Habari za Punde

UWT Manispa ya Iringa Kopeni Kwa Malengo ya Maendeleo.


Mwenyekiti wa umoja wa wanawake manispaa ya Iringa (UWT) Ashura Jongo akizungumza wakati wa baraza la UWT manispaa ya Iringa akiwaasa wanawake kukopa kwa malengo
Mwenyekiti wa CCM manispaa ya Iringa Said Rubeya akitoa neno kwa wanawake wa UWT manispaa ya Iringa. 
 

NA FREDY MGUNDA,IRINGA.
Kukosekana kwa elimu ya matumizi bora ya mikopo kwa wanawake kumetajwa kuwa sababu ya wanawake wengi wa manispaa ya Iringa kushindwa kurudisha mikopo katika taasisi za kifedha.

Akizungumza kwenye baraza la UWT manispaa ya Iringa,mwenyekiti wa umoja huo Ashura Jongo  amesema kuwa wananwake wamekuwa wanakopa bila ya kuwa na elimu ndio maana wanashindwa kurejesha mikopo ambayo wamekopa kwenye taasisi za kifedha.

“Changamoto za wanawake kutokuaminika katika vyombo au taasisi za kifedha ni kutokana na hali ngumu,wanawake wanaweza wakakopa wakiwa na malengo lakini wakirudi nyumbani wanakutana na matatizo mengi yanahitaji matumizi ya fedha” aliema Jongo

Jongo alisema kuwa wanawake wanatakiwa kuendelea kuwawezesha kwa kuwa wanauwezo wa kutmia vizuri fedha ambazo zinapatikana hivyo ukimuwezesha mwanamke umewawezesha watu wengi kwa kuwa wanawake ndio nguzo ya familia hasa kwenye maswala ya kiuchumi.

Kwa upande wake mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa kupitia chama cha mapinduzi Rose Tweve amezitaka taasisi za kifedha kutoa elimu kwa wakopaji ili waweze kuzitumia vizuri fedha hizo.
“Shida moja wapo ya wanawake kushindwa kurudisha mikopo ni kutokana na kutokuwa naelimu ya matumizi ya fedha kwa kuwa pesa hiyo inahitaji nidhamu na matumizi bora ya fedha hizo za mikopo” alisema Tweve

Tweve alisema kuwa tasisi za kifedha zinatakiwa kutoa elimu kwanza kabla ya kutoa mikopo kwa wanawake ili waweze kuzirejesha kwa wakati kwa kuwa tayari ameshapata elimu ya matuzi bora ya mikopo waliyokopa.

“Pale wanapokopa lazima wajue matumizi ya hizo pesa la sivyo watazitumia bila nidhamu fedha hizo na kushindwa kuzirejesha na kujikuta wakiwa matatani kutokana na kushindwa kulipa mkopo huo” alisema Tweve

Naye mgeni rasmi kwenye baraza hilo mwenyekiti wa CCM manispaa ya Iringa Said Rubeya amewataka wanawake kuwa na nidhamu ya matumizi ya fedha ili kufikia malengo waliyojiwekea kabla ya kwenda kukopa.

“Kwa kwali wanawake wa CCM manispaa ya Iringa wengi mnakopa mikopo lakini hamrejeshi kwa wakati na hili ni bomu kubwa kwa chama hivyo mnatakiwa kuwa na nidhamu ya matumizi ya mikopo hiyo” alisema Rubeya

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.