Habari za Punde

Jumuiya ya Wafanya Biashara Wenyeviwanda na Wakulima Zanzibar Kutumia Fursa ya Ushindani wa Kibiashara Kanda ya Afrika Mashariki -Waziri Balozi Amina.

 
Waziri wa Biashara na Viwanda Zanzibar Mhe Amina Salum Ali  akizungumza na  Jumuiya ya Wafanyabiashara, Wakulima na wenye Viwanda vidogo vidogo (chamber of commerce)  huko katika Ukumbi wa Ofisi ya Wizara ya Biashara na Viwanda, Migombani 
Washiriki wa Jumuiya ya  Wafanyabiashara, Wakulima na wenye Viwanda vidogo vidogo (chambe of Commerce) wakimsikiliza Waziri wa Biashara na Viwanda Mhe Amina Salum Ali  huko katika Ukumbi wa Ofisi ya Wizara ya Biashara na Viwanda,, Migombani
Rais  wa Jumuiya ya Wafanyabiashara, Wakulima na wenye Viwanda vidogo vidogo (Chamber of Commerce)  Toufiq S.Turky akielezea changamoto na fursa zilizopo za kibiashara katika soko la Afrika Mashariki  huko katika Ukumbi wa Ofisi ya Wizara ya Biashara na Viwanda, Migombani 

Na.Khadija Khamis -Maelezo Zanzibar.
Waziri wa Biashara na Viwanda Mhe Amina Salum Ali ameitaka Jumuiya ya Wafanyabiashara, Wakulima na wenye Viwanda vidogo vidogo (chamber of commerce)  kuitumia fursa walioipata ili kuingia katika  ushindani wa kibiashara Kanda ya  Afrika Mashariki .
Hayo aliyasema huko katika ukumbi wa Wizara ya Biashara na Viwanda, Migombani wakati akizungumza na Jumuiya ya Wafanyabiashara, Wakulima na wenye Viwanda vidogo vidogo katika kujipanga namna ya kuikabili fursa hiyo .
Alisema Serikali iko tayari kushirikiana na wafanyabiashara  kuimarisha mikakati ya kibiashara kwa wafanyabiashara wa Zanzibar , wakubwa wakati na hata wadogo wadogo ili kuweza kuwainua kibiashara .
Alisema Wizara ya  biashara na viwanda  itachukua juhudi za kushirikiana katika mipango ya kuzalisha bidhaa zilizobora na zenye kiwango jambo ambalo litatasaidia kuwaongeza nguvu ya kuyatumia masoko ya afrika mashariki
Aidha aliitaka jumuiya hiyo kuyatumia masoko ya afrika mashariki ikiwemo kongo sudan msumbiji kenya ili kukuza kiwango cha kibiashara hadi ikifika  julai mwakani iwe tayari matunda yameshaonekana
Hata hivyo alimpongeza Rais  wa Jumuiya ya Wafanyabiashara, Wakulima na wenye Viwanda vidogo vidogo (chamber of commerce)  Toufiq S.Turky kwa kuchaguliwa  kuwa  Mwenyekiti wa Afrika Mashariki  
Nae Rais  wa Jumuiya ya  (chamber of commerce)  Toufiq S.Turky alisema gharama zinazotozwa  zaidi ya mara tatu kwa  mizigo zinachangia kurudisha nyuma maendeleo ya kibiashara  .
Alifahamisha kuwa iwapo matatizo ya usafirishaji wa bidhaa utapofanyiwa marekebisho kwa  utasaidia kukuza kiwango cha kibiashara ambacho kitafikia ushindani wa kibiashara katika afrrika ya mashariki

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.