Na Mwandishi wetu
Naibu katibu mkuu UVCCM zanzibar Abdullighafari Idirisa Juma amesema serikali ina mpango wa kujenga bandari mpya ya kisasa wete ili kuinuwa shughuli za kiuchumi kwa wananchi.
Ameyasema hayo huko bandarini Wete katika ziara yake ya kuangalia shughuli mbali mbali za maendeleo pamoja na matawi ya ccm ikiwa ni miongoni mwa utekelezaji wa ilani ya chama cha mapindunzi..
Amesema kukamilika kwa bandari ya wete kutatoa fursa kwa wananchi kisiwani pemba kuendeleza shughuli zao za biashara kwa uhakika .
Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Wete,Rashid Hadidi Rashid amesema shughuli za uchumi katika wilaya hiyo zinaimarika kutokana na kuwepo kwa miundombinu ya uhakika ikiwemo maji safi na salama barabara pamoja na umeme jambo ambalo linawafanya wananchi kujiimarisha kiuchumi kwa miradi mbali mbali ya kimaendeleo.
Nae Mkurugenzi wa bandari Pemba, Hamad Salim Hamad amesema tayari kumejitokeza mfanya biashara ambae anataka kuwekeza katika bandari hiyo.
No comments:
Post a Comment