Habari za Punde

Wahujaji Watakiwa Kulinda Hijja Zao

Kiongozi  wa Mahujaji wa Taasisi ya Istiqama Zanzibar  Sheikh Suwedi Ali Suwedi  akiwaasa mahujaji waliorudi hijja  hivi karibuni kutekeleza nguzo ya tano ya kiislamu, akizungumza na Mahujaji hao katika ukumbi Baitul Yamin Malindi Mjini Zanzibar 
Mahujaji waliorudi Makka kutekeleza ibada ya hijja wakimsikiliza Shekh Suweid Ali (hayupo pichani)  wakati alipokuwa akizungumza nao katika ukumbi wa Baitul Yamin Mjini Zanzibar. 
Picha na Mwashungi Tahir  wa  Habari Maelezo.

Na.Mwashungi Tahir     Maelezo   28-9-2019.
Mahujaji waliorejea nchini kutoka Macca Saudia Arabia  kutekeleza Ibada ya Hija  wamehimizwa kulinda hija  zao kwa kujiweka karibu na Mwenyezi Mungu ili kuweza kupata mafanikio duniani na akhera.
Wasia huo ameutoa Kiongozi  wa Mahujaji kutoka Taasisi ya Istiqama Zanzibar Sheikh Suwedi Ali Suwedi huko katika ukumbi wa Bayt al Yamin Malindi mjini Zanzibar alipokuwa akizungumza na Mahujaji hao .
Alisema kuwa  Mahujaji waliorejea kutekeleza Ibada hiyo wajitahidi kulinda hija zao ili ibada zao ziweze kuleta tija kwao  na  kuwa kigezo kizuri kwa jamii iliyowazunguka 
 “Wajibu kwa Mahujaji kubadilika kutokana na Ikram kubwa waliyopewa na Allah S.W kupata uwezo wa kutekeleza ibada hiyo.”alisema Sheikh Suedi.
Aidha alisema kwenda hija sio kuhiji tu na kurudi ikawa basi, bali  Hija ni kukamilisha kwa moyo mmoja na kuonyesha mabadiliko ya kuwa karibu zaidi na Mwenyenzi Mungu  na kuyaacha yale yote aliyoyakataza .
Alifahamisha kuwa baada ya kurudi hija kwa kumuomba Mwenyezi Mungu kakupa lakini kile alichokupa utakitunza vipi , haina maana tusile vizuri tusende katika shughuli zetu za maisha lakini lazima tuoneshe namna ya kubadilika.
“ Hija ni hii ya mwanzo hata ikikariri mara kumi mara ishirini ukenda hija basi daraja ya hija ya mwanzo ndio Mwenyezi Mungu anampa mja wake milango ya kheri na fadhila katika umri wake``. alisema Sheikh Suedi.
Aidha amewasisitiza waislamu wenye uwezo kufanya haraka katika kutekeleza ibada hiyo muhimu ili kuweza kuondoa deni baina yao na Allah S.W.
Nae Mwenyekiti wa kamati ya hija Istiqama Sheikh Sultan Khamis Mazrui amesema tathmini hiyo ina faida kubwa katika kuondosha kasoro kwa jumuiya na viongozi mmoja mmoja katika kuwasimamia mahujaji kutekeleza ibada yao kwa ubora.
Nao Mahujaji hao waliosafiri na Taasisi ya Istiqama Zanzibar wamewashukuru wasimamiaji  kwa utekelezaji wa kazi zao za kusimamia Mahujaji hao katika harakati za  ibada hiyo hadi kukamilika na kurejea salama.
 Hata hivyo waliiomba Taasisi hiyo kuweza  kujipanga vyema katika safu ya Uongozi na Usimamizi wa  Mahujaji  katika mwaka ujao kwani wanapofika Mji wa Makka na Madina mahujaji  huwa  wageni katika kila maeneo na kuweza kuepukana na usumbufu utakaoweza  kujitokeza .
Pia wamewaomba waislamu wenzao wa kila mwenye uwezo afanye haraka ya kwenda Makka kufanya ibada hiyo,ikiwa  wangali wazima wa Afya na wasisubirie hadi wafikie watu wazima kwani jambo lolote la ibada ukilifanya na nguvu zako ndio linakuwa bora zaidi.
“walisema raha zaidi unapokwenda kule uwe na nguvu zako kwa kuweza  kufanya vitendo mwenyewe kila sehemu  hapo inakuwa uzuri  hasa,”walisema mahujaji hao.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.