RAIS wa Zanzibar
na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amempongeza
Kiongozi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto (UNICEF) ofisi za
Zanzibar, Laxm Bhawani kwa kazi kubwa na
nzuri inayofanywa na Ofisi hiyo na
akamhakikishia kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendelea kumuunga mkono
ili kufikia mafanikio katika maeneo anayofanyia kazi.
Dk. Mwinyi amesema hayo leo Ikulu Jijini hapa, wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto (UNICEF), Ofisi za Zanzibar Laxmi Bhawani.
Alisema Ofisi hiyo imekuwa ikifanya kazi kubwa katika kuhakikisha huduma mbali mbali ikiwemo za Afya na Elimu zinaimarika hapa nchini, sambamba na kuondokana na umasikini pamoja na utapia mlo kwa watoto.
Alisema upatikaji wa lishe kwa watoto ni jambo muhimu na akabainisha kazi kubwa inayopaswa kufanyika kufanikisha jambo hilo, kwa kuzingatia takwimu zilizopo za watoto wenye utapia mlo.
Alisema katika kuimarisha huduma za Afya, Serikali imekuwa ikifanya juhudi kubwa katika uwekaji wa miundo mbinu katika sekta hiyo pamoja na kuwajengea uwezo watendaji wake.
Dk. Mwinyi, alitolea mfano wa dhamira ya Serikali ya kujenga Hospitali katika Wilaya zote Unguja na Pemba na hivyo kuwepo mahitaji makubwa ya wafanyakazi wa huduma za Afya katika nyanja mbali mbali.
Rais Dk. Mwinyi,
alisema Serikali kwa kushirikiana na wadau mbali mbali, imekuwa ikifanya juhudi
kuona kwa namna gani itaweza kuimarisha kiwango cha elimu hapa nchini kupitia
sera ya elimu iliopo.
Mapema, Kiongozi
wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia watoto UNICEF, Ofisi ya Zanzibar
Laxmi Bhawani, alimueleza Rais Dk. Mwinyi
masuala mbali mbali yanayotekelezwa na Ofisi yake, ikiwemo ya
kufanikisha Programu ya Ulimwengu ya kuwarejesha watoto shule, mitaala ya
walimu ya kuinua viwango vya ufundishaji, sambamba na hatua
ya kushirikiana na taasisi mbali mbali,
ikiwemo Mradi w akunusuru Kaya maskini (TASAF) katika kufanikisha mpango wa kupunguza umasikini
nchini.
Kitengo cha habari,
Ikulu Zanzibar
No comments:
Post a Comment