Habari za Punde

Wasimamizi wasaidizi wa Uchaguzi ngazi ya jimbo watakiwa kuzingatia sheria na maelekezo

Baadhi ya wasimamizi wasaidizi wa Uchaguzi wakiwa katika mafunzo ya vitendo yaliyoandaliwa na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar .


Na Jaala Makame Haji---ZEC
Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar ZEC imewataka wasimamizi wasaidizi wa Uchaguzi ngazi ya jimbo walioteuliwa kusimamia Uchaguzi katika Majimbo ya Uchaguzi ya Zanzibar kuifanya kazi hiyo kwa kuzingatia Sheria na maelekezo waliyopewa na Tume.

Mjumbe wa Tume hiyo Dk. Kombo Khamis Hassan alitoa ushauri huo wakati akifungua mafunzo ya siku tatu kwa Wasaidizi wasimamizi wa uchaguzi kwa Majimbo ya Unguja yaliyofanyika katika ukumbi wa Sheikh Idrisa Abdul Wakil Kikwajuni jijini Zanzibar.

Dk Kombo alisema Tume imekuwa ikiendelea kuchukua juhudi mbali mbali za kuwakutanisha Wadau wa uchaguzi wakiwemo Vyama vya Siasa, Waandishi wa habari, Asasi za Kiraia na Wadau wa kutoka katika makundi yenye mahitaji maalum kwa lengo la kuona uchaguzi wa mwaka 2020 unafanyika kwa kufuataa misingi ya Kidemokrasia na kudumisha Amani na utulivu hata baada ya Uchaguzi.

Akifunga Mafunzo hayo Mjumbe wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar Kanali Mstaafu Fetehe Saad Mgeni aliwataka Wasimamizi wa uchaguzi na Wasaidizi Wasimamizi kuhakikisha kila mwenye haki ya kuchagua na kuchaguzliwa anapata haki yake ili kuweka mustakbali mzuri wa uchaguzi.Mkuu wa mwaka 2020.

Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Sheria Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar Khamis Issa Khamis alisisitiza kuwa kazi za Uchaguzi zinahitaji umakini wa hali ya juu kati hatua zote muhimu ikiwemo hatua ya ujazaji wa fomu za matokeo ya Uchaguzi, utunzaji wa vifaa, kuhesabu kura na kutangaza matokeo.

Ndugu Khamis alifafanua kuwa Sheria ya Uchaguzi Namba 4 ya mwaka 2018 imeeleza makosa na adhabu kwa atakaye kwenda kinyume Sheria hizo na  aliwasihi wasaidizi wasimamizi wa Uchaguzi pamoja na Watakao pewa jukumu la kusimamia uchaguzi katika vituo vya kupigia kura kuzingatia zaidi Sheria za Uchaguzi ili kuepuka kuingia hatiani kwa mujibu wa Sheria.

Mkuu wa kurugenzi ya Elimu ya Wapiga kura, habari na Mawasiliano ya Umma Juma Sanifu Sheha alieeleza kuwa ZEC katika kuwaondolea usumbufu watu wenye mahitaji maalum wakiwemo watu wenye ulemavu imeandaa mikakati maalum ambayo itawawezesha kupiga kura wenyewe na kuingia katika vituo vya kupigia kura bila kukaa foleni.

Ndugu Sanifu alieendelea kusema kuwa, ZEC inatekeleza maelekezo ya Sera ya jinsia na ushirikishwaji wa makundi maalum ya mwaka 2014 iliyoanzishwa na Tume hiyo ili kuondosha usumbufu kwa makundi yenye mahitaji maalum wakiwemo Wanawake wanao nyonyoshe, watu wenye ulemavu, Wazee na Wajawazito.

Akieleza kuhusu upigaji kura kwa Watu wasioona alifafanua kuwa, Tume itaanda kifaa maalum cha Kupigia Kura kwa Watu wasioona (Tactile Ballot Folder) chenye maandishi ya nukta nundu ili nawao waweze kupiga kura wenyewe bila msaada wa mtu mwengine.

Msaidizi Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo Chwaka Wilaya ya Kati Mwanajuma Khalfan Machano mara baada ya kula kiapo cha utekelezaji wa majukumu yake katika ukumbi wa Sheikh Idrisa Abdul Wakil kikwajuni jijini Zanzibar aliahidi kufuata na kutekeleza taratibu zote walizoelekezwa na tume kupitia sheria na kanuni za uchaguzi.

Naye Msaidizi Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Shauri Moyo Wilaya ya Mjini Hashim Ali Suleiman alisema matarajio yao ni kuifanya kazi hiyo kwa uhuru na uwazi ambapo aliwataka wananchi kushiriki uchaguzi katika hatua zote za uchaguzi kutokana na Tume ya uchaguzi imejipanga kutoa huduma bila ya usumbufu wowote.

Mafunzo hayo ya siku tatu yalifanyika Unguja na Pemba ambayo yalifunguliwa  tarehe 22/8/2020 na kufungwa tarehe 24/8/2020.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.