Habari za Punde

MTAJI WA BENKI YA TPB UMEKUWA KUTOKA BILIONI 8 HADI BILIONI 60



Mwenyekiti Mstaafu wa Bodi ya wakurugenzi wa Benki hiyo,Proffesa Lettice Rutoshobya akifungua tawi jipya la TPB mkoani Tanga kushoto ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya TPB Sabasaba Moshingi akishuhudia
 Mwenyekiti Mstaafu wa Bodi ya wakurugenzi wa Benki hiyo,Proffesa Lettice Rutoshobya akikata utepe kushiria ufunguzi wa tawi la TPB Tanga kushoto ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya TPB Sabasaba Moshingi na kulia ni Mwenyekiti Mpya wa Bodi ya Wakurugenzi wa TPB Dkt Edmund Mndolwa
 Wakisalimiana na wateja mara baada ya kufungua Tawi hilo
 Mwenyekiti Mpya wa Bodi ya Wakurugenzi ya TPB Dkt Edmund Mndolwa kushoto akiwa na Mwenyekiti aliyemaliza muda wake Proffesa Lettice Rutashobya anayesaini kitabu cha wageni mara baada ya kufungua tawi hilo la Tanga leo
 Mwenyekiti Mpya wa Bodi ya Wakurugenzi ya TPB Dkt Edmund Mndolwa akisaini kitabu cha wageni kulia ni Mwenyekiti aliyemaliza muda wake Proffesa Lettice Rutashobya
 Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya TPB Sabasaba Moshingi akisaini kitabu cha wageni
 Meneja wa TPB Tawi la Tanga Mwajabu Mshana kushoto akiwaeleza jambo Mwenyekiti  Mpya wa Bodi ya wakurugenzi wa TPB Dkt Edmundo Mndolwa kushoto aliyekaa na anayemaliza muda wake Proffesa Lettice Rutashobya mara baada ya kufunguliwa kwa tawi hilo leo
 Mwenyekiti  Mpya wa Bodi ya wakurugenzi wa TPB Dkt Edmundo Mndolwa kulia akitembelea maeneo mbalimbali kwenye benki ya TPB tawi la Tanga mara baada ya kufunguliwa na Mwenyekiti aliyemaliza muda wake Proffesa Lettice Rutashobya katika kushoto ni Afisa Mtendaji Mkuu wa benki ya TPB Sabasaba Moshingi
Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi wa TPB aliyemaliza muda wake Proffesa Lettice Rutashobya akizungumza katika ufunguzi huo wa tawi kulia ni Afisa Mtendaji Mkuu wa TPB Sabasaba Moshingi
Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi wa TPB Dkt Edmund Mndolwa akizungumza katika hafla hiyo
Afisa Mtendaji Mkuu wa TPB Sabasaba Moshingi akizungumza katika halfa hiyo

Meneja wa TPB tawi la Tanga, Mwajabu Mshana
Meneja Mwandamizi wa Uhusiano wa Umma wa Benki ya Posta Tanzania (TPB), Noves Moses
 Utoaji wa vyeti ukiaendelea mara baada ya kumalizika kwa ufunguzi huo
 Picha ya Pamoja mara baada ya uzinduzi huo
 Sehemu ya wananchi waliohudhuria uzinduzi huo

MWENYEKITI wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya TPB Dkt Edmund Mndolwa amesema mtaji wa benki hiyo hivi sasa umekuwa kutoka Bilioni 8 hadi kufikia Bilioni 60 hatua inayoonyesha utendaji mzuri wa wafanyakazi kutokana na kutoa huduma bora zinazowafanya wateja kuvutiwa na kujiunga nao.

Dkt Mndolwa aliyasema hayo leo wakati wa ufunguzi wa tawi la Tanga la Benki hiyo lililopo eneo la Chumbageni Jijini Tanga ambao ulifanywa na Aliyekuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Proffesa Lettice Rutashobya kwenye halfa iliyofanyika mjini hapa na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo wajumbe wa bodi ya wakurugenzi na wafanyakazi.

Alisema hatua hiyo inatokana na huduma nzuri inayotolewa na wafanyakazi wa benki hiyo na hivyo kusaidia kuwepo kwa ongezeko kubwa la wateja jambo ambalo limepelekea kuongezeka matawi nchini kutoka 32 mpaka 74 kwa sasa.

“Niwapongeze sana TPB kwa kasi kubwa ya utendaji mzuri mliokuwa nayo na kupelekea kuwezesha kupanua wigo wa matawi kwa wateja wenu ambapo awali kulikuwa na matawi 32 lakini hivi sasa yamefikia 74 hii ni hatua nzuri sana hivyo kuwatake muendelee nayo “Alisema.

“Lakini pia nimpongeze Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi anayemaliza muda wake Proffesa Lettice kwa kazi nzuri aliyoifanya jambo ambalo limewezesha kufikia mafanikio yaliyopo hivi sasa ndani ya benki hii nitaendelea kushirikiana na wafanyakazi “Alisema.

Awali akizungumza katika halfa hiyo, Afisa Mtendaji Mkuu wa benki hiyo Sabasaba Moshingi alisema benki yake imeendelea kukua kwa kasi mwaka hadi mwaka na kupata faida ambayo imewezesha kutoa gawio kwa serikali ya zaidi ya bilioni moja.

“Mwaka Jana 2017 benki ilipata kiasi cha Bilioni 18.4 kama faida kabla ya kodi lakini pia tumedhamiria kuboresha huduma zetu ili tuweze kufanya vizuri kwani ushindani kwenye sekta hii ya mabenki ni mkubwa “Alisema.

Kwa upande wake Mwenyekiti Mstaafu wa Bodi ya wakurugenzi wa Benki hiyo,Proffesa Lettice Rutoshobya alisema wanaamini tawi hilo jipya litaongeza idadi ya wateja kwenye benki hiyo kwani lengo kubwa ni kuwasogezea huduma karibu wananchi .

“Ni furaha kubwa sana kwetu sisi TPB kuweza kufikisha huduma zetu hapa Tanga kupitia tawi letu hili Jipya pia tunalo tawi lingine dogo kule wilayani Korogwe ambapo wateja wetu wanapata huduma za kibenki”Alisema.

Naye Meneja wa TPB tawi la Tanga, Mwajabu Mshana alisema mwitikio wa wakazi wa mkoa huu umekuwa mzuri tangu walipoanza kutoa huduma zake maeneo hayo ya Chumbageni huku akieleza wamejipanga kutoa huduma nzuri kwa wananchi (Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamiiya Tanga Raha)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.