Habari za Punde

NAIBU WAZIRI AWESO AWATUMBUA MENEJA WAKALA WA MAJI VIJIJINI PANGANI,MENEJA WA MAMLAKA YA MAJI SAFI PANGANI

 NAIBU Waziri wa Maji Jumaa Aweso na Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM)  akizungumza na watumishi wa wilaya ya Pangani wakati wa ziara yake wilayani humo.

Naibu Waziri wa Maji Jumaa Aweso amemsimamizi kazi Meneja wa Wakala wa Maji Vijiji Pangani ( DM) RUWASA PANGANI Ladislaus Modestus huku akiagiza Mkurugenzi wa Usambazaji wa Maji na Usafi wa Mazingira (Ruwasa) Makao Makuu Mkama Bwire kuondoka naye kutokana na kushindwa kusimamia miradi ya maji huku mingine akiwa haitambui.

Pia ameagiza Meneja wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira wilaya ya Pangani Adam Sadick kusimamishwa kazi kutokana na kushindwa kusimamia miradi na bili za maji na kupelekea mamlaka kupata hasara. 

Agizo la Naibu Waziri Aweso linatokana na mhandisi huyo kushindwa kusimamia miradi ya maji wilayani humo na hivyo kupelekea wananchi kukosa maji hali ambayo ilimchukiza Naibu Waziri huyo ambaye alikuwa kwenye ziara wilayani humo.

Alisema kwamba mkurugenzi huyo anapoondoka aondoke na mhandisi huyo ambayo ameshindwa kuendana na kasi ya kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya maji ambayo ni muhimu kwa ustawi wa maisha yao .

Aidha alisema kwamba hatua hiyo inatokana na kwamba mhandisi huyo kupewa fedha za kusimamia mradi milioni 26 lakini bado hafiki kwenye maeneo yanayotekelezwa miradi

“Ndugu yangu wewe ni mhandisi wa maji upo hivi kama ungekwa daktari si ungekuta umekwisha kuua watu hatuwezi kukubali kuona hali kama hii na hatupo tayari kuona watu wa namna hii”Alisema

“Kutokana na kwamba Mhandisi huyo anapata fedha za kusimamia miradi ya maji kwenye wilaya hii na anashindwa kufanya hivyo hata ukiangalia msafara wangu ameupoteza wewe hautufai ni bora ukaondoka naye “Alisema Naibu Waziri Aweso. 


Hata hivyo Naibu Waziri huyo aliagiza kuundwe tume itakayobaini nini changamoto iliyopo kwenye usimamizi wa miradi ya maji Pangani jambo ambalo limepeleka kushindwa kufanyika kwa ufanisi mkubwa kama ilivyo maeneo mengine.

“Pia eneo la kibinda linachangamoto kubwa ya maji mimi kama mbunge wakati sijawa Naibu Waziri nilimfuata Waziri Kamwele nikamuambia suala hilo…niambieni kwamba mradi wa kibinda mabomba yanafika lini? Alihoji Naibu Waziri huyo.

Awali akizungumza wakati akitoa taarifa ya wilaya ya Pangani Mkuu wa wilaya ya Pangani Zainabu Abdallah alimueleza Naibu Waziri Aweso kwamba wananchi mji wa Pangani wana changamoto ya maji zaidi ya wiki tatu na hivyo kupelekea wananchi kukosa maji.

Mkuu huyo wa wilaya alisema kutokana na kwamba alikuwa likizo aliporudi alikwenda kwenye eneo la mradi kwa ajili kukagua maji na juzi ameenda kwenye mradi huo na amegundua changamoto tatu awali ni mfumo wa umeme kwa maelekezo wa meneja wa Pasawa.

Alisema tatizo hilo la mfumo wa umeme limesababishwa na tatizo kubwa la umeme kuingia na mfumo kuharibika huku akieleza kwamva changamoto nyengine ni pampuni kuwa na uwezo mdogo kuliko inavyopaswa kutumika kwenye maji.

“Wataalamu wanasema pampu ina uwezo mdogo mimi nashangaa wakati ikinunuliwa …mashine ya kuvuta umeme na kuzima mashine zipo mbili na moja ni mbovu na pampu zaidi ya milioni 22 ni mbovu anasema maelezo ya mkandarasi mfumo wa umeme mbovu”Alisema Mkuu huyo wa wilaya ya Pangani.


