Msajili wa Vyama vya
Siasa nchini (RPP), Mhe .Jaji Mstaafu, Francis Mutungi akifafanua jambo wakati
wa Mkutano wake na Viongozi Wakuu wa Vyama vya Siasa kuhusu zoezi la Uhakiki wa
Vyama vya Siasa nchini. Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini (ORPP) inatarajia
kufanya zoezi la uhakiki wa Vyama vya
Siasa nchini kuanzia tarehe 17 Machi, 2020 kwa lengo la kuimarisha uhai wa
vyama hivyo. Kushoto ni Naibu Msajili wa Vyama vya Siasa Mohamed Ally Ahmed.
Na
Mwandishi Wetu, MAELEZO DAR
ES SALAAM 10.3.2020
MSAJILI
wa Vyama vya Siasa Nchini, Jaji Mstaafu Francis Mutungi amesema zoezi la
uhakiki wa vyama vya siasa linalotarajia kuanza tarehe 17 Machi mwaka huu,
halina malengo ya kufuta usajili wa vyama hivyo na badala yake ni utekelezaji
wa matakwa ya Sheria ya Vyama vya Siasa ya mwaka 2019.
Jaji
Mutungi aliyasema hayo leo Jumanne (Machi 10, 2020), wakati wa Mkutano wake na
Viongozi mbalimbali wa vyama vya siasa vyenye usajili wa kudumu nchini
uliofanyika katika Ukumbi wa Ofisi Ndogo ya Bunge Jijini Dar es Salaam.
Jaji
Mutungi alisema malengo ya zoezi hilo litakoendeshwa na Ofisi yake ni kuona namna bora ya kujenga uelewa wa pamoaj
wa sheria ya vyama hivyo katika kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu wa
Rais, Wabunge na Madiwani unaotarajia kufanyika mwezi Oktoba mwaka huu.
Alisema
kuwa ni wajibu wa vyama vyote vya siasa kushiriki kikamilifu katika zoezi hilo na
kuwa Serikali haiwezi kuahirisha zoezi hilo na badala yake kuvitaka vyama hivyo
iwapo vina hoja ya msingi ni vyema zikawasilisha katika Baraza la Vyama hivyo
ili kuweza kupatiwa mwafaka wa pamoja wa makubaliano.
Kwa
mujibu wa Jaji Mutungi alisema katika muda uliobaki kuelekea uchaguzi mkuu, kwa
mujibu wa sheria Ofisi yake haiwezi kufuta usajili wa chama chochote cha siasa
na hivyo kuwataka Viongozi wa vyama vya siasa kuondoa dhana potofu kuwa
Serikali imepanga kufuta baadhi ya vyama vyenye usajili wa kudumu nchini kutoka
katika daftari la Msajili wa Vyama vya siasa.
Aliongeza
kuwa zoezi la uhakiki linaendeshwa kwa mujibu wa sheria na kuwa zoezi hilo si
geni kwa kuwa serikali imekuwa ikiendesha zoezi la uhakiki wa taasisi,
makampuni na mashirika mbalimbali na hivyo kwa vyama vya siasa zoezi hilo
halina utofauti wowote kama ilivyo kwa taasisi na mashirika yasiyo ya
kiserikali.
Jaji
Mutungi alisema hakuna sababu ya vyama hivyo kujenga hofu kuhusu zoezi hilo
kwani limekusudia kubaini changamoto mbalimbali zinazovikabili vyama vya siasa
nchini ili kuweza kutoa mapendekezo kwa Serikali na hivyo kuimarisha mshikamano
uliopo ili kukukuza na kuimarisha demokrasia nchini.
‘’Tumeamua
kukutana na wadau ili kuondoa ombwe kuhusu utekelezaji wa sheria ya Vyama vya
siasa ya mwaka 2019, kwani suala la uhakiki lipo kisheria, serikali inatambua
changamoto zilizopo katika vyama vya siasa na zoezi hili limekusudia kujenga
msingi wa pamoja wa kujitathimini wapi tulipotoka, tulipo na tunapokwenda’’
alisema Jaji Mutungi.
Akifafanua
zaidi Jaji Mutungi aliwataka Viongozi wa vyama vya siasa kulitazama zoezi hilo
katika taswira chanya kwa kuwa zoezi hilo limekusudia kujenga amani ndani ya
vyama hivyo katika kipindi hiki cha kuelekea katika uchaguzi mkuu wa Rais,
Wabunge na Madiwani unaotarajia kufanyika nchini kote mwezi Oktoba mwaka huu.
Kwa
upande wake, Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Prof. Ibrahim Lipumba
alisema vyama vya siasa havina pingamizi kuhusu zoezi la uhakiki na badala yake
aliitaka Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa kutoa muda wa miezi mitatu ili kuhakikisha
kuwa vyama vyote vinakamilisha masuala mbalimbali ya kiutendaji na taratibu
zote za msingi kama inavyoelekezwa katika sheria.
