Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyejkiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi Amekutana na Kuzungumza na Mwakilishi Mkaazi wa UN Women Nchini Tanzania Ikulu Zanzibar.

 

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiagana na mgeni wake Mwakilishi Mkaazi wa UN Women Nchini Tanzania Bi.Hodan Addou, baada ya kumaliza mazungumzo yao yaliofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na Mwakilishi Mkaazi wa UN Women Nchini Tanzania Bi. Hodan Addou, alipofika Ikulu Jijini Zanzibar kwa mazungumzo na kujitambulisha, mazungumzo hayo yaliofanyika katika ukumbi wa Ikulu Zanzibar.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akimsikiliza Mwakilishi Mkaazi wa UN Women Nchini Tanzania Bi.Hodan Addou, wakati akimkabidhiwa  mkoba ukiwa na ujumbe  “Wanawake Wana Haki ya Kuongoza” , baada ya kumaliza mazungumzo yao yaliofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amezungumza na Mwakilishi mkaazi  wa ‘UN Women Tanzania’ Hodan Addou, aliefika Ikulu Jijini Zanzibar.

Dk. Mwinyi amesema Serikali iko makini kuhakikisha wanawake wa Zanzibar wanapata haki zao pamoja na kuondokana na vitendo vyote vya ukandamizaji, ikiwemo udhalilishaji dhidi yao na watoto.

Aidha, alisema Serikali imekuwa ikiwateua wanawake zaidi katika nafasi mbali mbali za uongozi sio kwa upendeleo, bali kutokana na juhudi,  uwezo na uaminifu  mkubwa walionao.

Nae, Mwakilishi Mkaazi wa ‘UN Women Tanzania’ Hodan Addou alitoa pongezi kwa Rais Dk. Mwinyi kwa juhudi zake za kuimarisha Uwakilishi wa wanawake katika Uongozi, sambamba na juhudi zinazofanyika katika kukabiliana na vitendo vya udhalilishaji dhidi ya wanawake na watoto.

Alisema UN Women Tanzania itaendelea kushirikiana na Serikali ili kuhakikisha wanawake wa Zanzibar wanapiga hatua kubwa ya maendeleo ya kiuchumi.

Alisema ana imani kubwa kuwa sekta ya Uchumi wa Buluu italeta faida kubwa kwa wanawake, hivyo akaunga mkono juhudi za Serikali zinazoendelea kuchukuliwa kuimarisha sekta hiyo, ili kuinua hali zao kiuchumi.

Abdi Shamna, Ikulu Zanzibar

Postal Address: 2422 Tel.:0777476982. Fax: 024 2231822 

 E-mail: abdya062@gmail.com

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.