 NAIBU Waziri wa Maji Jumaa Aweso ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) kushoto akimsikiliza Mkuu wa wilaya ya Pangani Zainabu Abdallah wakati wa ziara yake wilayani humo
 KATIBU Tawala wa wilaya ya Pangani Mwalimu Hassani Nyange akizungumza wakati wa ziara hiyo kulia ni Mkuu wa wilaya ya Pamngani Zainabu Abdallah kushoto ni Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Pangani Rajabu Abdallah
 Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Pangani Rajabu Abdallah  akizungumza wakati wa ziara hiyo kulia ni Katibu Tawala wa wilaya ya Pangani Mwalimu Hassani Nyange
 MWENYEKITI wa Halmashauri ya wilaya ya Pangani Seif Saidi akizungumza wakati wa ziara hiyo kushoto ni Afisa Tawala wa wilaya ya Pangani Gibson George
 AFISA Tawala wa wilaya ya Pangani Gibson George akizungumza wakati wa ziara hiyo
 NAIBU Waziri wa Maji Jumaa Aweso kushoto akilakiwa na Katibu Tawala wa wilaya ya Pangani Mwalimu Hassani Nyange wakati alipowasili
 NAIBU Waziri wa Maji Jumaa Aweso akikagua mradi wa Maji Kijiji cha Msaraza Kata ya Bushiri wilayani Pangani wakati wa ziara yake
Sehemu ya watumishi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) wakiwa kwenye ofisi ya mkuu wa wilaya ya Pangani wakifuatilia kwa umakini taarifa ya wilaya ya Pangani kuhusu maji aliyokuwa akisomewa Naibu Waziri wa Maji Jumaa Aweso


Naibu Waziri wa Maji Jumaa Aweso amemsimamizi kazi Meneja wa Wakala wa Maji Vijiji Pangani ( DM) RUWASA PANGANI Ladislaus Modestus huku akiagiza Mkurugenzi wa Usambazaji wa Maji na Usafi wa Mazingira (Ruwasa) Makao Makuu Mkama Bwire kuondoka naye kutokana na kushindwa kusimamia miradi ya maji huku mingine akiwa haitambui.

Pia ameagiza Meneja wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira wilaya ya Pangani Adam Sadick kusimamishwa kazi kutokana na kushindwa kusimamia miradi na bili za maji na kupelekea mamlaka kupata hasara. 

Agizo la Naibu Waziri Aweso linatokana na mhandisi huyo kushindwa kusimamia miradi ya maji wilayani humo na hivyo kupelekea wananchi kukosa maji hali ambayo ilimchukiza Naibu Waziri huyo ambaye alikuwa kwenye ziara wilayani humo.

Alisema kwamba mkurugenzi huyo anapoondoka aondoke na mhandisi huyo ambayo ameshindwa kuendana na kasi ya kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya maji ambayo ni muhimu kwa ustawi wa maisha yao .

Aidha alisema kwamba hatua hiyo inatokana na kwamba mhandisi huyo kupewa fedha za kusimamia mradi milioni 26 lakini bado hafiki kwenye maeneo yanayotekelezwa miradi

“Ndugu yangu wewe ni mhandisi wa maji upo hivi kama ungekwa daktari si ungekuta umekwisha kuua watu hatuwezi kukubali kuona hali kama hii na hatupo tayari kuona watu wa namna hii”Alisema

“Kutokana na kwamba Mhandisi huyo anapata fedha za kusimamia miradi ya maji kwenye wilaya hii na anashindwa kufanya hivyo hata ukiangalia msafara wangu ameupoteza wewe hautufai ni bora ukaondoka naye “Alisema Naibu Waziri Aweso. 

Hata hivyo Naibu Waziri huyo aliagiza kuundwe tume itakayobaini nini changamoto iliyopo kwenye usimamizi wa miradi ya maji Pangani jambo ambalo limepeleka kushindwa kufanyika kwa ufanisi mkubwa kama ilivyo maeneo mengine.

“Pia eneo la kibinda linachangamoto kubwa ya maji mimi kama mbunge wakati sijawa Naibu Waziri nilimfuata Waziri Kamwele nikamuambia suala hilo…niambieni kwamba mradi wa kibinda mabomba yanafika lini? Alihoji Naibu Waziri huyo.

Awali akizungumza wakati akitoa taarifa ya wilaya ya Pangani Mkuu wa wilaya ya Pangani Zainabu Abdallah alimueleza Naibu Waziri Aweso kwamba wananchi mji wa Pangani wana changamoto ya maji zaidi ya wiki tatu na hivyo kupelekea wananchi kukosa maji.

Mkuu huyo wa wilaya alisema kutokana na kwamba alikuwa likizo aliporudi alikwenda kwenye eneo la mradi kwa ajili kukagua maji na juzi ameenda kwenye mradi huo na amegundua changamoto tatu awali ni mfumo wa umeme kwa maelekezo wa meneja wa Pasawa.

Alisema tatizo hilo la mfumo wa umeme limesababishwa na tatizo kubwa la umeme kuingia na mfumo kuharibika huku akieleza kwamva changamoto nyengine ni pampuni kuwa na uwezo mdogo kuliko inavyopaswa kutumika kwenye maji.

“Wataalamu wanasema pampu ina uwezo mdogo mimi nashangaa wakati ikinunuliwa …mashine ya kuvuta umeme na kuzima mashine zipo mbili na moja ni mbovu na pampu zaidi ya milioni 22 ni mbovu anasema maelezo ya mkandarasi mfumo wa umeme mbovu”Alisema Mkuu huyo wa wilaya ya Pangani.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.