Habari za Punde

Mchezaji Nguli wa Brazil Pele Amefariki Dunia

Nyota wa zamani wa timu ya Taifa ya Brazili na klabu ya Santos FC, Edson Arantes do Nascimento maarufu kama Pele amefariki Dunia mara baada ya kusumbuliwa na saratani kwa muda mrefu mpaka kufikia kulazwa hospitali hivi karibuni.

Ripoti ya utabibu kabla ya Krismasi ilionyesha alihitaji uangalizi kwa ajili ya ugonjwa wa Moyo na Figo, na amekuwa akipambana na Saratani ya Utumbo tangu Septemba 2021
 
Pele ambaye alitajwa kama mchezaji bora wa karne ya 21, enzi za uchezaji wake alifanikiwa kushinda mataji matatu ya Kombe la Dunia akiwa na timu ya taifa ya Brazil.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.