RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi
akiwa na Mkewe Mama Mariam Mwinyi wakisalimiana na kuagana na Makamu wa
Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe.Hemed Suleiman Abdulla, katika Uwanja wa Ndege wa
Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar, 26/5/2021,akielekea Nchini Msumbuji kuhudhuria
Mkutano wa SADC unaotarajiwa kufanyika Jijini Maputo Msumbiji.RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na kuagana na Viongozi wa
Serikali katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar,
akielekea Nchini Msumbiji kuhudhuria Mkoato wa SADC unaotarajiwa kufanyika
kesho Jijini Maputo Msumbiji
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi na
Mkewe Mama Mariam Mwinyi, wakisalimiana na Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na
Usalama Zanzibar, katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar,wakati
akielekea Nchini Msumbuji kuhudhuria Mkutano wa SADC unaotarajiwa kufanyika
kesho Jijini Maputo
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la MapinduziDk. Hussein Ali Mwinyi
ameondoka nchini leo kuelekea Maputo nchini Msumbiji kwa ajili ya kuhudhuria
Mkutano wa dharura wa Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika
(SADC), utakaofanyika nchini humo Mei 27,2021.
Akiondoka katika kiwanja cha ndege cha
Kimataifa cha Abeid Karume Zanzibar, Rais Dk. Mwinyi aliagwa na Viongozi mbali
mbali wa Serikali wakiongozwa na Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Hemed
Suleiman Abdallah pamoja na viongozi wengine.
Mkutano huo wa nchi za (SADC) unaofanyika
nchini Msumbuji unatarajia kujadili masuala ya hali ya ulinzi na usalama unawajumuisha
viongozi wakuu kutoka nchi za Jumuiya (SADC) zikiwemo Msumbiji, Malawi,
Tanzania, Botswana, Afrika Kusini, na
Zimbwabwe.
Rais Dk. Mwinyi anatarajia kurejea nchini
Alkhamis ya Mei 27 mwaka huu.
Rajab
Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024
2231822
E-mail:
rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment