Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na
Michezo Dkt.Hassan Abbas akizungumza katika kikao cha Waziri wa Wizara hiyo
Dkt.Harrison Mwakyembe (kushoto) pamoja na Uongozi wa Arusha Press Club kuhusu
namna bora ya kutekeleza majukumu yao ya kutoa habari sahihi kwa wananchi leo
Jijini Dodoma.
Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo
Mhe.Dkt.Harrison Mwakyembe akipokea kipeperushi cha majukumu ya Uongozi wa Arusha Press Club mara baada ya
kumaliza kikao na Uongozi huo kuhusu namna bora ya kutekeleza majukumu yao ya kihabari leo Jijini Dodoma.
Na
Eleuteri Mangi, WHUSM, Dodoma
Wizara
ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo imezitaka ofisi za Umma kutoa taarifa
kwa wanahabari kwa kuwa siyo hisani na siyo hiyari, bali ni takwa la kisheria
kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ibara ya 18 (d).
Kauli
hiyo imetolewa na Waziri mwenye dhamana ya tasnia ya Habari Dkt. Harrison
Mwakyembe alipokutana na ujumbe wa viongzi wa Chama cha Waandishi wa Habari
kutoka mkoani Arusha pamoja na Asasi ya Vyombo vya Habari Mbadala (Alternative
Media) leo jijini Dodoma.
“Serikali
haina ugomvi na vyombo vya habari, bila vyombo vya habari hatutaweza
kuwahabarisha wananachi masuala mbalimbali ya maendeleo ya nchi yetu” amesema
Dkt. Mwakyembe.
Aidha,
amewakumbusha wanahabari kuwa kazi wanayofanya ni muhimu sana ambapo nchi
zilizoendelea bado wanatumia vyombo vyao vya habari ikiwemo Shirika la
Utangazaji la Uingereza (BBC) ambalo lina miaka zaidi ya 90 na linatangaza
habari zake kwa lugha zaidi ya 40 ili kuwafikia wananchi wake na dunia kwa
ujumla.
Kwa
upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari kutoka mkoa wa Arusha Bw. Claud Gwandu amemshukuru Waziri
Dkt. Mwakyembe kwa mapokezi, majadiliano yenye tija kwa uwazi na ukweli na
kumpongeza kwa kazi nzuri anayofanya katika sekta anazozisimamia.
“Tunamshukuru
Waziri kwa kutupa nafasi ili tuweze kushirikiana katika kuimarisha tasnia ya
habari iwe bora kwa mustakabali wanchi yetu” amesema Gwandu.
Aidha,
Mwenyekiti huyo amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John
Pombe Magufuli kwa kazi kubwa anayofanya kwa kutekeleza miradi mingi kwa
manufaa ya Watanzania na kusisitiza kwa mwenye macho haambiwi tazama.
No comments:
Post a Comment