Rais wa Zanzibar na Mwenmyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akiwa na Mama Mwanamwema Shein wakimsikiliza Msanifu Majengo wa Kampuni ya SRAT Consuat ya Tanzania,inayosimamia Ujenzi wa Majengo ya Skuli ya Kisasa ya Msingi Kwarara Ndg. Salim Rajab Twakyondo, akitowa maelezo ya michoro ya ramani ya majengo ya Skuli hiyo wakati wa ziara yake na kuweka Jiwe la Msingi la Mradi huo leo, akiwa katika ziara yake katika Wilaya ya Magharibi B, Unguja.
Na.Abdi Shamnah.Ikulu Zanzibar.
RAIS
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi, Dk Ali Mohamed Shein amesema
katika kutekeleza sera ya elimu bila malipo, Serikali inaendelea na juhudi za
kuimarisha miundo mbinu ya kielimu ili kwenda sambamba na mahitaji yaliopo.
Dk
Shein amesema hayo leo katika hafla ya uwekaji wa jiwe la Msingi wa Skuli ya msingi
Kwarara, Wilaya ya Magharibi ‘B’ Unguja.
Amesema
kutokana na ongezeko kubwa la wanafunzi hali inayotokana
na kiwango kikubwa cha wakaazi wa Zanzibar hivi sasa, Serikali inalazimika
kuongeza idadi ya madarasa ili kwenda sambamba na ongezeko la wanafunzi katika
skuli za msingi na sekondari.
Alisema
ongezeko la idadi ya watu kutoka 300,00 mwaka 1964 hadi kufikia Milioni moja na
nusu hivi sasa imefanya kuwepo mahitaji makubwa ya madarasa , huku baaadhi ya
skuli zikiwa na wanafunzi wanaofikia 234 katika darasa moja,
Alisema
hivi karibuni Serikali imeagiza madawati
na vikalio 44,000 kutoka nchini China na
kubainisha kuwa nusu ya samani hizo zimewasili nchini na kugawiwa katika skuli
za msingi na sekondari.
Dk.
Shein alisisitiza azma ya serikali na kuwataka wazazi na walezi wa wanafunzi
kutokuchangia huduma zote za kielimu katika skuli za msingi na sekondari, ikiwemo vitabu madaftari
Alisema
lengo la serikali ni kuwaandaa vijana wake kielimu ili kufanikisha azma ya kuwa
an wataaalamu katika fani mbali mbali
ili kuliwezesha Taifa kupata maendeleo ya haraka.
Alisema
uchumi wa Zanzibar umeendelea kuimarika kadri miaka inavyosonga hatua inayotokana
an makusanyo mazuri ya mapato na kubainisha kuwa hivi sasa Serikali inakusanya kati
ya shilingi Bilioni 65 hadi 70 kwa mwezi,
hivyo kumudu gharama za uendeshaji wa
miradi mbali mbali ya maendeeo, ikiwemo ya maji na barabara.
Alisema
hali hiyo imechangia kufanikisha azma ya serikali ya kusomesha wataalamu wake
katika fani tofauti, ikiwemo madaktari.
Akigusia
historia ya elimu nchini, Dk. Shein alisema Mapinduzi ya 1964 yamekuja
kuwakomboa watoto wa wanyonge kutokana an dhuluma ya kukoseshwa elimu.
Alisema
wakati chama cha ASP kikipigania uhuru, kilibainisha wazi katika Ilani zake,
dhamira ya kuipa kipaumbele elimu na kutolewa bila malipo.
Alisema
elimu ina umuhimu mkubwa katika maisha ya binadamu, kama Mwenyezi Mungu
alivyobainisha katika kitabu kitakatifu cha Qoraan.
Alisema
ni lengo la Serikali katika siku zijazo kujenga skuli za msingi za ghorofa, ili
kukidhi mahitaji kutokana na ufinyu wa
ardhi uliopo.
Dk.
Shein alichukuwa fursa hiyo kuipongeza taasisi ya Good Neighbor kutoka Jamuhuri
ya Korea Kusini kwa msaada mkubwa wa kufanikisha
ujenzi wa skuli iyo.
Nae,
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali, Riziki Pembe Juma amesema alisema Wizara
hiyo kwa kushirikiana an Wizara ya Nchi (OR) Tawala za Mikoa na serikali za
Mitaa, Tawala za Mikoa, idara maalum na
Vikosi vya SMZ pamoja na Jamuhuri ya Korea
italiendeleza jengo hilo katika awamu inayofuata.
Waziri
Pembe alimhakikishia Rais Dk. Shein kuwa huduma za kielimu pamoja na vitabu na
madaftari zitaendelea kutolewa bure nchini kote ili kwenda sambamba na Sera ya
Elimu,
Mapema,Naibu
Katibu Mkuu Wizara ya elimu na maunzo ya Amali Madina Mjaka, alisema ujenzi wa
skuli hiyo itawasogeza wanafunzi karibu
na makazi, kama ilivyoainishwa kwenye ilani ya CCM.
Aidha,
alisema itapunguza mlundikano wa wanafunzi wa skuli za jirani, hususan Kijitoupele,
ambapo kwa sasa darasa moja hujumuisha hadi wanaafunzi 100 – 120.
Alisema
awamu ya kwanza ya ujenzi wa skuli hiyo umegharimu zaidi ya shilingi Bilioni
1.5, ambapo skuli hiyo inatarajiwa kuchukuwa wanafunzi 3,780.
Aidha
alisema katika kufanikisha ujenzi wa skuli hiyo Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar imetowa msamaha wa vifaa vya ujenzi pamoja na kuchangia samani.
No comments:
Post a Comment