Aliongeza
kuwa kwa mujibu wa Sheria ya Vyama vya Siasa, vyama vyote vinapaswa kuwa na
wanachama wenye uwezo wa kiutendaji ikiwemo kuwa na kadi za uanachama, hivyo
Ofisi ya Msajili wa Vyama vya siasa havina budi kuongeza muda ili kutoa nafasi
kwa vyama hivyo kuweza kuhakiki wanachama wake.
Naye
Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa Nchini, John Shibuda aliitaka Ofisi ya
Msajili wa Vyama vya Siasa kutengeneza mwongozo wa mfumo wa adili za uongozi
ndani ya vyama vya siasa na utaratibu huo uendeshwe katika vikao vya Baraza la
Vyama vya siasa nchini.
Akitoa
salamu za shukrani kwa niaba ya Viongozi wa vyama vya siasa nchini, Mwenyekiti
wa Chama cha UDP John Cheyo aliipongeza Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa kwa
utaratibu wa kufanya vikao kwani utaratibu huo haukuwepo tangu kuanzishwa kwa
mfumo wa vyama vingi nchini miaka 28 iliyopita.
Msajili Msaidizi wa
Vyama vya Siasa Nchini, Sisty Nyahoza akiwasilisha mada kuhusu mambo
yanayotakiwa kuzingatiwa na Vyama vya Siasa wakati wa Zoezi la Uhakiki wa Vyama
vya Siasa katika mkutano wa Msajili wa Vyama vya Siasa(RPP), Mhe. Jaji Mstaafu,
Francis Mutungi na viongozi wakuu wa Vyama vya Siasa nchini leo jijini Dar es
Salaam. Mkutano huo ulihusu
kuwapitisha viongozi hao katika hatua zitakazopitiwa wakati zoezi la uhakiki wa
Vyama vya Siasa. Linalotarajiwa kuanza tarehe 17, Machi 2020.
Naibu Msajili wa
Vyama vya Siasa, Mohamed Ally Ahmed akifafanua jambo mbele ya Viongozi Wakuu wa
Vyama vya Siasa nchini wakati wa Mkutano wa Msajili wa Vyama vya Siasa (RPP), Mhe.
Jaji Mstaafu, Francis Mutungi (hayupo pichani) uliofanyika katika ukumbi wa
Ofisi Ndogo za Bunge jijini Dar es Salaam leo. Mkutano huo ulihusu kuwapitisha
viongozi hao katika hatua zitakazopitiwa wakati zoezi la uhakiki wa Vyama vya
Siasa. Linalotarajiwa kuanza tarehe 17, Machi 2020.
Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi - CUF
akichangia mada wakati wa Mkutano wa Msajili wa Vyama vya Siasa nchini (RPP),
Mhe .Jaji Mstaafu, Francis Mutungi (hayupo pichani) na Viongozi Wakuu wa Vyama
vya Siasa kuhusu zoezi la Uhakiki wa Vyama vya Siasa nchini. Ofisi ya Msajili
wa Vyama vya Siasa nchini (ORPP) inatarajia kufanya zoezi la uhakiki wa
Naibu Katibu Mkuu wa Chama
Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar Dkt. Juma Abdulla Juma Saadala akichangia mada
wakati wa Mkutano wa Msajili wa Vyama vya Siasa nchini (RPP), Mhe .Jaji
Mstaafu, Francis Mutungi (hayupo pichani) na Viongozi Wakuu wa Vyama vya Siasa
kuhusu zoezi la Uhakiki wa Vyama vya Siasa nchini. Ofisi ya Msajili wa Vyama
vya Siasa nchini (ORPP) inatarajia kufanya
zoezi la uhakiki wa Vyama vya Siasa nchini kuanzia tarehe 17 Machi, 2020
kwa lengo la kuimarisha uhai wa vyama hivyo.
Baadhi ya viongozi wa
vyama vya siasa nchini wakifuatilia mada wakati wa wakati wa Mkutano wa Msajili
wa Vyama vya Siasa nchini (RPP), Mhe .Jaji Mstaafu, Francis Mutungi (hayupo
pichani) na Viongozi Wakuu wa Vyama vya Siasa kuhusu zoezi la Uhakiki wa Vyama
vya Siasa nchini. Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini (ORPP) inatarajia
kufanya zoezi la uhakiki wa Vyama vya
Siasa nchini kuanzia tarehe 17 Machi, 2020 kwa lengo la kuimarisha uhai wa
vyama hivyo.
(Picha Zote na Ofisi
ya Msajili wa Vyama vya Siasa-ORPP)
No comments:
Post a Comment