Habari za Punde

Watendaji Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais watakiwa kuendeleza mashirikiano

Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais  Mhe  Dkt Saada Mkuya akipokea Mafaili ya Ofisi kutoka kwa Kaimu Waziri Dkt Khalid  Salum Mohamed ambae ni Waziri  wa nchi  Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Uratibu wa shughuli za Baraza la Wawakilishi

 Kaimu Waziri Dkt Khalid  Salum Mohamed ambae ni Waziri  wa nchi  Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Uratibu wa shughuli za Baraza la Wawakilishi akipiga makofi baada ya kumkabidhi makabrasha ya Ofisi kwa  wa nchi Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais  Mhe  Dkt Saada Mkuya

Na.Raya Hamad – OMKR .

Watendaji wa Ofisi ya  Makamu wa Kwanza wa Rais wametakiwa kuendeleza  mashirikiano kiutendaji  kwa lengo la kutekeleza vyema majukumu  malengo na matarajio ya Serikali kwa kuzingatia maagizo aliyoyatoa  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi  Mhe Dkt Hussein Mwinyi 

Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais  Mhe  Dkt Saada Mkuya ameyasema hayo mara baada ya makabidhiano ya  Ofisi hio na aliyekuwa Kaimu Waziri Dkt Khalid  Salum Mohamed ambae ni Waziri  wa nchi  Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Uratibu wa shughuli za Baraza la Wawakilishi

Serikali ya awamu ya nane  inadhamira ya kuondosha kero zinazowakabili wananchi hivyo atahakikisha malengo hayo anayatimiza   kwa mashirikiano ya pamoja  na wakuu wa Taasisi zote na wafanyakazi katika  kuwatumikia wananchi na kuleta maendeleo ya jumla

Dkt Saada amewaomba wafanyakazi kuendelea kumuombea dua aliekuwa Makamu wa Kwanza wa Rais marehemu Maalim Seif Sharif Hamad aliefariki Febuari 17 mwaka huu ambae aliacha msingi mzuri wa majukumu ya Ofisi hio na jamii kwa ujumla

Akizungumzia changamoto zinazoikabili Ofisi hio Dkt Saada amesema  ni muhimu kuangalia mapungufu yaliyopo na kuyapatia ufumbuzi ikiwemo wafanyakazi kupata stahiki zao, kuandaa utaratibu wa kuyalipa madeni pamoja na kuziangalia namna bora ya kuzipitia sheria

‘tuhakikisha tunasimamia stahiki za wafanyakazi ila niwaombe sana wakuu wa taasisi  kuwafahamisha wafanyakazi kutofanya kazi kwa mazowea au kupitia migongo ya wengine kwani  wapo baadhi ya wafanyakazi hawana ari ya kiutendani hivyo  wajiandae maana tunataka kuona vipi mshahara wake anautendea haki  kiutendaji’ alisisitiza Dkt Saada

Aidha Mhe Saada amesema Ofisi ya  Makamu wa Kwanza wa Rais inasimamia masuala mtambuka hivyo  wakuu wa Taasisi wanawajibu wa kusimamia vyema vyanzo vya mapato  na kuchangia ukuwaji wa uchumi kama ilivyokusudiwa

Nae  Waziri  wa nchi  Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Uratibu wa shughuli za Baraza la Wawakilishi  Dkt Khalid  Salum Mohamed ambae alikuwa akikaimu  Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais amewashukuru watendaji na wafanyakazi wote na  kuwataka kumpa mashirikiano Mhe Saada ili aweze kutekeleza vyema majukumu yake

Akitoa shukurani kwa niaba ya watendaji wa Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Mkurugenzi kutoka Mamlaka ya Mazingira ndugu Sheha Juma Mjaja wameahidi kumpa mashirikiano na upendo katika utekelezaji wa majukumu ya kazi na kuhakikisha ofisi inakwenda sambamba na dhamira ya Serikali ya kuitumikia jamii

Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais  inatekeleza majukumu yake kupitia Ofisi ya faragha, Idara ya mipango Sera na utafiti, Idara ya Uendeshaji na Utumishi , Idara ya mazingira, Idara ya Watu wenye Ulemavu,  Mamlaka ya Mazingira, Tume ya Ukimwi, Tume ya Kuratibu na Udhibiti wa Dawa za Kulevya na Afisi Kuu Pemba ambapo  inawafanyakazi 306  Unguja na Pemba kati yao 156 wanawake na 150 wanaume .

 

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.