Habari za Punde

Mhe Othman akutana na Balozi Mdogo wa Nchi za Falme za Kiarabu - UAE

 

 IMEELEZWA kwamba zipo fursa nyingi za kiuchumi na uwekezaji zinazoweza kutumika kwa ushirikiano na kuchangia kuleta maendeleo  makubwa kati ya Zanzibar na nchi za Falme za Kiarabu (UAE).

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman ameyasema hayo Ofisini kwake Migombani mjini Zanzibar alipokutana na  kuzungunza na Balozi Mdogo wa Nchi za Falme za Kiarabu Bw. `Saleh Alhemeiri kuhusiana na ushirikiano katika maeneo mbali mbali ya kiuchumi na kijamii.

Mhe. Othman amesema kwamba nchi kwa kuwa zinao uhusiano mkubwa wa kijamii hivyo fursa za mashirikiano katika maeneo ya uchumi, wa bluu , utamaduni, uvuvi, Kilimo na biashara katika sekta ya huduma ya usafiri wa Anga.

Amefahamisha kwamba Zanzibar inaweza kuutumia na kufaidika na uzoefu mkubwa uliopo katika nchi hizo  ili kusaidia pamoja na mambo mengine kujenga uwezo wa Zanzibar katika maeneo mbali mbali  kwenye sekta hizo na kuweza kuwa na tijha kubwa kimaendeleo.

Ameongeza kwamba sekta ya uchukuzi wa anga hivi sasa inamuelekeo wa kuwa sekta kubwa na tegemeo muhimu la kiuchumi inayoweza kusaidia Zanzibar kuweza kupiga hatua kimaendeleo.

Naye Balozi Mdogo wa UAE Bw. `Saleh Alhemeiri, asmesema kwamba UAE ipo  tayari kuisaidia Zanzibar katika maeneo mbali mbali ya sekta hizo ili kuendelea kujenga uhusiano wa muda mrefu uliopo kati ya nchi hizo mbili.

Amesema kwamba nchi hiyo wanaweza kusaidia pia kutoa mafunzo kwa vijana kutoka Zanzibar ili kuisaidia Zanzibar kuwa kituo muhimu katika sekta ya huduma ya usafiri wa Anga.

Wakati huo huo Mhe. Othman amekutana na ujumbe Watendaji wa Taasisi kutoka Ofisi ya Rais ya Ufuatiliaji ,usimamizi wa Utendaji Serikalini na kuwaeleza kwamba taasisi hiyo inakazi kubwa ya kusaidia kunyanyua na kutimiza matumaini ya wananchi hasa wanyonge kwa  kuwepo na kuimarika utolewaji wa huduma za kijamii kama matarajio ya wananchi yalivyo.

Mhe. Makamu amesema kwamba Taaisi hiyo ni nyenzo muhimu katika kufikia matarajio ya kweli na matumaini mazuri ya wananchi iwapo watendaji hao wataangalia, kuanisha na kuyafanyia kazi maeneo mbali mbali muhimu yatakayosaidia kunyanyua uchumi na maendeleo ya  Z          anzibar.

Amefahamisha kwamba yapo maeneo mengi yanayohitaji kufanyiwa kazi ili kusaidia ipasavyo  nchi katika kunyanyua matumaini na matarajio ya wananchi wa Zanzibar hasa kwenye kufikia upatikanaji wa huduma bora za kijamii na maendeleo kwa jumla.

Naye Kiongozi wa  ujumbe huo ambaye ni naibu mtendaji Mkuu wa Taaisi hizi Ndugu Josphine Kimaro amesema kwamba taasisi hiyo imeundwa katika kusaidia utekelezaji wenye tija kwa maeneo ya vipaumbele vya maendeleo vilivyowekwa na serikali ikiwemo uchumi wa bluu, miundombinu,huduma za jamii kama afya , umeme na maji  sambamba na kuwafahamisha wananchi kuhudu juhudi za serikali kwenye hatua za utekelezaji wa mambo mbali mbali yalivyopfikiwa.


Imetolewa na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar kupitia Kitengo chake cha Habari leo tarehe 18.01.2023.    

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.