Habari za Punde

Mhe Ayoub Alitaka Jeshi la Polisi Mkoa wa Kaskazini Unguja Kuandaa Utaratibu wa Ufuatiliaji wa Vitendo vya Udhalilishaji.

Na. Mzee George.

Kaimu Mkuu wa Mkoa Kaskazini Unguja ambae pia ni Mkuu wa Mkoa Mjini Magharibi Mhe Ayoub Mohammed Mahmoud amesema serikali imeweka mikakati maalum katika kuhakikisha wanawafichuwa waovu ikiwemo udhalilishaji.

Akizungumza na wananchi wa Wilaya ya Kaskazini ‘A’ Unguja huko katika kiwanja cha Mpira Mkokotoni wakati akiendelea na ziara yake ya kiserikali akiwa ni kusikiliza kero za wananchi zinazowakabili katika Wilaya zao.

Alisema hatua hiyo itaweza kusaidia kwa kiasi kikubwa katika kupambana na vitendo vya udhalilishaji katika Mkoa wa Kaskazini Unguja.

Alisema Mkoa huo ni mkoa miongoni mwa vitendo hivyo licha ya jitihada zinazochukuliwa na wanaharakati wa masulaya hayo ambayo mara nyingi wamekuwa wanavikemea na kuvipiga vita.

Hata hivyo aliliagiza Jeshi la Polisi Mkoa huo kulitilia mkazo suala hilo ikiwemo kufuatilia tatizo lilojitokeza hivi karibuni kwa mtoto mwenye umri wa miaka mitano kufanyiwa kitendo cha kubakwa hakiwezi kuvumiliwa ili hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa kwa haraka.
Hivyo aliwataka wananchi kushirikiana na serikali katika kuhakikisha wanakomesha vitendo hivyo ikiwemo kutoa taarifa kwa vyombo vya sheria ili kuona vitendo hivyo vinaondoka kabisa katika mkoa huo.

“Hatupendi kuona kila wakati vitendo hivi vinatajwa midomoni tu sisi linatusikitisha kupita kiasi kwani tunashangazwa kwa nini mkoa huu tu, hivyo jitihada tuzifanye ili tuweze kukomesha kabisa” alisema.

Mbali na hayo aliwataka wazazi na walezi kuwa karibu na watoto wao katika kufuatilia nyendo zao kwa lengo la kunusuru jamii na janga hili ambalo limekuwa linatishia kuharibu vijana ambao ni taifa la baadae.


Akizungumzia dawa za kulevya Mhe.Ayoub alisema anahakikisha wanafanya Operesheni maalum mkoani humo ya kukamata vikundi vyote vinavayojihusha na uuzaji na usambazaji wa dawa hizo pamoja na watumiaji wa dawa hizo kwa kuwachukulia hatua za kisheria.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.