Habari za Punde

Mwalimu Madrasa atuhumiwa kumlawiti mwanafunzi wake


NA ZUHURA JUMA, PEMBA

MWALIMU msaidizi wa madrasa Seif Said Rashid ‘denja’ (18) mkaazi wa Kiungoni wilay ya Wete, anatuhumiwa kumlawiti mwanafunzi wake, wa kiume miaka (9), wakati akiwa mtoni anakoga.

Baba mzazi wa mtoto huyo, alisema kuwa tukio hilo lilitikea Oktoba 30 mwaka huu, ambapo mtuhumiwa alimlawiti mwanafunzi wake huyo, baada ya kumkuta anakoga na kisha kumpeleka kichani, kumfanyia unyama huo.

Alisema kuwa, aliporudi kazini alipata taarifa kutoa kwa mkewe wake kuwa, mtoto wao amekutwa akilawitiwa na mwalimu wake, ndio alipoanza kumuhoji mtoto wake na kumueleza kuwa amemlawiti.

"Nilipoambiwa nilikasirika sana, siku ya pili nilienda kituo cha Polisi Wete kuripoti, kisha tulienda hospitali ingawa daktari alithibitisha kuwa hakuwahi kumlawiti“, alisema baba huyo.

Alieleza kuwa, alipomuhoji mtoto wake alimwambia kuwa yeye alikuwa hataki na badala yake kutumia nguvu kumlazimisha na kumvua nguo zote na ndio alipotaka kumfanyia, ingawa hakuwahi kutokana na kutokea watoto wenzake katika eneo hilo.

"Kutokana na kishindo cha kukataa kitendo hicho mwanagu, hakuwahi kumuingiza ndani kama alivyosema daktar, lakini alikuwa na nia hiyo kwani alikuwa tayari kashamvua nguo", alieleza.

Mama mzazi wa mtoto huyo alieleza kuwa, alipata taarifa kutoka kwa jirani yake, kwamba mtoto wake ameonekana kichakani na watoto wenzake, akifanyiwa kitendo cha kulawiti na mwalimu wake wa chuoni  ‘denja’.

"Nilipomdadisi mwanangu aliniambia kwamba yeye alikuwa akikoga mtoni na ndio alipotokea mwalimu na kumkamata mkono, na kumpelekea kichakani, ili amlawiti ingawa hakiufanikiwa”, alisema mama hiyo.

Kwa upande wake Khamis Hamad Nassor msaidizi wa sheria aliwataka wazazi na walezi, kushirikiana katika malezi pamoja na kuchukua juhudi ya kuwafuatilia, ili kujua sehemu wanazokwenda.

Nae Sheha wa shehia ya Kiungoni Omar Khamis Othman aliwataka wazazi pamoja na mashuhuda wa tukio hilo, waache muhali na badala yake, washirikiane pamoja katika kuhakikisha wanatoa ushahidi mahakamani.

Mratibu wa shehia hiyo, Mchanga said Hamad alisema kuwa, mradi wa kukuza usawa wa Kijinsia na Kuwawezesha Wanawake GEWE ni mkombozi wa Wanawake ba Watoto katika kuwaelimisha wanajamii kuviripoti vitendo vya udhalilishaji.

Mkuu wa Dawati la kijinsia Wilaya ya Wete Khamis Simai Faki alieleza kuwa, tayari kesi hiyo, imeshafika ofisini kwao  na kwa sasa wanaendelea na uchunguuzi, utakapokamilika hatua za kumfikisha mahakamani zitafuta.

Afisa Ustawi wa Jamii Wilaya ya Wete Haroub Suleiman Hemed, alisema shehia ya Kiungoni ni moja ya shehia iliyopata elimu ya kupiga vita vitendo vya udhalilishaji kupitia mradi wa GEWE, ingawa bado vitendo hiyo vinatokea siku hadi siku.

Nae Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba Haji Khamis Haji alithibitisha kutokea kwa tukio hilo Oktoba 30 mwaka huu saa 9:39 jioni, huko Kiungoni Wilaya ya Wete Pemba.

Kamanda Haji alisema kuwa, tayari jalada la kesi hiyo lishafunguliwa, ingawa mtuhumiwa bado hajapatikana, na kusema wapiganaji wake kwa kushirikiana na raia wema wanamtafuta.

Kuanzia mwaka 2015 hadi mwezi Oktoba mwaka huu, tayari wilaya ya Wete kumesharipotiwa matukio matukio 15 ya udhalilishaji kwa njia utawiti ambapo matukio hayo ni yele yalioripotiwa Ustawi wa jamii pekee.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.