Habari za Punde

Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma Zanzibar yatoa elimu kwa Mabaraza ya Vijana wa Wilaya za Magharibi na Mjini Unguja juu ya nafasi ya vijana katika kukuza maadili.

Katibu wa Tume ya Maadili Zanzibar, Ndugu; Kubingwa Mashaka Simba akifunga mkutano uliojadili nafasi ya vijana (kulia) Katibu wa Baraza la Vijana Taifa, Ndugu; Khamis Faraji Abdalla (kushoto) Makamu Mwenyekiti Baraza la Vijana Taifa, Ndugu; Mariam Ishau Abdalla.
Mwenyekiti wa Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma Zanzibar, Mhe: Assaa Ahmad Rashid akihutubia mabaraza ya Vijana ya Wilaya za Magharibi na Mjini wakati alipofungua mkutano uliojadili nafasi ya Vijana katika kukuza maadili uliofanyika katika ukumbi wa Sheikh Idriss Abdul Wakil Kikwajuni. 
Afisa Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma Zanzibar, Ndugu; Haji Juma Chapa, akijibu baadhi ya hoja zilizotolewa na Wajumbe wa Mabaraza ya Vijana Wilaya za Magharibi na Mjini katika mkutano uliojadili nafasi ya vijana katika kukuza maadili ulioandaliwa na Tume ya Maadili kwa Mabaraza hayo. Pembeni yake Ndugu; Khamis Faraji Abdalla, Katibu wa Baraza la Vijana Taifa Zanzibar.

Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Baraza la Vijana Taifa kutoka Wilaya Magharibi B, Ndugu; Said Moh’d akichangia mada katika mkutano uliohusu nafasi ya vijana katika kukuza maadili ulioandaliwa na Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma Zanzibar kwa Mabaraza ya Vijana za Wilaya za Mjini na Magharibi Unguja uliofanyika katika ukumbi wa Sheikh Idriss Abdul Wakil Kikwajuni.

Baadhi ya wajumbe wa Mabaraza ya Vijana Wilaya za Magharibi na Mjini wakifuatilia kwa makini mada zinazowasilishwa na watendaji wa Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma katika mkutano uliojadili nafasi ya vijana katika kukuza maadili uliofanyika ukumbi wa Sheikh Idriss Abdul Wakil. wajumbe wakifuatilia mada zinazowasilishwa na maofisa wa Tume ya Maadili


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.