Habari za Punde

Kikao cha wajumbe wa Kikosi Kazi cha Utekelezaji wa Mpango wa Kutokomeza Kipindupindu Zanzibar

Mratibu wa Mpango wa Kutokomeza Kipindupindu Zanzibar Makame Ame Simai akiwasilisha muhtasari wa ufuatiliaji na  utekelezaji  wa kutokomeza  kipindupindu katika ukumbi wa Kamisheni ya Kukabiliana na Maafa, Maruhubi Januari 27,2023 .
Wajumbe wa  Kikosi Kazi cha  Utekelezaji wa Mpango wa Kutokomeza Kipindupindu Zanzibar (ZACCEP) wakimsikiliza Katibu wa Mpango Makame Khatibu Makame (hayupo pichani) huko katika ukumbi wa Kamisheni ya Kukabiliana na Maafa, Maruhubi Januari 27,2023.

Na Khadija Khamis -Maelezo Zanzibar,27/01/2023.

 

Katibu wa Kikosi Kazi cha  Utekelezaji wa Mpango wa Kutokomeza Kipindupindu Zanzibar(ZACCEP,)  ambae pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa kukabiliana na Maafa Zanzibar Makame Khatibu Makame  amewataka watendaji  kutekeleza majukumu yao kiufanisi ili kufikia lengo lililokusudiwa.

 

Hayo ameyaeleza huko Kamisheni ya kukabiliana na Maafa Maruhubi alipokuwa akizungumza na wajumbe wa Kikao  kazi cha Mpango wa Kutokomeza Kipindupindu Zanzibar wakati wa uwasilishaji wa ripoti ya  miezi mitatu  Oktoba hadi Disemba 2022..

 

Amesema kila Mjumbe anaewakilisha Taasisi yake iliyomo kwenye mpango huo ni vyema kusimamia  utekelezaji wa majukumu na kuwasilisha ripoti ili kuonyesha  maendeleo na changamoto zilizopo  .

 

Alifahamisha kuwa iwapo wajumbe hao  watafanyakazi kwa mashirikiano na bidii kutasaidia kufikia malengo yaliyotarajiwa kuliko kufanyakazi Kwa mazowea,

 

Alieleza kuwa bado kumekuwa na mazingira machafu Katika baadhi ya  maeneo mbali mbali ya Zanzibar jambo ambalo ni hatarishi kwa kusababisha mripuko wa maradhi ya kipindupindu.hivyo aliagiza Taasisi husika kuchukuwa hatua stahiki kusimamia

 

"Kwani hatuwezi kudhibiti taka ikawa mfano kama Arusha na Moshi isiwe kila siku sisi tunakwenda kujifunza kwao ," Alisema Katibu huyo.

 

Nae Mratibu wa Mpango wa Kutokomeza Kipindupindu Zanzibar Makame Ame Simai  ameeleza changamoto mbali mbali zilizojitokeza  kwenye utekelezaji wa Mpango wa kipindi cha Mwaka mmoja uliopita ambao ulitekelezwa na Taasisi  mbali mbali zilizomo katika mpango .

 

Aidha alisema changamoto zilizojitokeza katika utekelezaji wa mpango huo  ni kukauka kwa visima 32 vilivyosababishwa na mabadiliko ya  hali ya hewa wakati wa kiangazi pamoja na kukosekana kwa gari ya kusafirishia maji taka hasa kwa upande wa Pemba na sehemu husika ya kumwagia maji hayo.

 

  Nae Mjumbe kutoka Manispaa ya Magharibi ‘B’ Yussuf Mati Ali amesema wameondoa majaa mbali mbali ambayo sio rasmi katika maeneo  ya kivigo Mwanakwerekwe, Taveta, ,Magirisi pamoja na Magereza na kusafisha mitaro ya kombeni, mazizini na mwanakwerekwe.

 

Vile vile alisema wamefanya ukaguzi kwa wafanyabiashara wa mikahawa 83 na mamalishe 50 kwa upande wa wilaya ya magharibi ‘B’ na baadhi  walifungiwa na wengine kutoleshwa faini ya papo kwa papo.

 

Kwa upande wa wajumbe wametoa ushauri wa kuongezawa  mjumbe kutoka shirika la umeme ili kuongeza  nguvu katika uendeshaji wa visima vya maji kutokana na upungufu wa umeme hasa unapokuwa mdogo husababisha kuunguza mashine pamoja na kushindwa kusambaza maji katika maeneo mbali mbali .

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.