Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akizungumza na baadhi ya Viongozi wa Mikoa Miwili ya Kaskazini na Kusini Pemba katika ukumbi wa Ikulu Ndogo Chakechake Pemba akiwa katika ziara yake ya siku mbili Kisiwani Pemba.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.
Ali Mohamed Shein amewataka viongozi wa Mikoa ya Pemba kuwatoa hofu wananchi juu ya maradhi yanayosababishwa na virusi vya
KORONA na badala yake waendelee kujikinga kama walivyopewa maelekezo na
wataalamu wa afya.
Rais Dk. Shein
aliyasema hayo leo huko katika Ikulu ndogo, Chake Chake, Mkoa wa Kusini Pemba,
wakati alipofanya mazungumzo na Viongozi wa Mikoa ya Pemba.
Katika maelezo yake
Rais Dk. Shein aliwasisitiza viongozi hao kuendelea na mikakati yao waliyoiweka
kisiwani humo katika mapambano ya janga hilo na kuwataka kuendelea kuhakikisha
wanatoa maelekezo kwa wananchi kama vile yanayotolewa na wataalamu wa avya.
Alisema kuwa viongozi
hao wa Mikoa yote ya Pemba wamefanya kazi kubwa na nzito hasa ikizingatiwa kuwa
dunia imepata mtihani mkubwa wa janga la vizurisi hivyo vya KORONA na ndio
maana WHO limetangaza kuwa hilo ni jaanga la dunia.
Rais Dk. Shein aleleza
namna Serikali zote mbili zilivyolifanyia kazi suala la kupambana na maradhi ya
virusi vya KORONA na kuonggeza kuwa kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa upande
wake ilitoa taarifa zake yakiwemo mambo kumi pamoja na kutoa taarifa kwa
kuwaeleleza wananchi juu ya ukweli wa janga hilo.
Alieleza jinsi
tahadhari zote zilizotolewa na Serikali kupitia wataalamu wake wa afya ikiwa ni
pamoja na uvaaji wa barakoa kwa wananchi wote na kutoa pongezi kwa wananchi
kisiwani humo kwa kuitikia wito huo.
Rais Dk. Shein alisema
kuwa yeye na Rais John Pombe Magufuli hawakuwa tayari kuzuia wananchi kusafiri
na kufanya shuhuli zao za kimaisha na badala yake waliwataka wananchi kuendelea
kuelimishwa juu ya kujikinga na janga hilo.
Aidha, Rais Dk. Shein
alipongeza juhudi zilizochukuliwa na viongozi hao wa Mikoa ya kisiwani Pemba na
kusisitiza kuwa ni vyema juhudi zikaendelezwa katika kuwaelimisha watu hasa
wale wa vijijini.
Alieleza kuwa wapo
baadhi ya watu ambao hawatoi ushauri mzuri kwa Serikali na wamekuwa wakitumia
mitandao ya kijamii vibaya kuilazimisha Serikali jambo ambalo Serikali haiko tayari
kulazimishwa katika kufanya wanavyotaka wao.
Hivyo aliwataka
viongozi hao kutowasikiliza watu wa aina hiyo na kuwataka kuendekea kuisikiliza
Serikali yao huku akiwataka kuendelea kutoa maelekezo sahihi kwa wananchi.
Rais Dk. Shein alisema kuwa jambo la msingi ni
kuzingatia afya na nidhamu katika kujikinga, kuwaelekeza wananchi namna ya
kujifunza pamoja na kujikinga kwani Tanzania bado haijafikia hatua ya
kuwafungia wananchi kutotoka nje.
Alieleza kuwa SMZ na
SMT haikatai kushauriwa lakini anaetaka kutoa ushauri ama maoni yake atoe kwa
mujibu wa sheria na taratibu zilizopo na sio kuandika mitandaoni kwani Serikali
zote mbili zitafanya lile ambalo zitahakikisha
zitawasaidia wananchi.
Alileza kuwa nchi
nyingi duniani zikiwemo za Ulaya zimekuwa zikishirikiana katika kupambana na
maradhi hayo na ndio maana Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaendelea
kushirikiana.
Dk. Shein alisisitiza
haja ya kuendelea kuwasisitiza wananchi kuvaa barakoa, kunawa mikono kwa maji
ya kutiririka, kutumia vitakasa mikono pamoja na kufuata taratibu zote za kinga
zinazotolewa na wataalamu wa afya pamoja na viongozi wa Serikali.
Akieleza haja kwa
Kamati ya Ulinzi na usalama kisiwani Pemba, Dk. Shein alisisitiza haja kwa
Kamati hiyo kufanya kazi zake ipasavyo ikiwa ni pamoja na kutumia taratibu za
kisheria katika kuwaelekeza wananchi juu ya mapambano ya janga hilo na
atakaekaidi ni vyema akachukuliwa hatua za kisheria.
Aidha, alieleza kuwa
Serikali haitowaonea wananchi bali itaendelea kuwaelekeza ukweli juu ya janga
hilo.
Alieleza kuwa ni
lazima viongozi hao wakawapongeza wananchi kwa kuendelea kuiamini Serikali yao
kwani wengi wao wanafuata taratibu na
maelekezo ya Serikali na yale maeneo ambayo bado hayajafanya vizuri katika kufuata
maelekezo ya kinga elimu iendelezwe ikiwa ni pamoja na kuwapeleka wataalamu wa
afya kwenda kuielimisha jamii hiyo.
Rais Dk. Shein
aliwataka viongozi hao kuendelea kuwasisitiza wananchi kufanya kazi kwa kasi
kubwa ikiwa ni pamoja na kuwataka wakulima kuzitumia vyema mvua za masika ili
chakula kiendelee kupatikana hapa nchini.
