Habari za Punde

Rushwa ya muhali ndio kichocheo kikubwa cha kupotoka kwa Ngono - Makala

 


                         

Na, MOHAMMED SHARKSY


KUPOTOKA KWA NGONO (SEXUAL DEVIATION)

Kupotoka kwa ngono (sexual deviation)  ni janga kubwa lilioikumba jamii yetu, rushwa ya muhali ndio kichocheo kikuu cha ongezeko la kupotoka kwa ngono na unyanyasaji wa kijinsia.

Katika siku za hivi karibuni kumetokezea kesi za uzalilishaji wa kijinsia hasa kutoka  jamii ya kiume dhidi wanawake na watoto kiasi ambacho kila uchao katika vyombo vyetu vya habari vinazungunzia matukio haya ya uhalifu,mbali   kwamba vyombo vya sharia kama  polisi na mahakama vinafuatilia kwa ukamiliffu katika kutatua tatizo hili bado limekuw kidonda ndugu.

Makala hii Imeona kuna umuhimu wa kuzungunguzia hali halisi ilivyo , hasa kutokana na chanzo  chake kikuu huwa kinasabishwa na kupotoka kwa ngono

Kupotoka kwa ngono (sexual deviation) inawezeka ikawa ni  laana inayofanywa na baadhi ya watu kutokana na ujinga wa kutojitambuwa katika mzingira fulani au tunaweza kukasema ni ugonjwa wa akili  ambao  mara nyingi unapoanza unaonekana ni hali ya kawaida tu na huenda pasiwepo na jitihada yoyote ya kupata msaada wa kimatibabu mpaka hali itakapokuwa mbaya au kuzidiwa

Ngono/tendo la ndoa ni ile hali ya faraha ya kuonana kimwili  baina ya mke na mume ,ni zawadi  maalumu kutoka kwa Mungu inapofanywa katika ndoa kwa raha na bashasha tele  ndani yake kukiwa na utulivyo  katika moyo . Kufurahiana na kuonana kimwili ni jambo la kutiliwa maanani katika ndoa.

Mungu aliumba hali ya kuonana kimwili kuwa uhusiano katika ya mke na mume katika ndoa.  Na ifahamike  kwamba kufanya  tendo la ndoa kinyume na maumbile ni haramu na   haikubaliki katika dini zetu zote,

NINI MAANA YA KUPOTOKA KWA NGONO KIAFYA?

Kupotoka kwa ngono ni ugonjwa wa akili unaompata binadamu  na kuifanya akili yake iwe na matamanio kinyume cha fikra umri na uhalisia ulivyo.

AINA ZA KUPOTOKA KWA NGONO

 Ziko aina nyingi sana za Kupotoka kwa ngono, zifuatazo ni aina chache na maarufu sana  katika jamii zetu hasa katika hizi nchi za dunia ya tatu kama  Zanzbar na T anzania kwa jumla.

Ø  Kupiga bodi (Voyerisim) , hii ni ile hali inayomfanya mtu kuchungulia madirishani au kupanda kuta za majumbani mwa watu na kuchungulia watu wakiwa wamelala na familia zao kwa lengo la kiujifurahisha na   kujisikia  kwamba matamanio yake yamekamilika

Ø  Kuingilia watoto wadogo kinyume na maumbile ya  kawaida. Hii humtokezea mtu mwenye umri mkubwa   kwa kujitosheleza na matamanio yake kwa kumuingilia mtoto

Ø  Kusagana (exhihibitionism).hii ni hali inayowafanya wanawake au wasichana wa umri mkubwa kufanya tendo la mapenzi  kwa kuchezeana kwenye tupu zao ilimradi wajizirishe kuondowa hisia zao za mapenzi

Ø  Kuingiliana kwa wanaume kwa wanaume. Hii ni mila potefu ambayo hata katika dini  zote zimeharamisha kitendo hichi lakini hufanywa na baadhi ya wanaume ili kumalizia matamanio yao ya mapenzi

Ø  Kubaka. Hiki nikitendo cha kijinai kinacho fanywa na wanaume kumlazimisha kufanya tendo la ndoa kwa kumuingilia mwanamke  bila ya ridhaa yake mwenyewe .

Ø  Sexology;     Ni wale wat u ambao wanjisikia  kama kwamba wamefanya tendo la ndoa pale wanpoonyesha jamii sehemu za siri bila ya aibu  bila kujali umri au rika ya mtu ilivyo .

Ø  Zoophilia wale watu wanajiridhisha hisia zao kwa kufanya  tendo la ndoa na wanyama 

Ø  Fetishism ni wale watu ambao wanatumia vitu visivyokuwa na uhai  kwa kufanya tendo la ndoa ili kujiridhisha, mara nyingi hutumiwa sana na wanawake  kama bilingani, muhogo, ndizi nk.

