Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizungumza na kuwapongeza Viongozi na Wachezaji wa Timu ya Taifa ya Mpira wa Miguu kwa Watu wenye Ulemavu, kufuatia kufuzu kushiriki katika Kombe la Dunia kwa Watu wenye Ulemavu 2022 Nchini Uturuki. Hafla hiyo iliyoambatana na Chakula cha Mchana imefanyika leo tarehe 07 Disemba 2021 katika Viwanja vya Ikulu Jijini Dar es salaam.
Baadhi ya wachezaji wa Timu ya Taifa ya Mpira wa Miguu kwa Watu wenye Ulemavu ambao wamefuzu kushiriki katika Kombe la Dunia kwa Watu wenye Ulemavu 2022 Nchini Uturuki wakiwa katika hafla hiyo katika Viwanja vya Ikulu Jijini Dar es salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiwa na Baadhi ya Viongozi wa Timu ya Taifa ya Mpira wa Miguu kwa Watu wenye Ulemavu baada ya kuzungumza nao leo tarehe 07 Disemba 2021 katika Viwanja vya Ikulu Jijini Dar es salaam.
WAZIRI KOMBO APOKEA MAGARI KUTOKA QATAR
-
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imepokea magari
mawili aina ya Land Cruiser Prado kutoka Taifa la Qatar kwa ajili ya
kuhudumia ...
0 Comments