Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Hassan Mwinyi akisalimiana na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali pia Kaimu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Mhe.Simai Mohamed Said alipowasili viwanja vya Ukumbi wa Sheikh Idrissa Abduulwakil Kikwajuni Jijini Zanzibar katika Mkutano na Wafanyakazi wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii uliofanyika leo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Hassan Mwinyi (katikati) akifuatana na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali pia Kaimu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Mhe.Simai Mohamed Said (kushoto) Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Mhe.Idrisa Kitwana Mustafa wakati alipowasili viwanja vya Ukumbi wa Sheikh Idrissa Abduulwakil Kikwajuni Jijini Zanzibar katika Mkutano na Wafanyakazi wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii uliofanyika leo.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Hassan Mwinyi (katikati) akifuatilia kwa makini changamoto zilizotolewa na Wafanyakazi wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii katika Mkutano maalum na Wafanyakazi hao uliofanyika leo katika Ukumbi wa Sheikh Idrissa Abduulwakil Kikwajuni Jijini Zanzibar (kulia) Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali pia Kaimu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Mhe.Simai Mohamed Said (kushoto) Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais,Sera,Uratibu na Baraza la Wawakilishi Dk Khalid Mohamed Suleiman.
Baadhi ya Wafanyakazi wa idara mbali mbali katika Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani) wakati alipozungumza nao leo katika mkutano wa kusikiliza changamoto za wafanyakazi hao katika ukumbi wa Sheikh Idrissa Abdulwakil Kikwajuni Jijini Zanzibar.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Hassan Mwinyi alipokuwa akizungumza na Wafanyakazi wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii pamoja kutoa ufafanuzi wa changamoto mbali mbali zinazowakabili wanyakazi hao katika mkutano Maalum uliofanyika leo katika Ukumbi wa Sheikh Idrissa Abduulwakil Kikwajuni Jijini Zanzibar
Wafanyakazi wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kutoka kada mbali mbali wakiwa katika mkutano maalum wa kusikiliza changamoto zinazowakabili wafanyakazi hao katika ukumbi wa Sheikh Idrissa Abdulwakil Kikwajuni Jijini Zanzibar leo ambapo mgeni rasmin alikuwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi .
Wafanyakazi wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kutoka kada mbali mbali wakiwa katika mkutano maalum wa kusikiliza changamoto zinazowakabili wafanyakazi hao katika ukumbi wa Sheikh Idrissa Abdulwakil Kikwajuni Jijini Zanzibar leo ambapo mgeni rasmin alikuwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi 
Mchangiaji Hafidh Sheha Hassan katika kitengo cha maradhi ya Ngozi na maradhi ya kujamiiana akiwasilisha mchango wake katika Mkutano maalum wa Wafanyakazi wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii uliofanyika leo katika Ukumbi wa Sheikh Idrissa Abduulwakil Kikwajuni Jijini Zanzibar chini ya Mwenyekiti wake Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Hassan Mwinyi (hayupo pichani).
Muuguzi na Mkunga Rukia Balo kutoka Mpendae akiwasilisha mchango wake katika Mkutano maalum wa Wafanyakazi wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii uliofanyika leo katika Ukumbi wa Sheikh Idrissa Abduulwakil Kikwajuni Jijini Zanzibar chini ya Mwenyekiti wake Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Hassan Mwinyi (hayupo pichani).

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Hassan Mwinyi (katikati) akisikiliza michango na changamoto zilizotolewa na Wafanyakazi wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii katika Mkutano maalum na Wafanyakazi hao uliofanyika leo katika Ukumbi wa Sheikh Idrissa Abduulwakil Kikwajuni Jijini Zanzibar (wengine kulia) Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Kazi, Uchumi na Uwekezaji Mhe.Mudrik Ramadhan Soraga na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali pia Kaimu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Mhe.Simai Mohamed Said (kushoto) Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais,Sera,Uratibu na Baraza la Wawakilishi Dk. Khalid Mohamed Suleiman na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais,Katiba,Sheria,Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe Haroun Ali Suleiman.

Dk.Sanaa Suleiman Said kutoka SUZA akiwasilisha mchango wake katika Mkutano maalum wa Wafanyakazi wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii uliofanyika leo katika Ukumbi wa Sheikh Idrissa Abduulwakil Kikwajuni Jijini Zanzibar chini ya Mwenyekiti wake Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Hassan Mwinyi (hayupo pichani).[Picha na Ikulu] 31/12/2020.
No comments:
Post a Comment