Habari za Punde

Mwenge yaitumbua Chipukizi



 NA HAJI NASSOR, PEMBA

TIMU ya Mwenge ya mji wa Wete, imeivuruga Chipukizi ya mjini wa Chakechake, kwa mabao 2-0, kwenye mchezo wa ligi kuu ya Zanzibar kituo cha Pemba, kwenye ngarambe iliopigwa uwanja wa FFU.

Mchezo huo ulianza kwa kasi, na kila timu kuonyeshena ubabe wa kusakata soka, huku wakitiwa hamasa na ari kupitia wapenzi na washabiki wao, waliojazana uwanjani hapo.

Chipikuzi walionekana kuwa wazuri, kwenye eneo la katikati, hivyo kuruhusu washambuliaji wao, kufika mara kwa mara langoni mwa Mwenge, ingawa kisha mashuti yao kukosa mwelekeo.

Mwenge ukaanza kumwilika vyema, dakika ya 15 kwa bao la kuongoza, likifungwa na Abdu-l Yussuf, baada ya walinzi wa Chipukizi, kufanya uzembe na kufungwa bao bilo.

Wanaume wao waliokuwa wakiwinana vyema, walikwenda mapunziko, kwa wenyeji Mwenge, wakiwa mbele kwa bao moja kibindoni, na ngwe ya lala salama, ilianza kwa kasi mara dufu, huku timu zote, zikifanya mabadiliko.

Dakika ya 80, Mwenge walijihakikisha ushindi wa pointi tatu muhimu, baada ya mshambuliaji wake, alionekana kuitesa ngome ya Chipukizi Ali Salum, kuwapachika bao la pili.

Kwa matoke hayo, baada ya kila timu kushuka dimbani mara tatu, Mwenge ndio inayoshika usukani wa ligi kuu ya Zanzibar kwa kituo cha Pemba, kwa kujikusanyia alama tisa.

Timu nyengine zinazokabana koo, kwenye nafasi ya pili ni Younger Islanders na FSC zenye alama sita kila timu, huku timu za Okapi na New star zikiwa na pointi nne nne, wakati timu za Chipukizi, Shaba na Kizimbani zikichuuana kwa pointi tatu tatu.


Ligi kuu ya Zanzibar kituo cha Pemba, itaendelea tena leo kwa mchezo mmoja tu, baina ya Opec yenye point moja,  watakaovutana vilivyo na Kizimbani yenye point tatu, mchezo unaotarajiwa kuchezwa uwanja pekee wa FFU Finya.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.