Habari za Punde

Mahakimu watakuwa kuwa waadilifu wanapotekeleza majukumu yao

 Na Mwashungi Tahir  Maelezo  9-7-2021

Jaji Mkuu wa Zanzibar Mhe Omar Othman Makungu  amewataka mahakimu kufanya kazi zao kwa uadilifu ili waweze kuondokana na malalamiko katika sehemu zao za kazi wanazotarajiwa kuzifanya kila siku.

 

Hayo ameyasema  huko katika ukumbi wa Vuga wakati alipokuwa akiwaapisha   Mahakimu  Haroub Amour Bakari na Hidaya Muhamed Mussa kuwa wasuluhishi na waamuzi katika kitengo cha usuluhishi wa migogoro ya kazi kilicho chini ya kamisheni ya kazi.

 

Amesema kiapo hicho kimefanywa chini ya kanuni ya kumi na moja no(5) ya usuluhishi na uwamuzi wa  kanuni za mwaka elfu mbili na kumi na moja 2011.

 

Aidha amesema kutokana na kuapishwa kwa wasuluhishi na waamuzi hao kutazidisha  idadi ya wasuluhishi na waamuzi  katika shughuli za kazi  na kutarajia kwenda vizuri kazi hizo za kila siku.

 

 

Vile vile  Jaji Omar amewataka mahakimu hao  kuacha upendeleo katika sehemu zao za  kazi na kujitahidi  kutekeleza majukumu yanayowakabili  na kuondosha malalamiko kwa wananchi  kwa haraka ili waweze  kuondokana   na mrundikano wa malalamiko yanayohusu sehemu za kazi.

 

Hata hivyo amewasisitiza kufanya kazi kwa mashirikiano na  kuwatakia mafanikio mazuri katika utekelezaji wa kazi zao za kila siku na kuepuka kuweko na migogoro.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.