(Kutoka Maktaba) Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akimkabishi Kombe la Mapinduzi mwaka 2017 Nahodha wa Timu ya Azam John Bocco jana, baada ya timu hiyo kuifunga Simba kwa bao 1-0 katika mchezo uliomalizika Uwanja wa Amaan Mjini Unguja,[Picha na Ikulu.] 14/01/2017.
Na A K Khiari
Moja katika matukio makubwa ya kihistoria katika Taifa lolote huwa yanashuhudiwa na watu wengi na kubaki kuwa gumzo kwa muda mrefu.
Pia
imekuwa ni kawaida kuona viongozi wa kitaifa wakati Timu zao za Taifa zinapofika fainali
ya mashindano makubwa kuona viongozi wao wa kitaifa wakiacha na kuvunja shughuli
zao ili nao waende kuwashuhudia wachezaji wanaowawakilisha wakipambana kwa
ajili ya kulileta hadhi taifa lao.
Kwa
muktadha huu Zanzibar imepata fursa adhimu ya kutinga katika fainali za
michuano mikubwa pekee ambayo Zanzibar huweza kushiriki kama Zanzibar.
Michuano ya CECAFA. Fursa hii imekuja baada ya miaka 22 ya kusubiri kwani mara ya mwisho kuchukua kombe hili ilikuwa mwaka 1995.
Zanzibar
Heroes haishiriki michuano mengine zaidi
ya hii ya CECAFA na iliwahi kushiriki mashindano ya Dunia ya nchi ambazo hazina
uwakilishi FIFA mwaka 2012.
Kesho
Jumapili macho yetu yatakuwa katika mji wa Machakos nchini Kenya tukiwasubiri
kwa hamu mashujaa wetu, maheroes wetu kutoka Zanzibar wakizidi kuushangaza
ulimwengu wa soka kwa kuweza kufanya kile ambacho dunia inashindwa kuamini kama
kinawezekana kwa kajinchi kadogo kisicho na ufadhili wa aina yoyote hakimo
katika CAF wala FIFA lakini kimeweza kuwang’oa walio katika CAF na FIFA katika
mashindano haya yanayofikia tamati hapo kesho Jumapili.
Kesho
Jumapili wimbo wetu wa Taifa la Zanzibar utaimbwa, itapendeza kama Rais wetu
atakuwepo.
Kesho
Jumapili bendera ya Taifa letu la Zanzibar itapepea, itapendeza kama Rais wetu
atakuwepo
Kesho
Jumapili vijana wetu wanaweza kuibuka kidedea na kutwaa ubingwa wa kombe le
Chalenji, itazidi kupendeza kama Rais wetu atakuwepo na kuwa miongoni mwa watu wa
kwanza kukabidhiwa kikombe (Yaa Rabb tujaalie iwe hivyo kwa uwezo wako Yaa
Rahmaan).
Kesho
Jumapili kila mzanzibari mwenye uchungu na nchi hi na mwenye mapenzi na nchi hii
atakuwa chini ya TV akiwashuhudia mashujaa wetu wana hakikisha kulirudishia
heshima Taifa letu, itazidi kupendeza kama Rais wetu ataonekana kuwa mmojawapo
ambao wapo uwanjani akishangilila na kuwahamasisha vijana wake wazidi kupata
moyo.
Ninaungana
na Mhe Waziri wa Afya, Mahmoud Thabit Kombo pale alipokuwa Baraza la
wawakilishi aligusia nukta muhimu ya kuwapa vijana kile kinachoitwa ‘Moral
Support’ hasa wakiona viongozi wakuu wa nchi wapo uwanjani inawezekana ikawa
ndie mchezaji namba 12 wa timu kwa kuwapa morali.
Mheshimiwa
Rais! Majuzi hapa ulitupa Darsa la uzalendo na kutueleza kuwa mzalendo ni yule aliyezaliwa pahala fulani
kwenye asili yake ambapo pia, ni mtu mwenye mapenzi ya dhati sana ya kuitumikia
nchi yake na kueleza maana ya uzalendo kuwa ni hali ya mtu kuwa na nasaba ya
asili ya nchi ambaye pia hujitolea kwa hali na mali kwa ajili ya nchi yake.
Vijana wetu ni mfano mzuri
wa kujitolea jinsi walivyoweza kufanya kazi ya ziada kufika fainali ya
mashindano makubwa Afrika Mashariki na kati. Kwa ufupi walielewa darsa lako la
uzalendo na kuuonesha kwa vitendo.
Mheshimiwa
Rais! Dk Ali Mohamed Shein, kwa heshima na taadhima nafikisha ujumbe huu mfupi
waunge mkono vijana kwa uzalendo: Itapendeza ukiwapo uwanjani Machakos kesho, ni matarajio vijana hawatokuangusha hasa wakikuona kwenye jukwaa wakati wakiimba wimbo wa Taifa la Zanzibar.
No comments:
Post a Comment