Habari za Punde

Mafunzo ya Vijana ya Uongozi na usimamizi wa fedha ukumbi wa Skuli ya John Magufuli Mwanakwerekwe

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya amali Zanzibar Khamis Abdalla Khamis akifungua mafunzo ya Uongozi  na usimamizi wa fedha katika ukumbi wa Skuli ya John  Magufuli Mwanakwerekwe Wilaya ya Magharibi “B”,( 'Januari 26,2023 kulia) Katibu Mtendaji wa Baraza la Vijana Zanzibar Salum Issa Ameir.
 Baadhi ya Vijana walishiriki  mafunzo ya Uongozi  na usimamizi wa fedha, wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Khamis Abdalla Khamis  (hayupo pichani) katika ukumbi wa Skuli ya John  Magufuli Mwanakwerekwe Wilaya ya Magharibi “B” Januari 26,2023
 Katibu Mtendaji wa Baraza la Vijana Zanzibar  Salum Issa Ameir  (wa kwanza kulia ), (kati) Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Khamis Abdalla Khamis,( kushoto) aliyevaa suti rangi ya jivujivu Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa Sensa ya Filamu na Utamaduni Zanzibar Dkt. Omar  Abdalla Adam wakipongeza mara baada ya  ufunguzi wa mafunzo ya Uongozi  na usimamizi wa fedha huko ukumbi wa Skuli ya John  Magufuli Mwanakwerekwe Wilaya ya Magharib “B” Januari 26,2023 
Mmoja kati ya Washiriki  akitoa neno la shukrani  kwa Mgeni rasmin katika hafla ya  ufunguzi wa mafunzo ya Uongozi  na usimamizi wa fedha, huko ukumbi wa Skuli ya John Magufuli Mwanakwerekwe Wilaya ya Magharibi “B” Januari 26,2023

Mkufunzi  Ramadhan Khamis Ramadhan  akitoa mada kwa Vijana  waliofika katika ufunguzi wa mafunzo ya Uongozi na usimamizi wa fedha, huko ukumbi wa Skuli ya John  Magufuli Mwanakwerekwe Wilaya ya Magharibi “B” Januari 26,2023.

            Picha na Miza Othman BTMZ.

Na Khadija Khamis – Maelezo , 26.01.2023.

 

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Khamis Abdalla Khamis amewataka vijana kuanzisha miradi yenye kuleta tija ili kujiajiri.

 

Aliyasema hayo katika Ukumbi wa Skuli ya John Magufuli Mwanakwerekwe,Wilaya ya Magharibi 'B'

wakati wa Mafunzo ya Mabaraza ya  Vijana  kwa Wilaya saba za Unguja .

 

Amesema iko haja kwa vijana kuandaa miradi mbalimbali na kuisimamia kwa uaminifu na uandilifu katika utekelezaji wa miradi hiyo ili kuleta tija na kufikia malengo waliyokusudia

 

Aidha alifahamisha kuwa Mafunzo yanayotolewa Kwa vijana hao ni Uongozi na usimamizi wa Fedha ,Utalii na Uwandishi wa Miradi Usimamizi na Uendeshaji wa Miraadi  ni utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi ya Mwaka 2020 hadi 2025 Ibara ya 210 (C). 

 

Nae Katibu Mtendaji wa Baraza la Vijana Zanzibar Salim Issa Ameir amewafahamisha vijana kuwa wabunifu kwa kuandaa miradi kulingana na mahitaji ya sehemu husika ili kuleta mafanikio na kupata soko .

 

Alisisitiza kwamba pindi vijana wakipatiwa Fedha za miradi  kuwa wazalendo Kwa kuzisimamia na kutoa ripoti za uingiaji na utokaji wa fedha hizo ili kuleta maendeleo ya utekelezaji  pamoja na kubainisha changamoto zinazojitokeza

 

Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa, Sensa, Filamu na Utamaduni  (BASSFU) Dkt.Omar Abdalla Adam amewasisitiza Vijana kuwa makini katika kuisimamia raslimali Fedha za miradi ambazo zinazotoka serikalini na  wafadhili ili kuleta tija na kuzifikia ndoto walijiwekea.

 

Kwa upande wa Afisa Mipango Muandamizi Ramadhan Khamis Ramadhan akitoa mada kuhusiana na namna  ya kuandaa miradi na njia bora za utekelezaji wa miradi hiyo.

 

 Alifahamisha jinsi ya kuratibu na kuisimamia pamoja  na kujipangia malengo ya baadae ya miradi ili kuleta maendelo na kufikia matarajio 

 

Mafunzo ni ya siku moja yaliyowashirikisha zaidi ya Vijana 200 wa Wilaya saba za Unguja ambayo  yameandaliwa na Baraza la Vijana Zanzibar.

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.