Kikosi cha Timu ya Jang'ombe Boys
Ni kati
ya Jang’ombe Boys na Gulioni.
Mashabiki
waelezea matumaini kwa timu zao.
Tamasha
la kimichezo la Zanzibar New Year Bonanza lililoandaliwa na Taasisi ya Rafiki
Network linatarajiwa kuzinduliwa Rasmi siku ya Jumatatu ya tar. 25 Disemba kwa
mechi ya mpira wa miguu kati Jang’ombe Boys na Gulioni Fc inayotarajiwa
kuchezwa katika dimba la uwanja wa Aman saa 2:00 usiku. Mgeni Rasmi katika
mchezo huo atakua Kocha wa timu ya Zanzibar Heros Nd. Hemed Morocco.
Rais
wa Taasisi hiyo Nd. Hamad Hamad, amesema maandalizi ya mchezo huo yamekamilika na kuongeza kwamba
tasisi yake imejipanga vya kutosha kuhakikisha kwamba inaimarisha michezo hapa
Zazibar.
Nae
Rais wa timu Jang’ombe boys Nd. Ali Othman Ali amesema timu yake imefarijika
sana kupata mwaliko wa kucheza na timu ya Gulioni ambapo timu itakayoibuka
mshindi itapata kombe na fedha taslim. Akizungumza katika kipindi cha michezo
ya wiki ‘coco sport’ kinachorushwa hewani kila Jumamosi kupitia kituo cha Redio
cha Coconut FM, bwana Ali amesema awali pambano hili lilipangwa kufanyika
tarehe 31 mwezi huu ambapo ilitarajiwa kuwakutanisha na mahasimu wao Taifa ya
Jang’ombe.
Nd.
Ali ameelezea sababu za kufutwa kwa mechi hiyo kuwa ni kupisha michuano yenye hadhi
na taswira ya urithi na uzalendo wa nchi maarufu kama Mapinduzi Cup. Amefafanua
kwamba kutokana na kuongezeka kwa idadi ya timu zinazoshiriki michuano hiyo
ratiba ya Mapinduzi cup imelazimika kuanza mwishoni mwa mwezi huu.
Nae
shabiki maarufu wa timu ya Jang’ombe boys Nd. Kassim Jecha amesema anamatumaini
makubwa kwamba timu yake itaibuka na ushindi na kuandika historia wakati
tukielekea mwaka mpya 2018.
Nae
Rais wa timu ya Gulioni fc amesema maandalizi ya mchezo huo yamekamilika na
kwamba timu yake ipo katika hali nzuri kuweza kuibuka mshindi katika mchezo
huo.
Mechi
hiyo ya mpira wa miguu ni sehemu ya bonanza la kimichezo la Zanzibar New Year
Bonanza ZNYB, ambapo mbali na mchezo huo kutakua na Ngoma za mitaani ‘Street
dance’ na Ngoma za asili zitakazochezwa Ngome Kongwe tarehe 29 Disemba, Michezo
mbali mbali ya watoto itakayochezwa kule Fumba tarehe 30 Disemba na mashindano
ya baiskeli kutoka Makunduchi hadi Uwanja wa Amani tarehe 31 Disemba.
No comments:
Post a Comment