Ø  Frotteurisme ni ile jamii ya watu wanojiridhisha wakihisi wamesha fanya tendo la ndoa pale  wanapo jigusanisha sehemu zao za siri na mtu mwengine pindi ambao wamevaa nguo, hii sana huwa inatokezea kwenye vyombo vya usafiri kama vile kwenye dala dala  pindi pale watu wanaposimama ,na hii hufanyika sana kwa wanaume.

Ø  Masterbeshan/kupiga beshion.Hii ni ile ya wanaume kusuguwa uume wake kwa milihaji  ya kujitowa  shahawa/manii ili kujiridhisha kama vile amefanya tendo la ngono.

MATIBABU YA  KUPOTOKA KWA NGONO

Ø  Kupatiwa ushauri nasahaha   kuhusiana na mambo ya ngono salama na athari zake

Ø  Kutumia dawa za kemikali zinazozosaidia kupunguza vichochezi vya ngono (lutilizing hormones releasing argonisting)

Ø  Kuangalia historia ya mgonjwa  katika kumbukumbu ya magonjwa ya akili katika familia

Ø  Kuwashauri watu  kupunguza msongo wa mawazo na kuwa huru kujieleleza   kwa hali yeyoyte

Ø  Kuwashajihisha walengwa wa vitendo hivi kusoma  vitabu vitakatifu na kujuwa juu ya maamrisho na makatazo ya alwah.

MADHARA YA KUPOTOKA KWA NGONO.

Mara nyingi sana madhara ya kupotoka kwa ngono yanawaelemea sana wanawake kuliko wanaume.

Ø  Kuongezeka kwa matukio ya udhalilishaji wa kijinsia .

Ø   Wanawake kuathirika kwa magonjwa ya zinaa kama vile Ukimwi,kaswende,kisonono, nk.

Ø  Ufanyaji wa mapenzi ya ngono potofu usiokuwa na msukumo wa kutosha  hasa kwa wanawake huwafanya waishiwe na msisimko  na kuzifanya sehemu zao za siri kutowa ute unaoweza kuwakinga na michubuko na hivyo  kuwasababishia michubuko itakayoweza kuleta m madhara makubwa katika uke wao.(hii nikutokana na kukosa ridhaa yake ya kufanya tendo la ndoa)

Ø  Kupotezea haiba zao kwa jamii

Ø  Kathirika kisaikolojia

Ø  Kupata  mimba sisizotararajiwa

Ø  Kongezeka kwa watoto wa mitaani.

Ø  Kuparaganyika kwa familia

Ø  Kongezeka kwa vifo vya wanawake visivyotarajiwa kama kujiuwa kwa makusudi kutokana nakadhia ya kubakwa .

Ø  Kuongezeka kwa vifafa vya mimba kutokana na mimba za utotoni katika umri mdogo katika miaka ya kumi  mpaka kumi na tano.

Ø  Kuongezeka kwa wanawake tegemezi.

Ø  Kupata kwa maambukizi ya viungo vya ndani vya uzazi kama vile shingo ya kizazi,mirija ya uzazi kwa ujumla wake kama tatizo la PID,(Pelvic Infamatory diseases tatizo ambalo linaweza kuathiri mfumo wake wa uzazi.

CHANGAMOTO

Akizungumza na  mmoja kati ya Afisa Ustawi  wa jamii wa Wilaya ambae hakutaka jina lake kutajwa alizungumzia  changamoto zinazowakabili sana ni kwamba makosa mengi ya udhalilishaji  wa kingono na kijinsia yanaongezeka kwa kasi zaidi kwasababu zifuatazo kama vile ruchwa/rushwa ya muhali kwa wanafamilia na wanajamii,kutowajibika kwa  baadhi ya watendaji,kesi kuchukuwa muda mrefu, kukosa imani ya kiroho,wazazi kutokuwa karibu na watoto wao ,matumizi mabaya ya mitandao na mwisho kuondoka kwa malezi ya kizamani

USHAURI

Sio watu wote wanayofanya vitendo vya udhallishaji  wa  ngono potovu kwamba wana makosa  baadhi yao ni wagonjwa wa akili  kwa hiyo serikali na jamii isichukulie kwa urahisi katika  kutowa maamuzi yake  kabla ya uchunguzi yakinifu .na iwapo itakugundulika na makosa hatua kali  za kisheria zichukulie zidi yao.

Imetayarishwa na:

Mohammed Sharksy .

Mkufunzi Msaidizi

Kutoka Skuli za Sayansi za Afya

Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar, SUZA

0777432493 au email: mohammed.rashid96@yahoo.com ruruma96@gmail.com

 

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.