Habari za Punde

Jumuiya ya Walemavu Zanzibar Yaipongeza VSO.


Na. Maida Hamza - MCC

Jumuiya ya watu wenye ulemavu Zanzibar imeishukuru Taasisi ya kujitolea ya kutoa huduma (VSO)  kwa kuwapatia  ufadhili wa mradi wa  kilimo cha matunda na mbogamboga .

 Mwenyekiti wa Jmumuiya hiyo Nd.Ali Omari Makame amesema Taasisi hiyo pia imewapatia  mabwanashamba kwa ajili ya kuwasaidia wakulima wanaojishughulisha na kilimlo hicho kwa lengo la kujiongezea kipato.

Ndugu Makame  ameeleza hayo wakati akizungumza na mwandishi wa habari Makao makuu ya Umoja huo Wireles Kikwajuni Mjini Zanzibar.

Amesema Umoja huo pia unaendesha programu ya kutoa taaluma  na mikopo ya fedha kwa wakulima wa mbogamboga na matunda  pamoja na wafanya biashara wadogowadogo wa maduka, mitumba, tungule, mkaa  ili kupata pesa ambazo zinaweza kuendeleza maisha yao ya kila siku

 Mwenyekiti wa Umoja wa watu wenye ulemavu ameongeza kuwa katika kuwasaidia vijana  walemavu ambao hawana   uwezo wa kujiendeleza katika  elimu ya juu wanawasidi vifaa na  fedha  ili kuhakikisha nao wanapata fursa hiyo kama wanayopata vijana wengine.

Ndugu Makame  ameishukuru Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar  kwa kuwapatia  madaktari wa  kushirikiana na maafisa wa  walemavu  vijijini   kuwatambua watoto  wenye  ulemavu na kuwapatia visaidizi.

 Ameongeza kuwa katika kuimarisha  Jumuia yao,  wameanzisha darasa la lugha za alama na  watu wote wanaopenda kushiriki  wanakaribishwa kujiunga  katika darasa hilo ili kuimarisha mawasiliano kati yao na watu wa kawaida.

Amelalamikia watu wenye ulemavu kukosa nafasi ya  kushirikishwa katika kamati za sheha na udiwani hali  inayopelekea kukosa utetezi wa  maslahi ya walemavu  katika ngazi za shehia na wadi.

Aidha amesema jumuia yao  imekuwa ikichukua hatua ya kusimamia kesi za udhalilishaji wa kijinsai kwa walemavu kwa kuandaa   taratibu  katika kutoa ushahihidi inapohitajika.

Ametoa wito kwa jamii  kuliona suala la walemavu  ni suala la wananchi na sio lao peke yao ama  taasis  zinazowasaidia  ili kujenga   jamii iliyobora   na kupunguza tofauti baina ya walemavu na wasio walemavu.


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.