Habari za Punde

Wakulima Iringa wampongeza Rais Samia

 


Mkuu wa mkoa wa Iringa Halima Dendego akiongea na wakulima waliofika ofisi kwake kwa ajili ya kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kwa kuboresha sekta ya Kilimo.

Baadhi ya wakulima waliofika ofisi kwa mkuu wa mkoa wa Iringa Halima Dendego kwa ajili ya kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kwa kuboresha sekta ya Kilimo
Baadhi ya wakulima waliofika ofisi kwa mkuu wa mkoa wa Iringa Halima Dendego kwa ajili ya kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kwa kuboresha sekta ya Kilimo.



Na Fredy Mgunda, Iringa.


WAKULIMA mkoa wa Iringa  wamefanya matembezi ya  kumpongeza Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania  Samia Suluhu Hassan kwa kuwapunguzia bei ya mbolea.

Wakizungumza Mbele ya Mkuu wa mkoa wa Iringa,wakulima hao wamesema kuwa  walikuwa wakinunua mbolea kwa shilingi  150,000 lakini sasa wananunua kwa shilingi  60,000  hadi 70000

“Tunampongeza na kumshukuru sana rais samia kwa kutuona sisi wakulima kwa sababu mwanzo tulikuwa tukinunua mbolea kwa laki moja elfu thelathini lakini saizi tunapata kwa elfu 60000 hadi sabini ni hatua nzuri tunampongeza mama na sasa tunaamini kila mwananchi wetu atalima"walisema

Akisoma risala Mbele ya Mkuu wa mkoa wa Iringa Abeid Kiponza alisema kuwa  wana kila sababu ya kumpongeza Rais Samia kutokana na kupunguza gharama za pembejeo za kilimo hususani upande wa mbolea

 “sisi wakulima wa mkoa wa Iringa tumefanya matembezi maalumu ya kumshukuru na kumpongeza mheshimiwa rais kutokana  na upendo wake kwetu kutokana na mambop makubwa anayoendelea kutufanyia kwenye kilimo tanzania nzima inajua wakulima wa nyanda za juu kusini tumekuwa tukizalisha viazi,mahindi,ngano,alizeti na mazao mengine ya chakula na hatuwezi zalisha mazo vizuri bila kuungwa mkono na serikali na tumwambie usiwasikilize wanasiasa ambao wamekuwa kama wasemaji wetu wakati sio wasemaji wetu usiwasikilize"alisema

Kwa upande wake Mkuu wa mkoa wa Iringa Mhe. Halima Dendego amesema kuwa  Serikali ya awamu ya sita imeamua kutatua matatizo ya msingi kwa kuwekeza kwenye kilimo na miradi umwagiliaji.

“Sisi wote ni mashuhuda mheshimiwa rasi ameweza kutoa pikip[iki kwa maafisa ugani wote na wanatakiwa wahikikishe wanafika kama kuna maswali muulize wawahudumie nyinyi na zimetoka billion 55 mradi wa pawaga umwagiliaji kwa hiyo tunaposema mama ameupiga mwingi na ametuletea ruzuku ambayo ndio tunategemea sisi wakulima"

Hata hivyo lengo la serikali ya Rais Samia Suluhu  awamu ya sita ni kuhakikisha inaboresha sekta ya kilimo na maslahi ya wakulima kwa ujumla.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.