Habari za Punde

Naibu Waziri wa afya Mhe.Hassan Khamis Hafidh asisitiza utendaji kazi vituo vya afya

Naibu Waziri Wizara  ya Afya Zanzibar Mhe.Hassan Khamis Hafidh akizungumza na watendaji wa kituo cha Afya Mpendae kuhusu uwajibikaji kazini  wakati wa Ziara yake kusisitiza utendaji wa kazi na utowaji wa huduma bora kwa Wananchi,ziara hiyo ni kwa Nchi Nzima ambayo imenzia Katika  vituo vya Afya vinavyotoa huduma ya mama na mtoto vya Wilaya ya Mjini. 
Daktari dhamana kituo cha Afya Mpendae Hamad Khamis Ali akimpatia maelezo Naibu Waziri Wizara  ya Afya Zanzibar Mhe.Hassan Khamis Hafidh kuhusiana na utendaji wa kazi katika kituo hicho wakati wa ziara yake kiakazi Kusisitiza utendaji wa kazi na utowaji wa huduma bora kwa Wananchi. 
Naibu Waziri Wizara  ya Afya Zanzibar Mhe.Hassan Khamis Hafidh akisalimiana  na baba mtoto anaesuburia huduma ya  Afya ya mtoto katika kituo cha Afya Sebleni mara alipofika kituoni hapo kusisitiza utendaji wa kazi na utowaji wa huduma bora kwa Wananchi. 
Naibu Waziri Wizara  ya Afya Zanzibar Mhe.Hassan Khamis Hafidh akizungumza na wananchi wanaosubiria huduma ya Afya katika Kituo cha Afya Sebleni kuhusu changamoto zinazowakabili  wakati wa ziara yake kusisistiza utendaji wa kazi na utowaji wa huduma bora kwa Wananchi. 

Naibu Waziri Wizara  ya Afya Zanzibar Mhe.Hassan Khamis Hafidh (kushoto) akibadilishana mawazo na Naibu Mkurugenzi kitengo cha kinga na Elimu ya Afya Dkt Salim Slim wakati wa ziara ya kikazi katika vituo vya Afya kusisitiza utendaji wa kazi na utowaji wa huduma bora kwa Wananchi.

PICHA NA FAUZIA MUSSA  -MAELEZO ZANZIBAR.

 

 Na Rahima Mohamed          Maelezo          27/06/2022

Naibu Waziri wa afya Mhe.Hassan Khamis Hafidh amewataka wauguzi wanaoshughulikia miradi mbalimbali kurudi katika vituo vya afya ili kuendelea  kutoa huduma kwa  wananchi.

Hayo amesema katika ziara ya kuangalia utendaji kazi kwa vituo vya afya vinavyotoa huduma ya mama na mtoto katika kituo cha afya Mpendae na Sebleni Wilaya ya Mjini amesema kurudi kwa wauguzi hao itasaidia kuondoa usumbufu uliopo katika vituo hivyo.

Amesema amaegundua changamoto nyingi ikiwemo uchelewaji wa watendaji wa afya hali inayopelekea  wananchi kusubiri muda mrefu kupata  huduma.

 Naibu Hassan ameeleza kuwa  azma ya Serikali  ni kuwapatia wananchi huduma bora hivyo watendaji wanawajibu mkubwa wa kuhakikisha wanafanya kazi kwa bidii na kufuata sheria za kazi ili kuondosha usumbufu kwa wagonjwa wanaofika vituoni kupata huduma.

Aidha amesema Wizara haitosita kuwachukulia hatua za kisheria wale wote watakaokiuka majukumu yao na kusababisha  uzoroteshaji wa huduma hiyo ili kuepusha malalamiko kwa jamii.

Nae Naibu Mkurugenzi wa Kinga wizara ya afya Salim Slim amesisitiza  mashirikiano katika malezi kwa kina baba kuwapeleka watoto kliniki ili kujua maendeleo ya ukuaji wa afya za watoto wao.

Nao watendaji wa vituo hivyo wamesema wanakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo vipimo vya kupimia damu kwa mama wajawazito,gari ya kubebea wagonjwa wa dharura,vikalio pamoja na uhaba wa eneo hali inayopelekea wagonjwa kukaa muda mrefu kusubiria huduma wanapofika vituon hapo.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.