Habari za Punde

Jamii yaaswa kutafuta njia bora za kusaidia watoto wanaoishi katika mazingira magumu

Spika wa Baraza la Wawakilishi Mhe. Zubeir Ali Maulid alipokuwa akisisitiza jambo alipokutana na uongozi wa Step Up Foundation walipofika Ofisini kwake Chukwani. Kulia ni Nae Mwenyekiti wa  Jumuiya ya Maendeleo ya Step Up Foundation inayosaidia Watoto yatima mama Asha Balozi.
Spika wa Baraza la Wawakilishi Mhe. Zubeir Ali Maulid akisikiliza kwa makini wakati alipokutana na uongozi wa Step Up Foundation walipofika Ofisini kwake Chukwani.
Spika wa Baraza la Wawakilishi Mhe. Zubeir Ali Maulid  akiwa katika picha ya pamoja na Uongozi wa  Step Up Foundation walipofika Ofisini kwake Chukwani.

Na Mwandishi wetu

Spika wa Baraza la Wawakilishi Mhe. Zubeir Ali Maulid ameishauri jamii na taifa kwa jumla kuangalia namna bora zaidi ya kusaidia watoto wanaoishi katika mazingira magumu hasa walioathirika na maambukizo ya maradhi ya ukimwi.

Amesema hali na namna wanayoishi Watoto hao ambao wamehifadhiwa katika vituo kadhaa binafsi kwa ajili ya kusaidiwa, hairidhishi na haiko rafiki katika upatikanaji wa huduma bora hasa wale walioathirika na maambukizo ya maradhi ya ukimwi kutoka kwa wazee wao.

Mhe. Zubeir ameeleza hayo ofisini kwake Chukwani wakati alipokuwa na mazungumzo  na uongozi wa jumuiya ya maendeleo ya baadhi ya wake wa viongozi wastaafu inayosaidia Watoto yatima .

Amesema baadhi ya taasisi binafsi zimeonekana kuwa tayari kusaidia katika upatikanaji wa huduma bora kwa watoto hao  lakini ipo haja kwa serikali kubuni mbinu bora Zaidi za kuisaidia ili kuwawezesha watoto hao kupata haki yao ya huduma zinazostahili.

Nae Mwenyekiti wa  Jumuiya ya Maendeleo ya Step Up Foundation inayosaidia Watoto yatima mama Asha Balozi, amewataka wajumbe wa baraza la wawakilsihi kuwa tayari kuchangia katika upatikanaji wa huduma zikiwemo za elimu ili kuwasaidia Watoto wanaoishi katika  mazingira magumu .

Kwa mujibu wa utafiti mdogo wa hivi karibuni wa Jumuiya ya Maendeleo ya Stepup Foundation inayosaidia Watoto yatima, zaidi ya wototo elfu 57 waliosajiliwa ni mayatima na wanaishi katika mazingira magumu.

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.