Pamoja na hayo, Rais
Dk. Shein aliwataka viongozi hao kuwaelekeza wafanyabiashara kuuza bidhaa zao
kwa kufuata misingi yote ya biashara kama ilivyowekwa na Serikali bila ya
kuwawekea wakati mgumu wananchi katika kupata bidhaa muhimu.
Alieleza kuwa kutokana
na kasi kubwa ya mapambano ya janga hilo zinavyoendelea hapa nchini anamatumaini
makubwa katika kufanikiwa kuyapiga vita maradhi yanayosababishwa na virusi vya
KORONA.
Aliwataka viongozi
kutojenga hofu na badala yake waendelee kupambana hasa ikizingatiwa kuwa
maradhi hayo ni thakili na ni adui asiyeonekana huku akisisitiza haja ya kutowafanyia
unyanyapaa wale waliokumbwa na maradhi hayo.
“Nakupongezeni kwa kufanya
kazi kubwa na nzito kwa mafanikio na hapana
hata mmoja aliyekuwa hajasikia namna viongozi wa Pemba mlivyofanya jitihada na
sote tumeridhika na juhudi zenu....dunia imepata mtihani, dunia imepata
msukosuko”,alisema Dk. Shein.
Aliwapongeza kwa dhati
viongozi hao kwa jitihada kubwa sana wanazozichukua viongozi hao katika
kupambana na janga hilo na kusisitiza kuwa hakuna wa kulaumiwa na kuwataka
kupeleka salamu zake kwa wananchi, viongozi wote wa Wizara ya Afya.
Pia, aliwapongeza
Walinzi wa Vikosi vya ulinzi na Usalama viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)
na wananchi wote pamoja na wafanyabiashaara na wasiofanya biashara kwa kutoa
misaada Unguja na Pemba katika kusaidia mapambano hayo.
Rais Dk. Shein
alitumia fursa hiyo kwa kumpongeza Makamo wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Idd
akiwa Mwenyekiti wa Kamisheni ya Kukabiliana na Maafa Zanzibar na Wajumbe wake
pamoja na Kamati ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya kupambana na janga hilo
kwa kufanya kazi vizuri.
Mapemba Waziri wa Nchi
Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Issa Haji Ussi Gavu,
akimkaribisha Rais Dk. Shein alimpongeza Rais Dk. Shein kwa hatua yake hiyo ya
kukutana na kufanya mazungumzo na viongozi hao wa Mikoa ya Pemba.
Nao Wakuu wa
Mikoa ya Pemba wakiwasilisha taarifa za
mikoa yao walieleza kuwa wananchi wanaendelea kushirikiana katika shughuli
mbalimbali za maendeleo na Serikali inaendelea kuwapelekea maendeleo wananchi
wake.
Walieleza kuwa Mikoa yao
inaendelea kupambana na suala zima la Udhalilishaji, rushwa pamoja na kupambana
na maradhi ya virusi vya KORONA, huku akisisitiza kuwa hali ya siasa katika
Mikoa hiyo vizuri.
Waliongeza kuwa
wananchi wanaendelea kushirikiana kama kawaida pamoja na kuhakikisha hali ya ulinzi na usalama iko
vizuri sambamba na kuhakikisha wafanyabiashara hawapandishi bei za vyakula hasa
kutokana na visingizio vya KORONA.
Aidha, walimpongeza
Rais Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli pamoja na Rais Dk.
Shein kwa kulisimamia vyema janga hilo kwa kuhakikisha wananchi wanaendelea na
shughuli zao za kimaisha bila ya kusitishwa usafiri, na kutowekwa karantini ya
kutokutoka ndani na kufunga mipaka.
Viongozi hao walielza
mafanikio yaliopatikana ikiwa ni pamoja na muitikio mkubwa wa wafanyabishara
kwa kuweka maji na vitakasa mikono, muitikio mkubwa kwa kujali muda wa huduma
za masoko, kuvaa barakoa, kuwapatia vyakula wagonjwa walioko makambini pamoja
na kutoa taaluma.
Walipongeza mashirikiano
makubwa wanayopata kutoka katika Mkoa wa Mjini Magharibi kwa kuhakikisha
wananchi wanaosafiri kwenda kisiwani Pemba wakitokea Unguja wote wanavuaa
barakoa.
Pia, viongozi hao walieleza
hatua zinazochukuliwa kuhakikisha wananchi wanavaa barakoa, kuondosha
mikusanyiko, kusimamia na kufuatilia watu wote waliopata maradhi hayo na wale
waliokuwa karibu na wagonjwa pamoja na wanaoingia katika Mkoani hiyo kwa
kuwaweka katika uangalizi maalum wa siku 14 wasafiri wanaoingia katika Mikoa
hiyo ili kujiridhisha iwapo hawajaambukizwa na maradhi hayo.
Pamoja na hayo, wakuu
wa Mikoa hao walieleza maafa ya mvua yalioathiri nyumba pamoja na mazao katika
Mikoa hiyo huku wakieleza kuwa licha ya athari hizo mvua hizo hazikuathiri sana
miundombinu ya barabara na madaraja hali iliyopelekea njia zote kuendelea
kupitika vizuri.
Viongozi hao kwa
pamoja walimpongeza Rais Dk. Shein kwa
hatua aliyoichukua yeye mwenyewe ya kwenda kisiwani Pemba na kuwapongeza kwa
juhudi zao wanazozichukua katika kupamabana na janga hilo kisiwani humo
Rajab
Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment