Habari za Punde

Tume ya Ardhi Kuanzisha Kazi Data ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi.

Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi (NLUPC) ipo mbioni kuanzisha Kanzidata (Database) ya mipango ya matumizi ya ardhi iliyofanyika nchini na wadau mbalimbali wa sekta ya ardhi.


Kwa kushirikiana na wadau wa upangaji, usimamizi na utekelezaji wa mipango ya matumizi ya ardhi wa taasisi za serikali pamoja na asasi za kiraia, Kanzidata hiyo itabeba taarifa zitakazoonyesha maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya shughuli mbalimbali kama vile kilimo, malisho, huduma za jamiii, n.k itarahisisha utendaji kazi kwa Tume, mamlaka zingine za upangaji, wadau pamoja na wananchi kwa ujumla ambao watatumia teknolojia kujua maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya shughuli mbalimbali nchi nzima
Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya mipango ya matumizi ya Ardhi(NLUPC) Dkt. Stephen Nindi akifungua mkutano wa kikosi kazi kwa ajili ya mchakato wa uanzishwaji wa kanzidata ya mipango ya matumizi ya ardhi,Mjini Morogoro
Mwenyekiti wa Kikao Bw. Jamboi Baramayegu kutoka ujamaa Community akielezea utaratibu wa namna kazi itakavyofanyika
Afisa Tehama kutoka wakala wa Serikali Mtandao Bw. Thomas Malinga akitoa maelezo ya malengo ya wao kushiriki katika mchakato wa uanzishwaji wa uanzishwaji wa kanzi data ya mipango na matumizi ya ardhi.
Afisa Mipango wa Tume ya Taifa ya mipango ya matumizi ya Ardhi Bw. Gelard Mwakipesile, akielezea kwa kina kwa wajumbe wa mkutano kuhusu mipango ya matumizi ya ardhi,mchakato ulipo anzia hadi kuanza kwa  mchakato wa uanzishwaji wa kanzi data ya mipango ya matumizi ya ardhi
 Bw. Paulo Tarimo kutoka Wizara ya Kilimo akichangia jambo wakati wa kikao cha mchakato wa uanzishwaji wa kanzi data ya mipango ya matumizi ya ardhi.
 Baadhi ya wanakikosi kazi kutoka sekta mbalimbali wakiendelea na majadiliano ya kutoa maoni yao juu ya kuandaa mchakato wa uanzishwaji wa kanzi data ya mipango ya matumizi ya ardhi.
 Katibu Mkuu wa Chama cha wafugaji Tanzania Bw. Magembe Makoye akiwasilisha mapendekezo yao kwa ajili ya mchakato wa uanzishwaji wa kanzi data ya mipango ya matumizi ya ardhi kutoka katika kundi la wafugaji
 Bw. Godfrey Massay Meneja utetezi kutoka LANDESA  akiwasilisha mapendekezo yao kwa ajili ya mchakato wa uanzishwaji wa kanzi data ya mipango ya matumizi ya ardhi kutoka katika kundi la Kilimo
 Afisa Sheria kutoka NLUPC Bi. Devotha Selukele akichangia jambo wakati makundi mbalimbali wakiwasilisha maoni yao juu ya kanzi data
 Afisa programu kutoka Haki Ardhi Bw. Joseph Kiombola   akiwasilisha mapendekezo yao kwa ajili ya mchakato wa uanzishwaji wa kanzi data ya mipango ya matumizi ya ardhi kutoka katika kundi la Asasi za Kiraia.
 Afisa wanyama pori (TAWA) Bw. Herman Nyanda   akiwasilisha mapendekezo yao kwa ajili ya mchakato wa uanzishwaji wa kanzi data ya mipango ya matumizi ya ardhi kutoka katika kundi la Maliasili
 Afisa Mpelembaji kutoka TNRF Bw. Wilbard   akiwasilisha mapendekezo yao kwa ajili ya mchakato wa uanzishwaji wa kanzi data ya mipango ya matumizi ya ardhi kutoka katika kundi la Utafiti
 Wadau wakiendelea na mkutano huo.
Picha na Fredy Njeje/Blogs za Mikoa Tanzania

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.