Habari za Punde

Ziara ya Kitalii Mji wa Bagamoyo kwa Mwaziri wa Kazi na Ajira SADC.

Mawaziri wa Kazi na Ajira kutoka Nchi za SADC wakizunguka katika mbuyu wenye umri wa Zaidi ya miaka 500 uliopo katika mji wa kihistoria KAOLE Bagamaoyo walipotembelea baada ya kumaliza Mkutano wa Mwaziri wa Kazi na Ajira na Wadau wa utatu wa Nchi za SADC ulifanyika Machi 5, 2020 JNICC Jijini Dar es Salaam, Tanzania.
Mawaziri wa Kazi na Ajira kutoka Nchi za SADC wakipata maelezo kutoka kwa mwongoza watalii wa makumbusho ya mji wa bagamoyo kuhusu kaburi la Binti Sharrfa sharifu aliyekuwa na nguvu za Ajabu na alifarika akiwa na umri wa miaka 13 katika mji wa  kihistoria KAOLE walipotembelea baada ya kumaliza Mkutano wa Mwaziri wa Kazi na Ajira na Wadau wa utatu wa Nchi za SADC ulifanyika Machi 5, 2020 JNICC Jijini Dar es Salaam, Tanzania.
Waziri wa Ajira, Kazi, Uzalishaji na Maendeleo ya Ujuzi wa Botswana, Mhe.Mpho Balopi akipiga ngoma za kikundi cha Utamaduni kutoka chuo cha Sanaa Bagamoyo TASUBA, kabla ya kutembelea makumbusho ya kihistoria KAOLE Bagamoyo, wanashuhudia kushoto ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenyeulemavu, Mhe.Jenista Mhagama na Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Bi. Zainabu Kawawa.
Mawaziri wa Kazi na Ajira kutoka Nchi za SADC wakinawa maji ya kisima cha Baraka kisichokauka wala kuongezeka maji yake yaliyo mita mbili kilichoko katika makumbusho ya KAOLE Bagamoyo walipotembelea baada ya kumaliza Mkutano wa Mwaziri wa Kazi na Ajira na Wadau wa utatu wa Nchi za SADC ulifanyika Machi 5, 2020 JNICC Jijini Dar es Salaam, Tanzania.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenyeulemavu, Mhe.Jenista Mhagama, akizungumza kwa Mawaziri wa Kazi na Ajira mara baada ya kuwasili kutalii katika makumbusho ya Kaole yaliyoko mji wa Bagamoyo Pwani, ili kujionea historia mbalimbali za wenyeji wa mji huo, Mawaziri hao walitembelea baada ya kumaliza Mkutano wao ulifanyika Machi 5, 2020 JNICC Jijini Dar es Salaam, Tanzania.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenyeulemavu, Mhe.Jenista Mhagama akiwa na wageni wake(Mawaziri wa Kazi na Ajira Nchi za SADC) baada ya kutembelea  Ngome kongwe katika makumbusho ya kihistoria  yaliyoko Mji wa Bagamoyo walipotembelea baada ya kumaliza Mkutano wa Mwaziri wa Kazi na Ajira na Wadau wa utatu wa Nchi za SADC ulifanyika Machi 5, 2020 JNICC Jijini Dar es Salaam, Tanzania.
Mawaziri wa Kazi na Ajira kutoka SADC waliosimama mbele wakiwa pamoja na wanafunzi wa mafunzo ya Ufundi katika fani mbalimbali walioko katika Chuo cha Don Bosco Jijini Dar es Salaam walipotembelea kujifunza baada ya Mkutano wa Mwaziri wa Kazi na Ajira na Wadau wa utatu wa Nchi za SADC ulifanyika Machi 5, 2020 JNICC Jijini Dar es Salaam, Tanzania.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenyeulemavu, Mhe.Jenista Mhagama akitoa maelezo kwa wageni wake(Mawaziri wa Kazi na Ajira Nchi za SADC) mara baada ya kuwasili Ngome kongwe katika makumbusho ya kihistoria Mji wa Bagamoyo walipotembelea baada ya kumaliza Mkutano wa Mwaziri wa Kazi na Ajira na Wadau wa utatu wa Nchi za SADC ulifanyika Machi 5, 2020 JNICC Jijini Dar es Salaam, Tanzania.
Wanafunzi wa Fani ya Ufundi magari kutoka chuo cha Don Bosco Jijini Dar es Salaam, wakionesha jinsi ya kurekebisha magari mbele ya Mawaziri wa Kazi na Ajira wa Nchi za Maendeleo Kusini mwa Afrika SADC (hawapo pichani) walipotembelea katika Chuo hicho kujifunza jinsi programu ya mafunzo ya ufundi katika Fani mbalimbali inavyofanyakazi ambapo Serikali ya Tanzania inawafadhili wanafunzi hao kupata mafunzo hayo

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.