NA HAJI NASSOR, PEMBA
MTU mmoja aliekuwa akiendesha Vespa ambae ni mkaazi wa
Mwambe wilaya ya Mkoani kisiwani Pemba, Juma Mohamed Juma (70), amefariki dunia
na mwengine kujeruhiwa, baada ya kugongana na gari ya abiria.
Tukio
hilo lilitokea juzi majira ya 1:30 eneo la Majenzi shehia ya Kengeja wilaya ya
Mkoani Pemba, wakati wapanda vespa huyo akitokea Mwambe kuwenda Mtambile, ndipo
walipogongana na gari hiyo ya abiria, iliokuwa ikitokea Mtambile kwenda Mwambe.
Mashuhuda
wa tukio hilo, walisema mpanda vespa ambae alifariki hapo hapo, aliacha eneo
lake na kwenda eneo lililokuwa likipita gari hiyo, na kugongana uso kwa uso.
Mashuhuda
hao walisema, mwili wa marehemu Juma, ulivurugika eneo hilo kutokana na ajali
ilivyokuwa kubwa , ingawa aliekuwa amempakiwa kwenye vespa hiyo, kijana Zaidu Khalfan Faki (25),
alipata majeraha na kukimbizwa hospitali.
“Baada
ya ajali na mzinga niliousikia kufika tu naona mwendesha vespa ameshafariki, na
baadhi ya mifupa imeganda kwenye gari, lakini mwenzake alichukuliwa baadae na
kukimbizwa hospitali kwa matibabu”,alisema shuhuda huyo.
Nae
shuhuda mwengine aliejitambulisha kwa jina moja la Mohamed, alisema yeye muda
mfupi wakati anatembea kwa miguu, alipitwa na muendesha vespa huyo kwa mwendo
usiokuwa wa kawaida.
Kamanda
wa Polisi Mkoa wa kusini Pemba, Shehan Moahemd Shehan, alisema chanzo za ajali
hiyo, kwanza ni mwendo kasi wa mwendesha vespa.
Alisema
aidha wamegundua kuwa, mpatwa na kifo hicho ambae alikuwa dereva, aliacha
sehemu anayopaswa kupita na kuifuata gari na kutokezea kwa ajali hiyo.
“Ingawa
uchunguuzi wa kina unaendelea, lakini kwa huu wa awali, basi tumegundua mambo
kadhaa yaliiopelekea kutokezea kwa ajali hiyo, likiwemo mwendesha vespa
kuifuata gari”,alieleza.
Hata
hivyo alisema bado wanamshikilia dereva ambae hakumtaja jina lake, wa gari hiyo ya abiria yenye namba za
usajili Z 464 DT namba 315, inayofanya kazi zake Chakechake-Mwambe, kwa
mahojiano zaidi.
Alifafanua
kuwa, wakati wowote taratibu zitakapokamilika atafikishwa mahakamani, kujibu
tuhuma zitakazomkabili, kutokana na ajali hiyo.
Hivyo
ametoa wito kwa madereva wa gari, waendesha vyombo vya magurudumu mawili, na
waenda kwa miguu, kuwa waangalifu wanapokuwa barabarani, kwani kila moja na
aina ya matumizi ya barabara hiyo.
No comments:
Post a Comment