Habari za Punde

Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo atembelea viwanja vya michezo vya Amaan, Mao Dze Dung na Kitogani

Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe. Tabia Maulid Mwita akipata maelezo kutoka kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kuhusu Uwanja wa mao Ze Dong Mhe Omar Hassan King alipofika kuukagua Uwanja huo
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe. Tabia Maulid Mwita akitoa maagizo kwa watendaji na wasimamizi wa viwanja kukiboresha kiwanja 
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe. Tabia Maulid Mwita akiambatana na  Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo huku akipata maelezo juu ya Uwanja wa Mao
 

Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe. Tabia Maulid Mwita alisema anataka wasimamizi wa viwanja wahakikishe wafanyakazi wanapatiwa vitendea kazi vya kisasa, vigari vya kufyekea, ofisi na upatikanaji wa maji  muda wote. zungumzeni na ZAWA ili suala la maji hasa ya kunywa lipatiwe ufumbuzi.

Nisisitize Mipango yote ambayo imepangwa na Wizara ya kukiboresha  kiwanja cha Mao ze dong ikiwemo ujenzi wa chumba cha kubadilishia nguo (changing room) ianze mara moja bila ya kusubiri ugeni wa wachezaji wa kimataifa.

Wafanyakazi wana dhamana kubwa ya kuvitunza viwanja vya michezo vidumu katika hali ya usafi  ndani na nje. Kila mmoja atimize wajibu wake  kwa mujibu wa nafasi yake ili sekta ya michezo iweze kuimarika.   

Taa za chumba cha viongozi mashuhuri (VIP) katika kiwanja cha Amani zifanyiwe matengenezo ya haraka hakuna sababu ya kusubiria mpaka kuwe na vikao na sherehe ndio zitengenezwe.

Kikundi cha Sanaa ya taarab asilia lazima kifufuliwe ili kitumike katika shughuli mbali  mbali za kitaifa sio kwenda kuvikodi vikundi vyengine vya sanaa.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.