mpya ya Mpigaduri ambapo ujenzi wake nao unatarajiwa
kuanza hivi karibuni.
Nae Balozi huyo Mdogo
wa Jamhuri ya Watu wa China aliyeko Zanzibar Xie Xiaowu alimuhakikishia Dk. Shein kuwa China
itaendelea kuiunga mkono Zanzibar kwa lengo la kuzidisha uhusiano na
ushirikiano uliopo ambao una historia kubwa.
Balozi Xie aliipongeza
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar chini ya uongozi wa Dk. Shein kwa mafanikio
makubwa yaliopatikana katika kuimarisha na kuendeleza sekta za maendeleo sambamba na kukuza uchumi Zanzibar.
Pamoja na hayo, Balozi
Xie alisema kuwa nchi yake itahakikisha inaendeleza ujenzi wa miradi yote
iliyoanzishwa hapa Zanzibar pamoja na kuendeleeza mengine mipya ikiwa ni pamoja
na kuendelea kutoa nafasi za masomo na ufadhili kwa Zanzibar pamoja na kuunga
mkono juhudi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuimarisha uvuvi wa
bahari kuu.
Wakati huo huo, Dk. Shein alifanya
mazungumzo na Balozi Mdogo wa India Tek Chad Barupal, ambapo katika mazungumzo
hayo viongozi hao walikubaliana kuendeleza uhusiano na ushirikiano wa asili
kati ya pande mbili hizo.
Katika maelezo yake
Dk. Shein alimueleza Balozi huyo kuwa Zanzibar na India zina historia kubwa
ambayo imeweza kuwafanya watu wa pande mbili hizo kukuza udugu wao hadi hivi
leo huku akisisitiza kuwa Zanzibar na watu wake wataendelea kuthamini udugu
huo.
Akielezea juu ya
ushirikiano na uhusiano kati ya India na Zanzibar, Dk. Shein alimueleza Balozi
huyo kuwa Zanzibar inathamini sana ushirikiano uliopo hatua ambayo imesaidia
kwa kiasi kikubwa kuongeza ushirikiano katika sekta mbali mbali za maendeleo
ikiwemo elimu, afya, biashara, miundombinu, huduma za kijamii na nyenginezo.
Kwa upande wa sekta ya
biashara, Dk.Shein alisema kuwa Zanzibar na India zimekuwa na uhusiano mzuri wa
kibiashara ikiwemo biashara ya karafuu na biashara nyenginezo ambapo sekta hiyo
nayo imeweza kukuza udugu huo kati ya watu wa pande mbili hizo.
Dk. Shein alitumia
fursa hiyo kutoa pongezi kwa India kwa kuendelea kuiunga mkono Zanzibar katika
sekta ya elimu ikiwa ni pamoja na kutoa nafasi kadhaa za masomo kwa Zanzibar
nchini India katika kada mbali mbali.
Dk. Shein alimueleza
Balozi huyo kuwa lengo na madhuminu ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ni
kuimarisha sekta ya viwanda vidogo vidogo sambamba na kuvifufua vile vya asili
vikiwemo viwanda vidogo vidogo vilivyopo Amani nje kidogo ya mji wa Zanzibar,
hivyo matarajiao makubwa ni kwa nchi hiyo kuweza kuiunga mkono Zanzibar katika
kufanikisha hilo.
Nae Balozi Barupal alimuhakikishia Dk. Shein kuwa India
itaendelea kuiunga mkono Zanzibar katika kuimarisha sekta zake za maendeleo
kwani inatambua na inathamini sana uhusiano na ushirikiano uliopo kati ya pande
mbili hizo.
Rajab
Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address:
2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822
E-mail:
rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment