Habari za Punde

Visiwani Zanzibar Sasa Masumbwi Ruhsa

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe.Hemed Suleiman Abdulla akiwa na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar wakifurahia kwa kupitishwa kwa mchezo wa ngumi Zanzibar. wakiwa nje ya ukumbi wa Kikao, baada ya kupitishwa jana 30-9-2022.   
Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mhe.Zuberi Ali Maulid akiwa na glavu za kupigania mchezo wa ngumi wakifurahia kupitishwa kwa mchezo huo wa ngumi Zanzibar na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar wakati wa Kikao cha Baraza la Wawakilisha jana 30-9-2022.


Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi  Zanzibar  leo (30/09/2020) wamebariki  kuruhusiwa Michezo ya Ngumi  kupitia hoja iliyotolewa na Waziri  wa Habari,  Vijana, Utamaduni na Michezo  Mhe. Tabia  Maulid Mwita.

Wakichangia hoja hiyo, katika kikao cha Baraza huko Chukwani, wajumbe hao  waliipongeza Wizara inayoshughulikia michezo kwa kulisimamia  jambo hilo ambalo limewahi kuwasilishwa katika vikao  vya  Baraza lilivyopita.

Akiwasilisha hoja hiyo Mhe. Tabia alisema  mijadala mbali mbali  imeendeshwa kwenye  vikao vya wadau wa michezo, vyombo vya habari na hata wananchi walithubutu  kwenda kwenye Baraza la  Taifa la Michezo kudai kuwepo kwa mchezo huo.

Aliongeza kuwa, katika kikao cha  Baraza la Wawakilishi cha mwaka 2021, Mheshimiwa Hemed Suleiman Abdulla, Makamo wa Pili wa Rais ambae ndio Kiongozi wa Serikali ndani ya Baraza la Wawakilishi aliliahidi Baraza la Wawakilishi kuwa Serikali itakusanya maoni ya wananchi juu ya michezo hiyo ili baadae taarifa ya maoni hayo iwasilishwe kwenye kikao cha Baraza hilo.


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.