Na Raya Hamad ….OMKR
Waziri wa Nchi
Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Mh Harusi Said Suleiman amewataka watendaji
wa ofisi hiyo kujitathmini na kujipanga upya katika utekelezaji wa majukumu yao
ya kazi ili lengo la serikali la utoaji wa huduma bora kwa wananchi liweze
kufikiwa kwa wakati.
Mh. Harusi
ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na watendaji wa Idara, Tume na Mamlaka
zilizo chini ya Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais katika mkutano wa
kujitambulisha kufuatia uteuzi wake hivin karibuni ili kuona maendeleo ya
taasisi hizo kwenye ukumbi wa mkutano Gombani Chake Chake.
Amesema ni
wajibu wake watendaji na wafanyakazi kufanya kazi kwa bidii na kufuata muongozo
wa utumishi ambapo pamoja na kujitathmini kiutendaji, kuona kipi ambacho
amekifanikisha kwa muda wa wiki nzima ambacho kimeweza kuleta tija kwa taasisi
na wananchi.
Aidha Mh. Harusi
amewaambia watendaji hao kuzidisha ari na nguvu ya kiutendaji kwa wananchi
wanaohitaji huduma na kutatua changamoto zao ukizingatia kuwa sekta za ofisi
hii ni mtambuka hivyo hawapaswi kukaa ofisini bali wajitoe kufikisha elimu na
huduma stahiki kwa wanajamii.
“watendaji
hakikisheni mnashirikiana pamoja ili wale wanaokufateni mnaowangoza nao waone
kuwa viongozi wao wapo makini na hakutakuwa na mwanya wa kufanya yaliyo sio
bali kama zipo changamoto zigeuke kuwa fursa kwa kuwa wabunifu wa mipango mipya
yenye kuleta tija “alisisitiza Bi Harusi
Mapema Mhe
Harusi alionana na Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Mh. Mattar Zahor Masoud na
kufanya mazungumzao mafupi ofisini kwake ambapo viongozi hao wote wameahidi
kushirikiana pamoja ili kufanikisha majukumu yatayoleta mafanikio ndani ya mkoa
huo kwa vile masuala yanaosimamiwa na ofisi hio yanamgusa kila mtu.
Afisa
Mdhamini wa Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Bw Ahmeid Abubakar amemuahidi
Waziri Bi Harusi kwa kushirikiana na watendaji wanahakikisha wanatekeleza
majukumu yao vyema kusimamia miradi ya maendeleo na kutekeleza Ilani ya Chama
cha Mapinduzi
Mh.Harusi
amezitembelea Idara na Mamlaka ya Usimamizi wa Mazingira, Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya, Baraza la Watu
wenye Ulemavu na Tume ya UKIMWI pia ameikaguwa miradi ya maendeleo ukiwemo Mradi
wa ujenzi wa tuta la kuzuwia maji ya chumvi yasiingie katika mashamba uliopo
Tovini
Kwengine ni
kuona mradi wa ujenzi wa Ukuta wa mawe katika fukwe ya mwambao
wa eneo la Msuka, mradi wa ujenzi wa mabwawa ya maji machafu ulipo Kichungwani,
pamoja na kufika Likoni Kojani kuangalia eneo linalotarajiwa kujengwa ukuta wa
kuzuwia mmongonyoko wa fukwe ambao pia utaunusuru mbuyu wa asili uliopo eneo
hilo ambao kwa sasa upo hatarini kuanguka
No comments:
Post a Comment