Habari za Punde

Waziri Castico aendelea na ziara yakeya kikazi kisiwani Pemba

 WAZIRI wa Wizara ya Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Vijana, Wanawake na Watoto Zanzibar, Mhe:Maudline Cyrus Castico, akizungumza na wafanyakazi wa Idara ya Ustawi wa Jamii Pemba, juu ya kuimaliza haraka nyumba ya wazee Limbani Wilaya ya Wete, wakati alipoitembelea nyumba hiyo.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
 MMOJA wa Mafundi wanaofanya ukarabati katika nyumba ya wazee limbani Wilaya ya Wete, akiwa katika harakati zake za kikazi, pichani fundi huyo akichukuwa jipsamu kwa kwenda kupaka katika moja ya sehemu za nyumba hiyo.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
 WAZIRI wa Wizara ya Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Vijana, Wanawake na Watoto Zanzibar, Mhe:Maudline Cyrus Castico, akitoa agizo kwa Idara ya uwezeshaji kuijengea uzio nyumba ya wazee limbani Wete.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
 WAZIRI wa Wizara ya Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Vijana, Wanawake na Watoto Zanzibar, Mhe:Maudline Cyrus Castico, akikagua mipaka ya nyumba ya wazee limbani Wilaya ya Wete, wakati wa ziara yake ya siku mbili Kisiwani Pemba.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)

 BANDA la kufungia asali la kikundi cha Pemba Clove Honey lililoko Kinyasini Wilaya ya Wete, likiwa na mizinga ya nyuki kwa ajili ya kutega asali.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)

 WAZIRI wa Wizara ya Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Vijana, Wanawake na Watoto Zanzibar, Mhe:Maudline Cyrus Castico, akikagua shamba ya misan flower la kiku ndi cha Pemba Clove Honey lililoko Kinyasini Wilaya ya Wete.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
MITI ya Misan Flower ikiwa imenawiri katika shamba linalomilikiwa na kikundi cha Pemba Clove Honey kilichopo Wete.(Picha na Abdi Suleiman,PEMBA.)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.