Afisa
Maandalizi Idara ya Maandalizi na Msingi Bi Fatma Mode Ramadhani akimkaribisha
Mkurugenzi Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara maalum za SMZ Nd.
Abdulla Issa Mgongo katika ufunguzi wa mafunzo ya siku tano kwa wasaidizi wa
vituo vya Tucheze Tujifunze.
Mkurugenzi
Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara maalum za SMZ Nd. Abdulla Issa
Mgongo akizungumza na Wasaidizi wa Vituo vya Maandalizi vya Tucheze Tujifunze wakati akifungua mafunzo ya
siku tano katika ukumbi wa Skuli ya Maandalizi Madungu.
Wasaidizi
wa vituo vya Tucheze Tujifunze wakiwa katika Ukumbi wa Skuli ya Maandalizi
Madungu Chake Chake Pemba katika ufunguz wa Mafunzo ya Siku tano ya kuwajengea
uwezo.
Na
Ali Othman
Wasaidizi
wa vituo vya maandalizi vya “Tucheze Tujifunze” kisiwani Pemba wametakiwa
kuzingatia na kuyafanyia kazi mafunzo
wanayoyapata ili waweze kuwaandaa vyema watoto katika kuikabili elimu ya msingi.
Hayo
yameelezwa na Mkurugenzi Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara maalum za
SMZ Nd. Abdulla Issa Mgongo wakati akifungua mafunzo ya siku tano katika ukumbi
wa Skuli ya Maandalizi Madungu Chake Chake Pemba.
Akifafanua
umuhimu wa mafunzo hayo, Nd. Mgongo amesema mafunzo hayo yamelenga kuwajengea
uwezo wasaidizi wa vituo hivyo na hivyo kutambua kwamba wanawajibu mkubwa wa
kuhakikisha kwamba watoto wanapata elimu bora.
Akielezea
malengo ya kuanzishwa kwa vituo hivyo Nd. Mgongo amesema kuwepo kwa vituo hivyo
kumesaidia kutatua tatizo la upatikanaji wa elimu ya maandalizi katika maeneo
na vijiji ambavyo viko mbali na Skuli za Msingi.
Aidha
Mkurugenzi huyo amesema, mbali na kuwapunguzia masafa watoto wadogo, kuwepo kwa vituo hivyo katika maeneo mbali mbali vijijini, kumesaidia kukabiliana
na vitendo vya udhalilishaji kwa watoto.
Awali
Afisa Maandalizi Idara ya Maandalizi na Msingi Bi Fatma Mode Ramadhani
akimkaribisha Mkurugenzi Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara maalum za
SMZ Nd. Abdulla Issa Mgongo amesema kuwepo kwa vituo vya Tucheze Tujifunze “TUTU”
kunasaidia kutekeleza lengo la Serikali la kuhakikisha kwamba kila mtoto mwenye
umri wa miaka mine anapata elimu ya maandalizi.
Katika
kuhakikisha kwamba mafunzo hayo yanafikia Ufanisi Mkurugenzi Idara ya
Maandalizi na Msingi Bi Safia Ali Rijali kwa mashirikiano na Mkurugenzi Ofisi
ya Rais TAMISEMI Nd. Abdulla Issa Mgongo wamekua wakifuatilia kwa karibu ili
kuhakikisha kwamba mafunzo hayo yanatoa elimu bora kwa watoto.
Jumla
ya vituo 344 vya Tucheze Tujifunze “TUTU” vimeanzishwa Zanzibar ambapo vituo
162 vipo Unguja na vituo 182 vipo kisiwani Pemba.
No comments:
Post a Comment