RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,
Dk. Hussein Ali Mwinyi ameahidi kushirikiana na
ofisi ya Haki za binadamu katika kuendeleza ushirikiano wao.
Alisema Zanzibar inafurahia kushirikiano uliopo baina yao na kuendeleza masuala
mbalimbali ya sheria na haki za binaadamu ili kujenga uelewa mpana kwa jamii.
Dk. Mwinyi aliyasema hayo Ikulu, Zanzibar
alipozungumza na Mwakilishi na Mkurugenzi wa Ofisi ya Kamishna Mkuu wa
Haki za Binaadam Kanda ya Afrika Mashariki na Umoja wa Afrika, Bw. Marcel
Akpovo aliyemtembelea.
Alisema Zanzibar kama sehemu ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ina maeneo mengi inayofanyakazi na
kutelekeza haki za binadamu ikiwemo, mahakama, ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka,
Jeshi la polisi na taasisi nyengine za sheria.
Alisema
ushirikiano baina Serikali na ofisi hiyo ya kimataifa unasadifu adhma ya
taasisi za sheria zilizopo nchini.
Aidha, Rais
Dk. Mwinyi aliiomba taasisi hiyo kuangalia uwezekano wa kuzisaidia taasisi za
Serikali zinazofanyakazi na kutekeleza masuala ya sheria kwa kuwajengea uwezo
kwenye maeneo wanayoyatumikia ikiwemo mafunzo ya muda mfupi na mrefu, warsha na
masuala yatakayowajengea ufanisi na kuwaongezea weledi kwenye majukumu yao ya
kila siku.
Alieleza Zanzibar
inafanyakazi chini ya mwamvuli wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania licha ya
baadhi ya taasisi hizo za Sheria kila moja ikijitegemea kwa mujibu wa maumbile
ya upande inakotokea lakini pande zote mbili za Muungano zinashirikiana moja
kwa moja kufanikisha wajibu wao wa kuwatumikia Watanzania wote.
Hata hivyo,
Dk. Mwinyi alitumia fursa hiyo kumtaka Mwakilishi huyo kuitumia vyema Zanzibar
sio kwa utalii pekee bali kuichagua hata kwa mikutano na makongamano yao ya
kimataifa kwani Zanzibar ina kumbi kubwa za mikutano ya kimataifa na vitutio
vizuri kwa wageni.
Kwaupande
wake Bw. Marcel
Akpovo alimuambia Rais Dk. Mwinyi kwamba Ofisi yao
inaungamkono juhudi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ya kuwatumikia watu
wake na kuwaletea maendeleo makubwa.
Alisema ofisi
yao pia ina imani kubwa na Serikali na kwamba ushirikiano wao utaleta mafanikio
zaidi kwa watu wa pande zote anazoziwakilisha nakuongeza kuwa, ujio wake kwa
Zanzibar mbali na kuonana na Serikali ya awamu ya nane lakini kuimarisha
ushirikiano wao.
Marcel ambae ni raia wa Bennin huko Afrika Magharibi, alimuahidi Dk. Mwinyi
kwamba taasisi yao watafanyakazi bega kwa bega katika kuiunga mkono Serikali
pamoja na kushirikiana kwenye masuala ya sheria na taasisi za sheria zilizopo
nchini.
Alieleza taasisi yake itashirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
kwa kutoa mafunzo kwa Makahimu, Majaji, Mawakili, Ofisi ya Mkurugenzi wa
Mashtaka na taasisi za sheria zilizopo Zanzibar.
Alisema moja ya majukumu ya ofisi yao ni kuitangaza na kuungamkono
kampeni ya kimataifa ya “Haki za wanawake na masuala ya jinsia” kwa kutekeleza
wajibu wa haki za kila mtu kwenye jamii na kuendelea kuhamasisha.
Alisema
Tanzaia ni nchi ambayo wameendeleza zaidi urafiki nakueleza kwamba wanaufurahia
uhusiano mzuri uliopo baina ya taasisi yao na Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania
ambao aliusifu ni Muungano wenye baraka na kuimarisha amani, upendo na
mafanikio makubwa ya watu wa pande mbili hizo.
“Uhusiano
wetu tulionao unaakisi maumbile halisi ya Muungano wa watu wa pande mbili za taifa
hili la Tanzania” alisifu mgeni huyo.
Alisema lengo
la ujio wao kwa Zaznzibar ni kuona kwa kiasi gani wataungamoko kwenye masuala
upatikanaji wa haki kwa Zanzibar na maeneo yanayohusiana na hayo
Bw. Marcel Akpovo
anatekeleza wajibu wake kwa mataifa ya Djibuti, Erictria, Ethiopia, Kenya,
Sudan, Somali, South Sudan, Tanzania na Uganda.
IDARA YA MAWASILINO, IKULU ZANZIBAR
No comments:
Post a Comment