Habari za Punde

DKT. ZAINABU CHAULA ARIDHISHWA NA MAENDELEO YA UJENZI WA JENGO LA PAPU *Kaziyakuchimbianguzo za kujengaghorofa 17 yakamilikakwaasilimia 75 *Ujenziwaofisi za PAPU kugharimushilingibilioni 33.7





Na Prisca Ulomi, WUUM, Arusha
Serikali yaridhishwa na maendeleo ya ujenzi wa jengo la ghorofa 17 za ofisi ya Makao Makuu ya Umoja wa Posta Afrika (PAPU) unaoendelea kufanyika Mkoani Arusha

Hayo yameelezwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Mawasiliano), Dkt.Zainabu Chaula ambapo jana alitembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa ofisi hizo mkoani humo akiwa ameambatana na viongozi wengine wa Serikali na PAPU akiwemo Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mary Makondo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Prof. Sifuni Mchome, Naibu Katibu Mkuu wa Sekta ya Mawasiliano, Dkt. Jim Yonazi, Katibu Mkuu Msaidizi wa PAPU, Kolawole Aduloju, na watendaji wengine wa Halmashauri ya Jiji la Arusha; na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania

Dkt. Chaula amesema kuwa ujenzi wa ofisi za PAPU utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 33.7 na ni mradi wa kimkakati na wa kibiashara nchini hususan kwa biashara ya posta nchinia mbapo inategemewa kukua kupitia mradi huu ambapo lengo la Serikali ni kuhakikisha kuwa nchi yetu inaendelea kukua zaidi kiuchumi na posta ni sehemu ya mkakati na ndio maana tunapitia mradi huu kila wakati ili kuhakikisha kuwa mradi huu unatekelezwa vizuri.

Ameongeza kuwa Serikali imejenga Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano na inahimiza matumizi ya TEHAMA, Shirika la Posta Tanzania (TPC) linatumia magari kutoa huduma zake kwa wateja ambapo moja ya jukumu lake ni kufanyabiashara hivyo TPC anatumia biashara mtandao kwa kuingia makubaliano na muuzaji na mnunuzi wa bidhaa kutoka nchi yeyote na zinakuja Tanzania na TPC anakuwa msafirishaji mkuu, hii ni fursa na ni jukumu langu kuhakikisha mawasiliano haya yanaendelea kukua hususani kupitia Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano

Naye msimamizi wa ujenzi wa jengo la PAPU, Mhandisi Hanington Kagiraki amesema kuwa jengo hili litakuwa na ghorofa 17 na ujenzi wake unagharamiwa kwa pamoja baina ya PAPU na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambapo hadi sasa kazi ya ujenzi na usimikaji wa nguzo za kujenga ghorofa 17 umefikia asilimia 75 ambapo jumla ya nguzo 145 zimezikwa kati ya nguzo 192 zinazohitajika kujengwa na mradi huu ni wa kipindi cha siku 900 na umeanza mwezi wa Januari 2020 na utakamilika mwaka 2022.

Katibu Mkuu Msaidizi wa PAPU, Kolawole Aduloju amesema kuwa anaishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa ushirikiano katika kujenga jengo hili na ujenzi unaendelea na wanaamini kuwa utakamalika kwa wakati

Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mary Makondo amesema kuwa Serikali imenufaika kwa kupata ardhi ili mradi huu uweze kutekelezwa na hadi sasa vijana 70 wamepata ajira na tunatarajia watanzania na wana Arusha wataendelea kupata ajira.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.